Afyaclass

Afyaclass Dr.Ombeni Mkumbwa:
Ushauri|Tiba|Afya🩺💊🌡️🏅
Call,Sms,Whatsapp+255758286584|
Pia Whatsapp Channel|Link📲👇

Dalili zifuatazo za ugonjwa huu wa ngozi hutokea kwa watu wazima:- vipele ambavyo vina magamba zaidi kuliko vinavyotokea...
28/10/2025

Dalili zifuatazo za ugonjwa huu wa ngozi hutokea kwa watu wazima:

- vipele ambavyo vina magamba zaidi kuliko vinavyotokea kwa watoto

- vipele ambavyo kwa kawaida huonekana kwenye mikunjo ya viwiko au magoti au sehemu ya shingo.

- vipele vinavyofunika sehemu kubwa ya mwili

- ngozi kuwa kavu sana kwenye maeneo yaliyoathirika

- vipele ambavyo huwashwa sana n.k

Je,Una tatizo hilo na hujapata Tiba,Kwa Ushauri zaidi na Tiba tuwasiliane +255758286584.

Moja ya Saratani ambayo husababishwa na Uvutaji wa Sigara kwa kiwango kikubwa ni Saratani ya Mapafu(Lung Cancer). Epuka ...
27/10/2025

Moja ya Saratani ambayo husababishwa na Uvutaji wa Sigara kwa kiwango kikubwa ni Saratani ya Mapafu(Lung Cancer). Epuka Uvutaji wa Sigara kwa ajili ya afya yako..

1.Kunywa maji ya Kutosha kila Siku2.Pata Muda wa kutosha wa kulala3.Fanya mazoezi mepesi ya mwili4.Punguza mawazo kwa ku...
22/10/2025

1.Kunywa maji ya Kutosha kila Siku
2.Pata Muda wa kutosha wa kulala
3.Fanya mazoezi mepesi ya mwili
4.Punguza mawazo kwa kufanya vitu uvipendavyo
5.Fanya Vipimo kama bado hali inaendelea.

Kujisaidia Kinyesi Chenye Damu,Sababu na cha kufanya:1.Ugonjwa wa Bawasiri2. Michubuko au Majeraha Sehemu ya haja kubwa3...
21/10/2025

Kujisaidia Kinyesi Chenye Damu,Sababu na cha kufanya:

1.Ugonjwa wa Bawasiri

2. Michubuko au Majeraha Sehemu ya haja kubwa

3. Vidonda kwenye Utumbo Mpana

4. Vidonda vya Tumbo

5. Maambukizi kwenye Utumbo

Maambukizi kutoka kwa bakteria (kama Shigella, E. coli), virusi au vimelea kama amiba (amoeba).huweza pia kusababisha hali hii.

NB: Cha kufanya: Ukiona Hali hii ;

- Usitumie Dawa yoyote pasipo maelekezo kutoka kwa Wataalam wa afya

hakikisha unaongea na Wataalam wa afya kwa Ushauri na Msaada wa Tiba.

- Kunywa maji mengi na vyakula vya nyuzi nyuzi zaidi,hasa ikiwa unapata Choo kigumu

-Lakini pia kwa Ushauri Zaidi,elimu na Tiba tunaweza kuwasiliana +255758286584.....

Chukua hatua hizi haraka Ukikabwa na mwiba wa samakiZipo njia mbali mbali ambazo wataalam wa afya hushauri ukiwa kwenye ...
18/10/2025

Chukua hatua hizi haraka Ukikabwa na mwiba wa samaki

Zipo njia mbali mbali ambazo wataalam wa afya hushauri ukiwa kwenye hali hii;

'Ikiwa mfupa wa samaki utakwama kwenye koo,

Bonyeza kwa nguvu tumbo. Hii itasaidia mfupa kutoka pamoja na hewa.

Pia Inasaidia kunywa soda mara kwa mara. Gesi iliyo kwenye soda huweka shinikizo kwenye koo, ambayo husababisha mwiba kutoka.

Ikiwa tiba hizi za nyumbani hazisaidii, unapaswa kushauriana na daktari mara moja.

Onyo:
Ingawa ni nadra sana kutokea,lakini tafiti zinaonyesha mfupa wa samaki pia unaweza kusababisha maambukizi. mfano;maambukizi ya ngozi(osteomyelitis),maambukizi ya mifupa au septicemia (maambukizi ya damu) .

Lakini haya hutokea tu katika matukio machache Sana......

Unafahamu kuwa 'Love Bite' inaweza kusababisha kiharusi?Love Bite, au alama nyekundu inayotokana na busu kali kwenye ngo...
16/10/2025

Unafahamu kuwa 'Love Bite' inaweza kusababisha kiharusi?

Love Bite, au alama nyekundu inayotokana na busu kali kwenye ngozi huzingatiwa kama ishara ya mapenzi, mara nyingi huwekwa shingoni na alama hii inabaki mwilini kwa muda.

Lakini je, unafahamu kwamba Love Bite ambayo ni alama ya busu inayobaki shingoni inaweza kusababisha tatizo kubwa la kiafya la kiharusi?

Mnamo mwaka 2010, madaktari nchini New Zealand waliripoti kisa cha mwanamke mwenye umri wa miaka 44 aliyepata kiharusi,baada ya kupata Ripoti hiyo ilieleza kuwa alama ile iligandisha damu kwenye mshipa wa carotid na kusababisha kuziba kwa mtiririko wa damu kwenda kwenye ubongo. Mwanamke huyo alipata ganzi upande mmoja wa mwili, dalili kuu ya kiharusi.

Vilevile, mwaka 2014, Jarida la Matibabu la Denmark lilichapisha ripoti ya kisa kingine cha mgonjwa aliyepata kiharusi kutokana na Love Bite. Wataalamu walieleza kuwa ingawa visa hivi ni nadra, vinaonyesha ukweli kwamba msukumo wa nguvu kwenye mishipa mikubwa ya damu unaweza kuchochea kuganda kwa damu na kuathiri ubongo.

Source:DW

Viazi vitamu vina beta-carotene, ambayo mwili hubadilisha kuwa vitamini A.Hii husaidia:-Kuimarisha macho-Kuboresha kinga...
16/10/2025

Viazi vitamu vina beta-carotene, ambayo mwili hubadilisha kuwa vitamini A.

Hii husaidia:

-Kuimarisha macho

-Kuboresha kinga ya mwili

-Kusaidia ukuaji wa seli

Unachopaswa kufanya baada ya mtoto kumeza Sarafu:1. Kwanza, tulia na tathmini hali ya mtoto Angalia kama mtoto:Anapumua ...
16/10/2025

Unachopaswa kufanya baada ya mtoto kumeza Sarafu:
1. Kwanza, tulia na tathmini hali ya mtoto Angalia kama mtoto:Anapumua vizuri,Hana kikohozi kikali,Hana kichefuchefu au kutapika,Anaongea au kulia kawaida.
Ikiwa anapumua vizuri na hana maumivu, sarafu inaweza kuwa imeingia tumboni, na mara nyingi hutoka yenyewe kupitia choo ndani ya siku 2–3.

2. Lakini ikiwa:
Mtoto anashindwa kupumua,Ana kikohozi kikali au damu,Ana maumivu ya kifua,shingo au tumbo,Anatapika,Au anaonekana kulegea,Wahi hospital

Hali hii hujulikana kama Genital Warts na Chanzo cha tatizo hili ni maambukizi ya Kirusi kinachoitwa Human Papilloma Vir...
01/10/2025

Hali hii hujulikana kama Genital Warts na Chanzo cha tatizo hili ni maambukizi ya Kirusi kinachoitwa Human Papilloma Virus(HPV), Haya ni Miongoni mwa maambukizi ambayo unaweza kuyapata wakati wa kujamiiana(Sexual transmitted Infection).

Sababu ya pua kushindwa kujua harufu yoyote,hali ambayo huitwa anosmia (kupoteza uwezo wa kunusa). Inaweza kusababishwa ...
15/09/2025

Sababu ya pua kushindwa kujua harufu yoyote,hali ambayo huitwa anosmia (kupoteza uwezo wa kunusa). Inaweza kusababishwa na mambo mbalimbali, ikiwemo:

1. Magonjwa ya pua na njia ya hewa kwa ujumla

Kuwa na Mafua

Sinusitis (uvimbe kwenye sinus)

Pumu ya pua (allergic rhinitis)

Uvimbe au polyps ndani ya pua

2. Magonjwa ya mfumo wa neva

Uharibifu wa olfactory nerve (neva inayosafirisha taarifa ya harufu kutoka puani kwenda kwenye ubongo)

Magonjwa ya ubongo kama Alzheimer’s disease, Parkinson’s disease, au multiple sclerosis

3. Majeraha

Kupigwa kichwani (traumatic brain injury) ambayo huathiri sehemu ya ubongo inayohusika na kunusa

Kuumia ndani ya pua n.k.

Je,Unatatizo hili na hujapata Tiba? Kwa Ushauri Zaidi&Tiba tuwasiliane +255758286584.

Address

Dar Es Salaam
00000

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afyaclass posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram