05/03/2026
Tatizo la upevukaji wa mayai (Premature Ovarian Failure) hutokea pale ambapo vifuko vya mayai huacha kufanya kazi ipasavyo kabla ya mwanamke kufikisha miaka 40. Vifuko vya mayai hushindwa kuzalisha homoni ya 'Estrogen' kwa kiwango kinachostahiki hata k**a mwili unatoa homoni za kuchochea mayai kwa kiwango cha juu (FLH). Matatizo ya vinasaba ni moja ya sababu ya kurithi, hali isiyo ya kawaida kwa mwanamke, ambayo pia inaweza kuongeza hatari ya kupata saratani ya mayai.
Dalili ni mwanamke kukosa hedhi kabisa (amenorrhea) au hedhi zisizo za kawaida, mifupa kuwa dhaifu (osteoporosis), ukavu wa uke (atrophic vaginitis) na kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa.