18/02/2026
FAHAMU KUHUSU MTOTO WA JICHO (CATARACTS).
Mtoto wa jicho ni ugonjwa wa macho ambao hutokea baada ya lenzi ya jicho kupata ukungu na kusababisha jicho husika kupunguza au kupoteza uwezo wa kuona.
Hali hii hutokea taratibu sana na inaweza kuathiri jicho moja au macho yote mawili.
Mtoto wa jicho huwapata zaidi wazee kwa sababu ya umri mkubwa , lakini pia unaweza kupata mtoto wa jicho kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo;
1. Kuumia jicho.
2. Kupigwa na mionzi.
3. Upasuaji wa jicho kwa sababu ya matibabu.
4. Kurithi (kuzaliwa ukiwa na mtoto wa jicho).
Mtu yeyote anaweza kupata mtoto wa jicho , lakini baadhi ya watu wapo kwenye hatari zaidi, wakiwemo.
1. Wagonjwa wa KISUKARI
2. Wavutaji wa sigara.
3. Wanywaji wa pombe.
4. Kupigwa na mionzi ya jua kwa muda mrefu.
Dalili zifuatazo humpata mtu mwenye mtoto wa jicho,
1. Kuona taswira zenye rangi zilizofifia.
2. Uoni hafifu.
3. Kuona taswira mbili kwa kitu kimoja.
4. Kupata shida kuangalia vitu vya kung'aa.
5. Kupata shida ya kuona wakati wa usiku.
MATIBABU.
K**a wewe au ndugu yako ana tatizo la mtoto wa jicho,hakuna haja ya kuwa na mashaka wala hofu. Tatizo hili linatiba.