team weupe sweger

team weupe sweger Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from team weupe sweger, Dar es Salaam.

Mambo zenu guys
14/03/2023

Mambo zenu guys

10/10/2020

SIMULIZI FUPI: NITARUDI
MTUNZI: JACOB NZOWA
MWANDISHI: JMB 23
MWAKA: 2020
MAWASILIANO: 0716579834

******* KWENYE MAISHA JITAHIDI SANA KUWA NA MSIMAMO KATIKA MAMBO YAKO, SIYO YOTE YANAYOSEMWA AU KUFANYIWA NA FULANI NAWE UYAFANYE AU UYAFATISHE.... KWA MAANA HATA WASWAHILI WALISEMA “ MIRUZI MINGI HUMPOTEZA MBWA”**

Mbele ya nyumba moja ya kifahari alionekana bwana mmoja mbele ya nyuma akiwa amezunguukwa na watu k**a wanne wakiwa na vifaa maalumu vya kuandikia wakiwemo na polisi wakiwa na pingu, huku kwengine walijazana majilani kushuhudia lile tukio.

Yule bwana alitambulika kwa jina la SUDI alionekana kuomba wampe hata wiki mbili aweze kuwalipa wale mabwana maana biashara yake haikuenda vizuri kwaiyo izo week mbili anaweza akapata hela yake na kuwalipa, lakini kwa upande wa pili anao waomba msamaha hawakuwa na mda nae, wakampa amri moja tu.

~ unaondoka au huondoki~

~ naondoka~ alijibu bwana sudi huku mkewe akiwa anaangalia tu hakuwa na lakufanya wala kuongea.

~ tunakupa dakika 10 uwe ushatoa mabegi yako ya nguo na usichukue kingine chochote~

sudi hakuamini aliachoambiwa lakini ndio hivyo haikuwa ndoto akaenda ndani na mkewe wakachukua nguo zao, kwa bahati nzuri sadi alikua na vijisenti vyake akavihifadhi na kutoka zao nje na mkewe, wale mabwana wakafanya mnada ile nyuma, lilikua jumba kubwa la kifahari.

Sudi na mkewe wakaondoka huku wakiangalia ile nyumba kwa mara ya mwisho mwisho, majilani waliwafariji lakini haikuleta faida yoyote wakaamua kujiondokea zao wakiwa njiani mkewe akambadilikia kibao mumewe, na kumwambia awezi kwenda kuishi maisha magumu kijiji kwaiyo amuache aende kijijini peke ake siku akipata hela atamfata.

Sudi alishangazwa na kauli ya mkewe akataka kumfokea nae mkewe akapandisha kibesi akaona isiwe tabu sudi akakubaliana na matokeo maana mdau huo alikua kashachanganyikiwa, akapanda kibajaji hadi stendi na kupanda gari la kijijini kwao.

Kwa upande wa mkewe nae akachukua simu yake na kumpigia hawala wake baada ya dakika kadhaa alifika na gari wakaondoka zao.

Sudi baada ya masaa kadha mida ya usiku alikua kijijini kwao, wazazi wake walimpokea kwa upendo wote na kumuasa kuwa aachane na mwanamke maana anaweza kumsababishia matatizo makubwa zaidi ya yale, bwana sadi aliweza kusikiliza ushauri wa wazazi wake lakini kwenye fikra zake alizidi kumkumbuka Yule mwanamke wake aliyebarikiwa sura nzuri na shepu namba nane,

lakini muda mwingine roho ilimuuma maana yeye ndiye chanzo cha yote kufilisika kwake hadi nyumba yake kupigwa mnada, akabaki kumshukuru Mungu.

Miaka ikaanza kwenda, mwaka wa kwanza , wa pili , watatu sudi akasahau kabisa kuhusu mkewe , akapata kibarua cha kuendesha tax ya mtu,biashara ile ya tax ilimkubali sana na alifahamika sana kwa jina la SUDI BISHOO maana alikua smart sana akinukia manukato mazuri mda wote.

Siku moja mida ya saa tatu alipata abilia wak**e akiwa amepaka MARASHI yenye harufu kali sana, hadi kichwa cha Sudi kilimuuma lakini akavumilia maana hawezi kumshusha mteja wake akakosa pesa kisa marashi.

Baada ya dakika chache yule mteja wake akaweza kufika mahali anapotaka, akashuka na kumkabidhi pesa elfu hamsini tathilimu .

“ dada mbona pesa kubwa sana hii , kutoka kule hadi hapa ni elfu kumi tu dada yangu” sudi aliikataa ile hela na kutaka kurudisha elfu arobaini.

“ hapana kaka angu chukua tu, ni haki yako iyo” yule mdada alijibu huku akiachia tabasamu mwanana akiwa na macho mregezo na sura mviringo ukimuangalia kwa haraka unaweza sema umekutana na malaika.

“daaah! Sawa dada angu kwakua umeridhia mwenyewe kunipa nashukuru sana”
“ usijali , ila samahani naweza kupata mawasiliano yako, ili atasiku nyingine nikitaka kuenda safari zangu nikuchue”.

“ ok usijali dada yangu, chukua kikadi changU cha namba hiki hapa” sudi alikijtoa na kumpa yule mdada, akakipokea yule mdada na kusoma jina la sudi.
“ unajina zuri, mimi naitwa Yusra “

“Ooh! Hata wewe unajina zuri mwanadada”
“ ahsante, ngoja nikuache basi , nitakutafuta sawa kaka”
‘ “sawa dada angu”

Sudi baada ya kuagana na yule mdada akageuza gari yake na kurudi kijiweni kwao huku akiwa na furaha tele akijiona amepata bahati ya mtendeni siku hiyo kwa maana biashara ilikua imemuendea vizuri, kwa maana alipata elfu arobaini bila kuitolea jasho.

K**a unavyojua vijana tunavyopenda majigambo, sudi alifika kwa wenzie na kuadisia wenzie jinsi alivyopewa pesa pamoja na kuombwa namba, wengine walimbeza wengine walimuonea donge, wengine walimsupport kwenye maongezi yake.

Wiki pili zilipita sudi hakutafutwa na yule mdada, lakini sudi nae hakuwa na kumbu kumbu k**a aliombwa namba na yule mdada ndipo siku moja akiwa anarudi zake usiku kwa ajili ya kuenda kupumzika ndipo akapigiwa na Yusra amfate mahali, hakuwa na wasi wasi aliweza kumfata ndipo akamkuta ametulia kwenye sehemu tulivu akijipatia maji na matunda tunda.

Sudi alipofika akakaribishwa na yule mdada hakuweza kukataa kwa kuwa kaombwa waliweza kula yale matunda huku wakipiga story muda ulipofika wa kuondoka wakaenda kwente tax na kuondoka zao, k**a kawaida ya yule mdada yusra aliposhuka akatoa kiasi cha juu,

Sudi nae alishazoea akashukuru na kuondoka zake, ila yule mwanadada alionekana anaduku duku moyoni mwake, lakini alikua anashindwa kulitoa akawa anatembea nalo kila siku.

Ndipo siku moja sudi alipoitwa na yule mwanadada Yusra akiwa pale pale mahali anapokulaga matunda, siku hiyo yusra akaamua kutoa duku duku lake alilokua anatembea nalo kila siku.

“ nakupenda sudi’

“ mmmmh!” sudi aliguna na kushindwa kusema lolote

“ mbona umeguna” yusra aliuliza huku akimuangalia kwa macho aibu sudi

“umenistua ulivyonambia ivo’”

“ kwani vibaya jamani kukupenda sudi’
“ hapana ! sijamaanisha ivo nimestuka kutoa hisia zako alafu mtoto wa k**e maana sisi wakiume ndiyo tumezoea kutongoza wanawake”

“ basi leo imekuwa tofauti’
“ sawa mimi sina neno kwakuwa umenitamkia mwenyewe haina shida ila daaah! Watoto wak**e nyie changamoto sana!”

“ kivipi sudi” yusra aliongea huku akimshika mkono wake sudi na kumfanya sudi asisimke kutokana na mikono laini ya Yusra.

“ nilishawai kuoa kabisa ila mke wangu alikua na hawala wake , hawala wake akamshawishi anifilisi ili wakaishi wote ndio mwisho wa siku ,

nikaja kufirisika na kurudi kijijini kwetu na kuanza maisha upya nikiwa sina mbele wala nyuma” sudi alisimulia kwa hisia kiasi cha kumfanya yusra aingiwe na huzuni.

“ pole sana sudi, nakuahidi sitokufanyia uliyofanyiwa na hautamkumbuka sawa”
“ sawa nimekuelewa”

“ok tuondoke” yursa akaomba waondoke, sudi hakuwa na shida wakatoka na kuingia katika Tax na kuondoka zao hadi mahali kwenye kiwanja cha mpira Yusra akaomba ashushwe pale kwa maana kwao siyo mbali na pale aliposhushwa.

“ jamani, si nikupeleke tu home kabisa”
“hapana mpenzi, nafika mwenyewe usijali, hadi hapa bei gani” yusra akauliza huku akitoa pochi yake ili atoe hela

“ hela ya nini mama, nimekuleta bure kabisa usijali hela nilizopata leo zinatosha” sudi akajitetea na kukataa hela za yusra.

“Hapana chukua tu hii elfu 30 kwa ajili ya mafuta” YUSRA alimsisitiza sudi Kuchukua ile hela ndipo sudi akakubali. Yule mwanadada akashuka zake na kutokomea gizani,

hata dakika moja haijapita sudi akajaribu kuwasha taa ili amuone yusra anapoenda cha ajabu yusra hakuonekana, alipatwa na mshangao kwa maana ni mda ule ule tu akajaribu kuenda mbele kuangalia labda yupo kwa mbele lakini hakumuona, wasi wasi ukamjaa na kuanza kupatwa na uoga akageuza gari lake na kuondoka zake.

Kile kitendo cha kupotea kwa Yusra kwenye macho yake hakuweza kunyamaza akaenda kuwasimulia wenzie, k**a unavyojua watu wa kijiweni kila mtu Ataongea Lake.

“Aaaah! Demu huli peke ako kaka wahuni wameenda kumla huyo hahahahaha!”

“ mmmh! Asiwe dem ni jini mshikaji tukaja kukukosa shauriako” hayo yote yalikua maoni mbali mbali ya washiaji zake hakuweza kuamini lipi ni sawa akaamua kuachana nayo yote.

Siku zikaanza kwenda, mahusiano ya sudi na yusra yalizidi kunoga lakini cha kushangaza sudi kila akiomba akutane na yusra kimwili hakuweza kukubaliwa kwa kigezo hadi wafunge ndoa,

sudi hakutaka kuteseka kisa utamu wa yusra, akajichanga changa na kufanikiwa kuoa mwanadada Yusra,, kwa upande wa Yursa waliweza kuja ndugu zake wawili tu kwenye harusi waliovalia nguo ndefu sana kuanzia chini hadi juu huku wakiwa na pete zinazong’aa sana halikua ni jambo la kushangaza kwa siku hiyo ya sherehe kwa maana kila mtu anajipamba anayotaka.

Maisha ya ndoa yakaanza kwa sudi na Yusra furaha na upendo ulitawala ndani yao, gafla maisha yalivyozidi kwenda sudi alizidi kunawili na kupata wateja wengi na kuanza kufanya biashara kubwa kubwa na kufikia kujenga jumba kubwa huku akiwa na biashara sehemu mbali mbali akiwa ameachana na kazi yake ya TAX DRIVER.

Maisha yalikua mazuri sana kwa sudi na mkewe hadi rafiki zake wakamuonea wivu kutokana na mizunguuko mingi ya biashara, ndipo sudi akamshauri Yusra waamie jijini dare s salaam itakuwa rahisi kwake kuendesha biashara zake,

jambo la kuamia dar es salaam halikua na shida shida ilikua ni kukutana kimwili kati ya Yusra na Sudi , Yusra hakuweza kumruhusu sudi kukutana nae kimwili, kile kitendo kilimkera sana sudi ndipo siku akamkalipia na kumtukana mkewe matusi makubwa makubwa.

Yusra alilia sana na kumwambia ukweli ya kuwa yeye sio mwanadamu basi ni mtoto wa malikia katika falme za majini na sharti lao kubwa ni kumsaidia mwanadamu na siyo kufanya nae mapenzi, sudi alitamani azimie baada ya kusikia anachoambiwa na Yusra ,

Kwa maana siku zote alikua anaishi na jinni bila ya yeye kujua, ila alichosisitizwa na Yusra asiweze kumwambia mtu yeyote iwe siri yake ataendelea kuwa na maisha mazuri.

Sudi mwanzoni haikuwa rahisi kuuukubali ukweli lakini siku zilivyozidi kwenda akaizoea ile hali huku moyoni akiwa na duku duku,

wazazi wake waliweza kumuuliza kuhusu watoto hakuweza kuwajibu jibu sahihi.
Miaka ikazidi kwenda ndipo akaanza kuchoka hali ile ya kutoa kuwa na mtoto ingali umri unaenda, siku moja akiwa zake katika mizunguuko ya biashara aliweza kustuliwa na mdada, alipomuuliza shida yake nini, ndipo yule msichana alipojitambulisha kuwa ni mkewa aliyeachana nae.

Sudi alimshangaa sana kutokana na hali dhohofu aliyokuwa nayo, alipomuuliza ndipo alipomwambia baada ya kuachana alienda kwa yule hawala wake, yule hawala wake alikua ni mtu wa kuruka viwanja hakuweza kutulia na mwanamke mmoja, alimtapeli mali zote na kutokomea pasipo julikana.

Kutokana na huruma aliyo nayo sudi aliweza kumsaidia kiasi cha pesa na kumuachia namba ya simu, akiwa na shida aweze kumsaidia k**a binadamu mwenzie.

Sudi aliweza kumsaidia mke wake wa zamani ila siku zilivyozidi kwenda wakaanza kujenga ukaribu sana, ndipo Yusra akiwa na mumewe akamuasa kuwa kuna hatari inamkaribia karibu yake , kwaiyo akae nayo mbali.

Hakuweza kumuelewa sudi na wala hakuyajali yale maneno , siku zilivyozidi kwenda ndipo sudi akazama kimapenzi upya na yule mke wake wa zamani na kumwambia siri zake zote kuhusu mkewa na sharti alilopewa, sudi alifanya yote bila yeye kujijua k**a alifanyiwa dawa na yule mke wake wa zamani.

Ndipo sudi kaanza kubadirika na kuanza kurudi usiku sana, na kumjibu mkewe, siku moja mkewe wa zamani akamshauri waende kwa mganga ili waweze kumuuwa yule mkewe jini ili wakifanikiwa waendelee kuishi pamoja na wazae watoto ili wazazi wake wawe na furaha.

Kutokana na akili za kushikiwa sudi akakubali na kupanga safari ya kwenda kwa mganga, siku iliyofuata sudi akaongozana na yule mke wa zamani na kwenda kwa mganga, walipofika kwa mganga wakasikilizwa na kupewa masharti ya kufanya ukiwepo kumtilia sumu yule mkewe , lile sharti halikuwa gumu kwa sudi kutokana na madawa aliyofanyiwa na yule mke shetani wa zamani.

Siku ya ijumaa, mida ya jioni sudi aliandaa mwenyewe chakula na kutegesha ile sumu , mkewe akiwa hajui hili wala lile, mda wa kula sudi akazuga anaenda kununua vinywaji mkewe aanzekula,ndipo akatoka zake na kufunga mlango kwa nje na kuondoka akaenda kulala kwa yule hawala wake.

Asubuhi na mapema aliweza kurudi zake na kukuta nyumba yake imetulia akafika kwenye mlango wa nyumba yake na kufungua mlango haku mtu akaingia ndani na kuangalia kila chumba hakumuona mtu yeyote, akaamua kurudi zake sitting room ndipo akasikia kicheko kikali kikiambatana na upepo mkali, sudi alichanganyikiwa akataka kutoka nje milango ikajifunga kisha kicheko kikakata.

Akaangalia huku na huku ndipo akaiona barua iko juu ya meza ya kioo akaenda kuichukua huku akiwa anatetemeka kwa hofu akaifungua na kukuta maandishi yaliyoandikwa kwa damu.

“ NILIKUPENDA SANA SUDI, NA KUJITOLEA KUKUSAIDIA NA KUKUAMBIA UKWELI WANGU,LAKINI HUKUTAKA KUNISIKILIZA UKAAMUA KUNIUA, ILA NITARUDI KWA AJILI YAKO NA SITA KUWA K**A MWANZO NILIVYOKUWA” ile barua ilisomeka vile sudi aliachnganyikiwa na kupiga makelele kwa uoga lakini hakupata msaada wowote.

Gafla akaanza kucheka cheka ovyo na kuongea peke ake akanyanyuka na kwenda mlangoni mlango ukafunguka na kutoka zake nje huku akianza kuvua nguo zake na kubakia na boxer.

Majirani zake walimshangaa sana na kuhisi labda kapatwa na uchizi, wakaamua kumk**ata na kumfunga kamba na kumuwahisha hospital, zile habari za kutembea bila nguo yule mke wake wa zamani alizisikia akaamua kwenda hospital na kumkuta mtu wake anacheka peke yake na kucheka cheka bila sababu.

Yule mdada alipoona vile akatoa taarifa kwa ndugu wa mwanaume kuhusu yaliyomkuta, alipohakikisha ametoa taarifa akatoka zake nje ili aende kuchukua pesa za kulipia gharama za kumlaza mgonjwa wao, akiwa njia anatembea gafla kilisikika kishindo kizito , watu walijazana kuangalia nini kimetokea ndipo wakamkuta yule mdada amegongwa na gari huku ile gari ikipotelea pasipojulikana.

Yule mdada akawaishwa haraka hospital lakini hakuweza kuvuta tena pumzi ya dunia alifariki akiwa njiani anawaishwa hospital,ndugu wa sudi waliweza kufika hospital na kukuta ndugu yao akiwahajielewi wakaamua kumchua na kuondoka nae kijijini kwa ajili ya matibabu.

Baaa ya siku mbili tatu, alipelekwa kwa mganga ndipo mganga akawaelezea kuwa sudi alikua anaishi na jini kutokana na kukiuka masharti ya yule jini na kumuekea sumu kwenye chakula ili afe ndiyo yamemkuta k**a wanavyomuona na kuhusu swala la tiba halitowezekana kwa maana yule jini anauwezo mkubwa sana, ndugu wa sudi hawakukubali kushindwa walizurula kwa waganga wengi sana lakini paligonga mwamba.

Mwisho wa siku ndugu wakachoka na kuamua kumueka sudi nyumbani, siku zilivyozidi kwenda sudi alizidi kubadilika na kudhofika kiafya Siku ya ijumaa mida ya usiku Sudi aliaga dunia akiwa anatoka damu puani na mdomoni.kule mjini mali za sudi zilipotea potea kwa mazingira ya kutatanisha hata ile nyumba haikuweza kuonekana pale mahali lipokuwa, siku zikaenda na kuhusu story ya sudi ikasahaulika kwenye vichwa vya watu.

********** MWISHO***********

10/09/2020

Wakati uongozi wa klabu ya Yanga ukiendelea na mchakato wa Mabadiliko ya mfumo wa Uendeshaji wa klabu hiyo, Mfanyabiashara Rostam Aziz ambaye anaidhamini Yanga kupitia kampuni yake ya Taifa Gas, ameonyesha nia ya kutaka kuwa Mwanahisa wa mabingwa hao wa kihistoria

Kulingana na Mwongozo wa Serikali, k**a Yanga itafuata mfumo wa hisa, asilimia 49 zitagawiwa kwa Wawekezaji wasiopungua watatu wakati asilimia 51 zitabaki mikononi mwa Wanachama

Imeelezwa kuwa Roastam amefanya mazungumzo na uongozi Yanga ambapo amebainisha kuwa yuko tayari kuwekeza kwa kitita cha Tsh Bilioni 30 kununua hisa asilimia 29

Aidha, amebainisha kuwa kuwa asilimia 20 zitakazokuwa zimebaki zinaweza kuchukuliwa na Wawekezaji wengine wasiopungua wawili kwa mauzo yasiyopungua Tsh Bilioni 20 na hivyo hisa zote kuuzwa kwa wastani wa Tsh Bilioni 50

Inaelezwa pia Mnyabiashara huyo yuko tayari kuchukua jukumu la kujenga uwanja wa klabu ya Yanga kule Kigamboni katika eneo la ekari saba ambalo lilikabidhiwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda mwaka uliopita

K**a hili litakamilishwa, litaifanya klabu ya Yanga kuwa ghali zaidi kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati

04/08/2020
04/08/2020
18/04/2020

HISTORIA YA WANYAKYUSA.

Wanyakyusa (pia huitwa Wangonde au Wasochile) ni kabila la watu wanaoishi kwenye wilaya ya Rungwe katika sehemu za kusini za Mkoa wa Mbeya (Tanzania) na wilaya ya Kyela.
Lugha yao, inayoendelea kutumika sana, ni Kinyakyusa.
Mara nyingi Wagonde upande wa kusini wa mto Songwe nchini Malawi huhesabiwa pamoja nao katika kundi lilelile. Mwaka 1993 watu zaidi ya milioni walikuwa wanajumlishwa kwa jina hili, takriban 750,000 upande wa Tanzania na 300,000 upande wa Malawi.

Wikipedia inasema Kihistoria watu wanaoitwa leo Wanyakyusa waliitwa Wakonde, ambao kati yao Wanyakyusa walikuwa ndio kabila kubwa. Wakati wa karne ya 20 "Wanyakyusa" limekuwa jina la kundi kwa jumla. Hadi leo kanisa la Kilutheri la KKKT linatumia jina "dayosisi ya Konde" kwa eneo lake katika mkoa wa Mbeya.
Wakati Wajerumani walipofika sehemu za kaskazini kwa Ziwa Nyasa mwisho wa karne ya 19 hawakuona tofauti ya kimsingi kati ya watu wa Malawi kaskazini na wale wa sehemu za Rungwe wakawaita wote "Wakonde" kutokana na jina lililokuwa kawaida ziwani.

Historia inasema kwamba asili ya Wanyakyusa ni mkoani Morogoro. Kabila hilo likitokana na kabila la Waluguru. Hili hasa ndilo chimbuko la Wanyakyusa. Inasemekana kwamba mwindaji mmoja wa Kiluguru alitembea peke yake porini bila ya kuongozana na mtu mwingine. Alitembea hadi akafika maeneo ya Kabale huko Suma, Tukuyu wilayani Rungwe. Akiwa huko, akaendelea na kazi yake ya uwindaji. Baadaye akatokea Mzulu mmoja kutoka Afrika Kusini aliyekuwa na binti yake. Akafika maeneo alikokuwa akiishi yule mwindaji Mluguru, naye akapiga kambi hapo Kabale, wakaungana katika maisha ya uwindaji.

Ikawa kila yule Mluguru akitoka asubuhi kwenda kuwinda, alikuwa akifanikiwa kurejea nyumbani na wanyama wakati rafiki yake wa Kizulu alikuwa akirudi mikono mitupu. Kutokana na hali hiyo, Mluguru akageuka kuwa mfadhili wa Mzulu, kwa kutoa misaada mara kwa mara, na kwa kulipa fadhila hizo, akamwoza bintiye kwa Mluguru. Akamwoa na maisha yakaendelea huku nyumbani kwa mwindaji wa Kiluguru na mkewe binti wa Kizulu, kukiwa hakukosekani nyama k**a kitoweo.

Kwa sababu ili kuihifadhi nyama ilibidi kwanza ibanikwe, basi kitendo hicho kilisababisha harufu nzuri ya kitoweo kile kusambaa eneo kubwa na kufika hadi ukweni kwake nyumbani kwa Mzulu.
Ndipo Mzulu yule akawa anasema mara kwa mara: “Pale panatoa kyusi kila siku” akimaanisha moshi kwa lafudhi ya lugha ya kwao.
Mazoea ya kutamka ‘kyusi’ kila siku, yakaligeuza neno ‘kyusi’ na sasa likawa linatamkwa ‘kyusa’, baadaye ‘kyusa’ ilipozidi kutamkwa kwa mara nyingi, nayo pia ikabadilika bila kukusudia ndipo watu walipokuwa wakimwita Mluguru ‘Mnyakyusa’, kwa kuwa moshi ukiambatana na harufu ulikuwa ukitokea ndani ya nyumba yake na kusambaa.

Kwa hiyo, tangu hapo na kutokana na jina hilo alilopewa kwa ajili ya mazoea ya kukosea kutamka kitu, hata watoto wake pia waliozaliwa na Mluguru na mkewe Mzulu, wakawa wakiitwa ‘Wanyakyusa’. Hiyo ndiyo asili na chimbuko la kabila la Wanyakyusa, na kwa kuwa Mnyakyusa alikuwa tayari ana asili ya pande mbili - wakati baba akiwa na asili ya Kiluguru na mama Mzulu wa ‘kwa Madiba

Na hata uchifu ukaanzia mahali pale palipokuwa panaitwa Kabale, na yule Mluguru aliupata uchifu kwa kuwa yeye ndiye aliyekuwa mwanzilishi na mkazi wa kwanza wa eneo lile na ndiye aliyekuwa anafahamika zaidi.

Mavazi yao
Kwa upande wa mavazi, Wanyakyusa walikuwa wakivaa mavazi yaliyokuwa yakijulikana k**a ‘Lyabi’, Ni mavazi ya kwanza kwa kabila yakivaliwa enzi za utumwa. Mavazi haya ni yale yanayofunika maeneo ya siri pekee, na kwa wale ‘waheshimiwa’, kidogo basi wao walivaa vazi lililokuwa likiitwa ‘kikwembe’ au ‘kilundo’. Mavazi haya yaliyovaliwa kwa mtindo k**a lubega, ndiyo yaliyomtambulisha na kumtofautisha mhusika mbele ya jamii.

Ngoma yao
Ngoma iliyokuwa ikichezwa na Wanyakyusa enzi hizo, ilikuwa ni ya kuchezea mikuki na mara nyingi ngoma hiyo ilikuwa ikichezwa wakati wa msiba. Lakini ngoma za kawaida zilizokuwa zikichezwa pasipo kutumia mikuki na wakati wa sherehe na shughuli nyingine, ni ‘Ipenenga’. Hii mara nyingi ilikuwa ikichezwa na watu ‘wastahiki’ tena kwa madaha na maringo ya hali ya juu. Hata machifu walikuwa wakiicheza sana ngoma hii.

Chakula chao
Chakula chao kikuu na ambacho Mnyakyusa angeonekana kuwa amemkarimu mgeni, si kingine bali ni dizi zinazomenywa na kupikwa maarufu k**a ‘mbalaga’. Mnyakyusa halisi k**a atakula chakula lakini akakosa ‘mbalaga’ hujiona k**a bado hajakamilisha mlo, ingawaje siku hizi kuna mabadiliko fulani ambayo wengi hupendelea ugali na wali; lakini bado asili ya chakula chao hawawezi kuibadilisha kamwe.
Na ni lazima chakula k**a ‘kande’ kipikwe kwenye tukio la msiba uwao wote, k**a shughuli za msiba zitakwisha pasipo kupikwa chakula hicho chenye mchanganyiko wa mahindi na maharage; msiba huwa haujakamilika hata k**a wafiwa ni watu wenye kujiweza kifedha zaidi lakini ni lazima kande zitapikwa japo kiasi.

Sifa za Wanyakyusa wa Kyela
1. Wacha Mungu
2. Wengi si Wapole mtu afanyapo kosa
3. Wanajua kupenda
4. Hawapendi dharau
5. Wanapenda kujulikana (hasa k**a wamesoma hadi kupata digrii n.k.)
6. Wapiganaji sana kimaisha
7. Wana wivu katika masuala ya mapenzi
8. Wanapenda haki itendeke, hawapendi ubabaishaji
9. Ni watu shupavu sana kwenye kazi za kujitolea hasa za kijamii

Sifa za Wanyakyusa wa Tukuyu
1. Wacha Mungu
2. Wapole
3. Wanajua kupenda
4. Hawapendi dharau kabisa
5. Wanajituma kwenye kazi, hasa kilimo
6. Wana wivu sana
7. Wanapenda haki itendeke na hawapendi ubabaishaji
8. Ni watu jasiri na wasioogopa vitisho
9. Ni Waelevu

Chanzo: Tanzania Safari channel

05/02/2020

DONDOO MUHIMU KUTOKA GSM. .

👏👏Klabu ya Yanga ilitangaza k**ati ambayo itasimamia na kuiongoza Yanga SC kuelekea mfumo wa kisasa, sisi k**a GSM pamoja na kuwa na plan nyingi za kusaidia timu in terms of technical bench na wachezaji ambazo tayari tumezifanya kwa kiasi kikubwa, Juzi tumemleta pia mtaalamu mwingine kutoka south Afrika ambaye ataongezeka katika technical bench kuungana na Luc, Riedoh. Hii yote ni kuifanya Yanga SC kuwa na nguvu.

🙏🙏Tunaendelea na tutaendelea kufanya vitu vingine ambavyo vipo nje ya mkataba , lengo ni kuendelea kuisaidia timu yetu ya Yanga SC.

👍👍Tukizungumzia kambi ambayo timu inakaa na uwanja wa kufanyia mazoezi ni 100% GSM inasimamia.

🙏🙏Tukaona haitoshi tu kuona timu ya Yanga inafanya vizuri uwanjani, tukaona tuwasaidie kuwapeleka katika mfumo ambao klabu itakuwa imara .

🤔🤔Watu wengi wanaweza wakadhani GSM ina nia ya kuichukua Yanga, ama kuimiliki. . hapana sisi lengo letu ni kuisaidia Yanga SC.

👍👍K**ati iliyoundwa kusimamia mabadiliko ina watu weledi sana, lakini changamoto wengi hawawezi kujitolea 100% kusimamia mchakato huo kwa kuwa wamebanwa na majukumu mengine ikizingatiwa mabadiliko yanahitajika haraka sana. .

👏👏Kwa kuliona hilo ndio maana tukamleta mtaalam Antonio Pinto ambaye ana experience kubwa sana kutokea Benfica na atakuwa dedicated katika wajibu huo. na amefanya mambo makubwa sana Benfica, ambapo wameuza wachezaji wenye thamani ya euro milioni 600 katika kipindi cha miaka 10, na wametwaa ubingwa mara 8 katika miaka 10.

🤔🤔Huyu hajaja katika operation za Yanga, amekuja katika transformation project tunayoitarajia kuifanya k**a klabu.

🙌🙌Pinto anaondoka leo, amekuja kwa ajili ya makubaliano na majadiliano ambayo tayari tumeafikiana. .

💪💪Sisi GSM tumefanya miradi mingi sana ambayo haijawahi kufail na ipo very succesfull na huu mradi nakuhakikishia utakuwa very succesful. .

👏👏Hatutaendana na zile njia ambazo watu wanazitumia. .tutakwenda very profesional tutampa muda Pinto nakuhakikisha ana fikia malengo. . hii project team itaenda bega kwa bega na k**ati ya mabadiliko ya klabu ili kuhakikisha tunaendana na matakwa halisi ya nchi yetu.

💥💥Pia tutafanya mabadiliko ya katiba ili kuendana na mabadiliko tunayoenda kufanya, hivi vitu vyote vitaenda parallel.

🚀🚀Muelekeo wetu ni kuisaidia Yanga SC isimame kwa miguu yake miwili. .

💥💥Infrastructure kuna trainning facility, sehemu ya kulala wachezaji na kuhakikisha viongozi wanakuwa na ofisi nzuri na zenye hadhi. . muda mfupi tu nawahakikishia kila kitu kitabadilika Yanga SC na itakuwa ni klabu yenye mafanikio makubwa kuliko klabu yoyote ukanda wa Afrika mashariki na kati.

Eng Hersi Said (Mkurugenzi mwekezaji GSM)

07/01/2020

JENNY MSAMBWANDA 01
(WAKUBWA TU: 18+)

By Kassym Ben

Nikiwa nimepitiwa na usingizi mzito usiku mnene, nikaamshwa na sauti za mtu aliyekuwa ananiita kupitia dirishani. Nikanyamaza kimya kwa muda wa dadika kadhaa nikijaribu kujiuliza ni nani aliyekuwa anagonga dirisha langu. Sikuweza kuitambua sauti ile ya k**e.

"Kassim, Kassim!"

Iliendelea kuniamsha sauti ile ya k**e ambayo ilionesha kuwa mwanamke yule aliyekuwa akiniita kupitia dirishani alijitahidi kuifanya sauti yake isisik**e na mtu mwengine yeyote zaidi yangu. Nikataka kuangalia saa kwenye simu yangu. Lakini ilikuwa mbali kidogo na kitandani nilipokuwa nimelala. Huwa nina kawaida ya kuizima wakati wa usiku na kuiweka kwenye chaji. Sikuweza kujua ilikuwa saa ngapi. Mtu yule aliendelea kuniita huku akigonga dirisha langu kidogo kidogo na kunyamaza kwa dakika chache.

"Wewe nani?"

Nikauliza kwa sauti ya chini.

"Mimi ni Jenny. Nna shida ya usafiri. Naomba unipeleke mahala na gari yako."

Mwanamke yule akaongea kwa sauti ya unyenyekevu kupita kiasi.

"Jenny yupi?"

"Jenny wa hapo nyumba ya pili, kwa Mbonea. Naomba nisaidie kaka angu."

"Mbona ni usiku sana? Kuna shida gani? Unataka nikupeleke wapi?"

"Nataka unipeleke Dodoma. Nikakulipa kiasi chochote unachotaka. Nakuomba nisaidie."

Sikujua cha kumjibu. Nilitamani sana pesa yake. Lakini muda ule gari ilikuwa kwa bosi. Nilishaipeleka kuilaza. Huwa naichukua asubuhi mapema na kufanyia biashara ya Uber na usiku nairudisha kwa bosi kabla ya saa tatu. Hayo ndiyo yalikuwa makubaliano yangu na bosi. Kwa muda ule nisingeweza kujaribu kumpigia simu bosi eti anipatie gari.

Nikajiuliza pia, kwanini Jenny alitaka kupelekwa na mimi wakati mume wake Mzee Mbonea ana gari? Sikuwa na jibu. Alinipa wasiwasi. Nikapata hisia kuwa pengine alikuwa anatoroka. Kwa kuwa k**a gari ya Mbonea likuwa na shida basi angekuja yeye mwenyewe kuniamsha ili nimpatie msaada ule wa dharura kwa kuwa alikuwa ananifahamu.

"Sasa Jenny, naelewa ndio una shida na usafiri. Lakini gari nimeilaza kwa bosi na muda huu siwezi kuipata. Ni mbaka kukuche. Kwa hiyo nenda kalale halafu nitakufata mapema asubuhi pale nyumbani kwako."

Nilimuelekeza Jenny.

"Hapana Kassim. Nisaidie naomba. Fanya namna yoyote tupate gari unipeleke. Nitakupa chochote. Nakuomba sana. Naomba nifungulie basi tuongelee huko ndani."

Jenny aliongea kwa sauti ya huruma. Alizidi kunipa wasiwasi. Ilionesha k**a alikuwa anatoroka kwa mume wake Mzee Mbonea. Nikajiuliza maswali yaliyokosa majibu. Lakini kiukweli nilitamani sana kumsaidia. Nilijua ningepata pesa nzuri kutokana na kauli zake. Na pia aliposema kuwa angeweza kunipa chochote alinisisimua zaidi na kunipa shauku ya kumsaidia.

Jenny ni mdada aliyejaliwa sura na umbo la kuvutia. Alikuwa na tako kubwa jambo ambalo lilipelekea watu kumpachika jina la 'JENNY MSAMBWANDA'. Rangi yake nyeupe kiasi iliipamba zaidi ngozi yake nyororo na kumuongezea uzuri. Alikuwa na umri wa k**a miaka 28 hivi. Wanaume waligeuza shingo zao kila upande aliokatisha. Anavutia mno.

"Hebu ngoja nijaribu kumpigia simu mshikaji wangu flani nione k**a anaweza kunipatia gari yake muda huu."

"Sawa. Jitahidi naomba. Nipo tayari kukupa zawadi yoyote na kiasi chochote cha pesa ukinifikisha Dodoma. Muda mrefu nilipiga haupatikani. Ndio maana nimekuja kukugongea dirishani."

Nikainuka na kuisogelea simu yangu wakati Jenny akiendelea kuniomba na kunishawishi kwa ahadi za kusisimua. Nikaiwasha. Nilipoangalia saa nikagundua kuwa ilikuwa saa nane na nusu usiku. Nikampigia rafiki yangu Timoth ambaye niliamini angeweza kunipatia gari yake. Bahati mbaya hakuwa hewani.

"Jenny, huyu jamaa hapatikani. Nenda ukala..."

Wakati najaribu kumalizia kauli yangu hiyo Jenny akaniwahi.

"Daah hapana Kassim. Nisaidie naomba. K**a haiwezekani kupata gari muda huu basi naomba nilale humo kwako halafu kabla hakujakucha uifate gari yako tuanze safari."

Mmh Jenny aliniweka njiapanda. Nikafikiri kwa muda kabla ya kumjibu chochote. Kabla sijazungumza jambo akaendelea kuongea.

" Naomba nifungulie basi tuongelee huko ndani Kassim."

Jenny aliongea kwa huruma. Licha ya wasiwasi niliokuwa nao nilishindwa kukataa kumsaidia. Nilijikuta natoka nje na...

SUBIRI SEHEMU YA 02. Usithubutu kuikosa hadithi hii yenye kusisimua.

Likes na comments zenu zitanipa kasi ya kuwapa burudani haraka zaidi. Pia kwa uklike na kucomment utaiona haraka kila ninapopost.

Kwa burudani zaidi jiunge na group la RIWAYA NA HADITHI TAMU kwa kubonyeza hapo chini.

Bofya hapa https://www.facebook.com/groups/541176899627277/?ref=share

28/12/2019

AISHA MAPEPE NIMERUDI!

Nianze na ipi hapa?

1) "RASHIDI NINYONYE NA HUKU!"

2) FUNDI NGUO ALIVYONIKOLEZA

3) "INGIZA POPOTE BOSI!"

Piga kura. Hakikisha unalike na kucomment ili uone haraka ninapoanza kupost baadae leo hii.

Pia ISIKUPITE HII (KWA WANAWAKE) 👇👇👇

FURSA YA MIKOPO KWA WANAWAKE

Ni mkopo wa haraka na rahisi. Hauhitaji dhamana yoyote wala kutoa kiasi chochote cha pesa kabla ya kupatiwa mkopo. Bonyeza hapo chini kuomba.

Bofya hapa 👇👇https://form.myjotform.com/92121761380552

29/10/2019

💋KITUMBUA CHA KIHINDI💋
SIMULIZI TAMUUUU
MTUNZI : Kizaro Mwakoba
TUNGO : Chombezo
Watsap : 0765388806
SEHEMU YA 10

ILIPOISHIA
Magosho aliendelea kumpagwawisha Bi.Fahreen ambaye alionekana kuwa hoi bin taaban na kumfanya aendelee kalalamika huku akiomba huruma ya Magosho imshukie.
“Omnh!....Go…Go..Gosooo…iko..ta..iko…kwisa…ve..ve...Com…aaaa!” maneno yalipotea mdomoni kwa Bi.Fahreen.
Mwanamke yule alikuwa hajitambui wala hatambuliki alichokuwa anakizungumza. Mbwembwe zote alizokuwa ameanza nazo zilimuisha. Hakujiweza tena, hata mkono hakuweza kuuinua. Macho aliyaona mazito utafikiri alikuwa amebebeshwa mifuko ya smenti kwenye kope zake, na hata sauti nayo ikakata. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakimuenda mbio kuliko kawaida na mwili ukaanza kumtetemeka utafikiri alikuwa amepatwa na degedege.

ENDELEA…. 10
Lilikuwa ni shindano kabambe la mchezo wa riadha. Washindanaji walitakiwa kukimbia kwa kuzunguuka uwanja uliokuwa na mita mia moja kiasi cha mara tano. Mwisho mwa raundi moja kulikuwa na kilima ambacho mkimbiaji alipaswa kukipanda kabla ya kuanza kukimbia roundi ya pili.
Mashindano yale yaliwahusisha wakimbiaji wa pande mbili ambao walikuwa ni Bi.Fahreen na mpinzani wake alikuwa ni kijana Magosho. Walikuwa wakigombania medali ya dhahabu ambayo ilikuwa ni lazima ichukuliwe na mmoja kati yao. Hivyo kila mmoja alikuwa na hamu kubwa ya kujinyakulia medali hiyo ambyo ilikuwa na thamani kubwa.
Washindanaji wakajipanga kwenye mstari na punde tu kipenga kilipopulizwa wote wawili wakaanza kutimua mbio. Kila mmoja alionesha mbwembwe zake mapema. Hakuna aliyekubali kushindwa na mwenzie.
Loo! Bi.Fahreen akafyatuka k**a mshale na kujikuta amefika kileleni ndani ya dakika tano tu. Magosho akajaribu kuongeza mbio lakini wapi hakufanikiwa kumfikia mama yule wa kihindi.
Magosho akiwa na matumaini ya kumfikia mpinzani wake, akashangaa Bi.Fahreen akimpita k**a mshale kutokea nyuma yake. Mama yule wa kihindi alikuwa anakwenda utafikiri amekula miguu ya mbuni. Alifika kileleni kwa mara nyingine wakati Magosho hakuwa na hata dalili ya kuukaribia mlima ule pamoja na jitihada zake zote.
Kijana alionekana kuvamia fani ile ya riadha kwani aliendelea kusua sua njiani wakati Bi.Fahreen akijitwalia pointi mara kadhaa. Hata hivyo kijana Magosho hakukata tamaa ingawa alikuwa akihemea juu juu kwani aliendelea kukimbia hadi kufanikiwa kufika kileleni angalau mara moja tu.
Mshindi aliyetwaa medali ya dhahabu alikuwa ni Bi.Fahreen kwasababu aliweza kufika kwenye kilele cha mlima ule mara tano, wakati mpinzani wake yeye alifika kileleni mara moja tu. Hata hivyo wote wawili walikuwa wamechoka vilivyo na kujikuta wamelala mithili ya wahanga wa mafuriko au wa kimbunga Katrina.
Magosho alikuwa wa kwanza kupata ahuweni kutoka kwenye ule uchovu, aliinua shingo yake na kumchungulia Bi fahreen usoni. Mama wa watu alikuwa amechoka utafikiri ametoka kufanya kazi ya kuhamisha milima ya Uruguru kwenda Usambara. Alikuwa amelala huku amefumba macho utafikiri amekata Kamba. Magosho akamshika kwenye mashavu mwanamke yule na kumpiga busu usoni ambalo lilimfanya mama wa kihindi kufumbua macho.
“Mama” aliita Magosho kwa sauti iliyo kwaruza.
“Nani iko mama yako?” alihoji Bi.Fahreen kwa sauti iliyotoka kwa shida.
“Si wewe jamani”
“Mimi hapana iko mama yako” alizungumza Bi.Fahreen kwa ile sauti yake ya kujilazimisha.
“Kumbe we nani?” Magosho alihoji kwa sauti nzito
“Ita mimi penzi bhanaaa.” Bi. Fahreen naye akazungumza kwa sauti ya kujilazimisha.
“Basi baby usijali” alisema Magosho na kumpiga busu la mdomo Bi.Fahreen.
“Mambo iko ivo toto zuri. K**a taka mimi chukie veve ita mimi mama” alisema Bi.Fahreen huku akimkumbatia Magosho kwanguvu. Magosho naye akamkumbatia mwanamke yule k**a vile alivyofanya yeye. Yani k**a ungepata bahati ya kuwaona ungefikiri wawili wale walikuwa wanalingana umri.
Pamoja na kwamba Bi. Fahreen ndiye aliyekuwa akifanya uchokozi katika kuhakikisha amemnasa Magosho, lakini kijana naye alionekana kufurahia mchezo ule pengine nafikiri ni kwasababu ya kupewa vitu adimu vyenye mahadhi ya Kuchi kuchi Hotahe. Ndugu msomaji, Magosho alitegwa akategeka na kuingia mzima mzima katika himaya ya mwanamke yule wa kihindi.
“Vipi lakini Baby?” Magosho alihoji baada ya kuachiana na mwanamke yule.
“Tangu mimi zaliwe hapana pata kitu k**a veve nipa leo” alisema Bi.Fahreen kwa furaha na kujidai.
“Mnh! Lakini hata wewe unaweza. Kumbe Nakeshiwar anafaidi kiasi hiki!” alisema Magosho na kuishika pua nyembamba ya Bi. Fahreen na kuivuta kidogo kimahaba.
“Hapana taja Nakeshi hapa bhana. Mimi lazima oa veve” alizungumza Bi. Fahreen kwa furaha kubwa.
“Wacha masihara Fahreen. Wewe si una mume wako?”
“Mume nini bhanaa, K**a veve iko nipa mimi raha hakuna bhaya!”
“Basi mtoto mzuri nitafanya unachopenda” alisema Magosho huku mkono wake ukiwa kwenye zigo la mama yule ukilipigapiga na kulitomasa tomasa kwa kiganja cha ule mkono wake.
“K**a iko sikia hamu, hapana sita ambia mimi” alisema Fahreen.
“Mnh!” Magosho akaguna.
“K**a veve iko furahisa Fahreen, basi No problem ongezea sahara kila mezi” alisema Bi.Fahreen kwa msisitizo mkubwa.
“Dah! Nitafurahisana mpenzi k**a kweli” Magosho lizungumza kwa furaha aliposikia kuwa ataongezewa mshahara. Yaani raha apewe halafu na mshahara pia aongezewe? Mnh! Haya bwana sisi yetu macho mana hakuna ajuae ya mbeleni. Au sio ndugu msomaji?
“Hapana hiyo tu Goso. Mimi taka jengea nyumba veve, nunulia gari, halafu fungulia Business” alisema Bi.Fahreen akionekana wazi kufurahishwa na ile starehe aliyopewa na mtoto wa kibantu, kijana wa marehemu mama Ashura.
Magosho akahisi k**a vile alikuwa ndotoni. Hakuyaamini yale maneno ya Bi.Fahreen yalikuwa yakitoka moyoni mwake. Alitamani sana ahadi ile itimie ndani ya dakika zile zile. Akajikuta akizidi kuvutiwa na penzi la mama yule wa kihindi ambaye alikuwa ni mke wa bosi wake.
* * * *
Ashura baada ya kugeuka nyumba, macho yake yalitua kwenye Starlet moja ambayo alimuona nayo Zawadi kwa mara ya kwanza kule kwenye kijiwe cha kuuzia vitumbua. Akajaribu kuangaza pengine angeona kitu ambacho kingekuwa ni uthibitisho tosha kuwa ile ilikuwa ni nyumba yake lakini hakuona chochone. Aligeuza macho na kumtazama rafiki yake.
“K**a sikosei unakusudia ile gari?” Ashura akahoji.
“Swadakta! unaikumbuka gari ile?” Zawadi alihoji
“Inafanana na ile niliyokuona nayo kwa mara ya kwanza”
“Sio ina fanana, ndiyo yenyewe”
“Kwahiyo unataka kusemaje?”
“Inatosha kuwa uthibitisho kwamba hapa ni nyumbani kwangu”
“Kwa upande wako inatosha, lakini kwa upande wangu bado ni kigugumizi” Ashura alizungumza.
“Kwani ulitegemea kuniona Zawadi mimi naendeha gari?” Zawadi akahoji.
“Kwakweli ni muujiza”
“Basi hata hii nyumba kuwa yangu na iwe muujiza”
“Mhn! basi hongera mwaya maisha ndo umesha yaweza hivyo” Ashura akazungumza kwa shingo upande huku akiamini shoga yake alikuwa anamuongopea.
“Ah kawaida, sio kazi saana k**a unavyo fikiri” Zawadi alizungumza na kumshika mkono Ashura.
Walivuta hatua kuelekea kwenye mlango wa ile nyumba kubwa. Ashura alikuwa makini kuangaza pande mabali mbali kukagua mazingira ya nyumbani pale. Kiukweli ndugu msomaji mazingira yale hayakuwa ya kitoto ukizingatia hali halisi ya mazingira aliyokuwa akiishi Ashura, hakuwa na ujanja wa kujizuia kushangaa.
Walipofika mlangoni Zawadi alitoa kadi k**a ya ATM na kuipitisha kwenye kitasa cha mlango ule ambao ulijifungua wenyewe. Ashura alizidi kupata mshangao. Mwenyewe alikuwa amezoea kuona na kutumia yale makufuli ya Athumani mfupi kasimama malangoni. Hakuwahi kuwaza wala kufikiri k**a kulikuwa na milango iliyokuwa ikifunguliwa na kadi.
Walifika kwenye sebule moja iliyokuwa pana kiasi cha kuingiza hewa na mwanga wa kutosha. Samani za gharama zilikuwa zimejaa na kuifanya sebule ile kupendeza na kuvutia mno.
“Karibu shosti jisikie upo kwako” Zawadi alizungumza huku akimuonesha Ashura mahali pa kuketi. Ashura alibakia amesimama akitafakari maisha ya rafiki yake yule yalivyokuwa ya maajabu. Akajaribu kumkumbuka Zawadi yule waliyekuwa wakiuza wote vitumbua kule uswahilini na kumfananisha na Zawadi wa leo aliyekuwa anafungua loki za milango kwa kutumia kadi k**a za benki.
"Vipi Shost mbona hukai?" Zawadi alihoji baada ya kumuona rafiki yake k**a vile amekauka kwa kupigwa na shoti ya umeme. Ashura baada ya kusisitizwa na rafiki yake aliketi kwenye sofa moja la gharama ambalo hakuwahi kufikiria k**a angewahi kulikalia maishani mwake.
"Dakika moja tafadhari" Alisema Zawadi na kuelekea kwenye korido moja ndefu ambayo ilimfikisha hadi kwenye mlango wa chumbani.
Baada ya sekunde kadhaa Ashura akasikia sauti ya Zawadi ikimuita kutokea kule kwenye korido. Akajiinua na kuelekea kule sauti ilipotokea.
"Shoga uko wapi?" Ashura alipaza sauti baada ya kuona milango ikimchanganya na kushindwa kuelewa rafiki yake alikuwa chumba kipi. Mlango wa chumba kimoja ulifunguliwa na zawadi akachunguli.
"Niko huku Shosti wangu" Alisema Zawadi
"Ka! shoga milango inachanganya"
"Kwasababu ni mgeni tu shoga ndiomaana unaona hivyo. Karibu ndani"
Ashura aliingia chumbani mle na kujikuta katika hali ya mshangao zaidi baada ya kuona mazingira ya chumbani mle jinsi yalivyokuwa yamejitosheleza. Ilimjaa zaidi hamu ya kutaka kufahamu jinsi ambavyo rafiki yake yule alivyoyapatia maisha yale.
"Shoga hebu nipe siri ya mafanikio yako" Ashura alihoji mara tu baada ya kuketi kitandani.
"Sio siri, ni KITUMBUA” Zawadi alizungumza huku akimimina wiski kwenye birauli.
"Kitumbua?" Ashura akahoji kwa mshangao.
"Ndio kitumbua, tena kitumbua cha kihindi"
"Unamaanisha nini?"
"Una maswali mingi kwani we ni polisi? hebu karibu kinywaji" Zawadi alizungumza huku akimkabidhi Ashura birauli ile iliyokuwa imejaa wisk.
TUENDELEE KESHO

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when team weupe sweger posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram