Seen Afya Kwanza

Seen Afya Kwanza Certified Doctor ⚕️👨‍⚕️
MSHAURI (Hearlth Expart 3Yrs)
Afya ya Uzazi, 🥦Mmeng’enyo
( +255 ) 757 223 987

(7)

*Iba Siri Hii | Jinsi PID Inavyo mumunya Ndoto za Uzazi wako....*Kuna ugonjwa mmoja ambao unatembea kimya kimya...Unakul...
04/09/2025

*Iba Siri Hii | Jinsi PID Inavyo mumunya Ndoto za Uzazi wako....*

Kuna ugonjwa mmoja ambao unatembea kimya kimya...

Unakula ndoto za ndoa, Unavunja tumaini la uzazi, na kugeuza furaha kuwa machozi...

*Umesikia nini kuhusu PID..!? (Pelvic Inflammatory Disease)* 🤔

Naam..! PID, Ni adui wa uzazi wa wanawake, Lakini cha kushangaza zaidi, Wanaume ndio chanzo kikuu bila hata kujua...☠️

*Ipo hivi.....*

PID (Pelvic Inflammatory Disease) Ni ugonjwa unaomchoma mwanamke —Si mwanaume.📌

Kwa sababu PID ni maambukizi yanayopanda juu kupitia njia ya uzazi ya mwanamke na kuathiri kizazi, mirija ya fallopian, na ovari...

*Hapa ndipo siri ilipo…* 👇

Mwanaume hauguwi PID, ila anaweza kuwa mhifadhi na msambazaji wa vimelea (bacteria k**a Chlamydia trachomatis na Neisseria gonorrhoeae)...

Bila dalili, bila maumivu, unajiona mzima lakini unabeba kifurushi kisichoonekana ambacho kwa kila tendo la ndoa, kinasafiri hadi kwa mke wako..🤒

*Na matokeo yake..?*

↳ Mirija inaziba kabisa, Yai haliwezi tena kusafiri...

↳ Hormone imbalance, Mfumo mzima wa mwili wa mwanamke unavurugika...

↳ Maisha Bila mtoto, Familia inageuka uwanja wa lawama, na maumivu ya kimya...

*Sasa, jiulize swali hili....*

Kwa nini wanawake wengi wakitibu PID hawaponi kabisa..?☠️

*Jibu ni gumu, lakini ukweli ni huu…* 👇

Sio PID pekee inayokuumiza, Ni usugu wa vimelea unaosababishwa na matumizi mabaya ya dawa..

↳ Dawa za kuweka ukeni bila ushauri..

↳ Sindano za mara kwa mara, Wengine wamechomwa hadi 7 days bila mafanikio...

↳ Kutumia dawa bila kufuata mpango kamili wa tiba sahihi...

*Matokeo yake?*

Vimelea vinakuwa sugu, vinakataa dawa, na ugonjwa unarudi mara kwa mara huku ndoto za uzazi zikizidi kufifia...☠️

*Siri ya ukombozi ipo hapa...* 👇

↳ Kupima kwa usahihi, Bila vipimo sahihi, tiba itakuwa ni kubahatisha.

↳ Kufuata ushauri wa daktari, Sio kujitibu ovyo ovyo kwa kununua dawa maduka ya dawa au mitandaoni...

↳ Wanaume kushiriki matibabu, Kwa sababu chanzo mara nyingi kiko upande wao..

*NB:* K**a wanaume tunalo jukumu la kulinda wake zetu.

K**a familia tunalo jukumu la kulinda vizazi vyetu.

Na k**a jamii, tunalo jukumu la kuvunja ukimya, ili PID isiendelee kuua ndoto za uzazi....

Hii sio tu elimu, ni wito wa mapinduzi ya afya ya uzazi, Tuchukue hatua, Leo...🫡 K**a upo na mimi nipe Reaction 👍 Kisha ni follow Seen Afya Kwanza kujifunza zaidi

Address

Ilala Boma
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Seen Afya Kwanza posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Seen Afya Kwanza:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram