15/02/2026
Kuna magonjwa kadhaa ya mfumo wa uzazi na homoni ambayo mara nyingi huchangia kuchelewa kupata mimba au ugumba kamili. Kitaalamu, athari hutokea kupitia kuvurugika kwa ovulation, uharibifu wa mirija ya uzazi, matatizo ya uterasi, au upungufu wa ovari. Haya ndiyo muhimu zaidi kuwa makini nayo
1. Polycystic O***y Syndrome (PCOS)
Hili ni tatizo la homoni linalosababisha ovulation kutotokea mara kwa mara au kutotokea kabisa. Wanawake wengi huwa na hedhi zisizo za kawaida, chunusi, kuongezeka uzito, au nywele nyingi usoni/mwilini. Kiini cha tatizo mara nyingi ni insulin resistance, inayochochea androjeni kuongezeka na kuvuruga ukuaji wa yai.
2. Pelvic Inflammatory Disease (PID)
Maambukizi ya muda mrefu kwenye kizazi na mirija ya uzazi, mara nyingi yanayotokana na magonjwa ya zinaa. Athari kubwa ni kuziba au kuharibu mirija (tubal factor infertility). Mara nyingi huanza kimya bila dalili kali, lakini madhara yake ni ya kudumu.
3. Endometriosis
Hali ambapo tishu za ndani ya uterasi hukua nje ya uterasi. Husababisha maumivu makali ya hedhi, maumivu wakati wa tendo la ndoa, na wakati mwingine cyst za ovari. Inaweza kuathiri ubora wa mayai na mazingira ya upandikizaji wa kijusi.
4. Uterine fibroids
Vivimbe visivyo vya saratani ndani ya mfuko wa uzazi. Kulingana na ukubwa na mahali vilipo, vinaweza kuzuia upandikizaji wa mimba au kusababisha mimba kutoka mapema.
5. Hyperprolactinemia
Kuongezeka kwa homoni ya prolactin kunazuia ovulation. Sababu zinaweza kuwa uvimbe mdogo kwenye tezi ya pituitari au dawa fulani.
6. Thyroid disease (hypothyroidism au hyperthyroidism)
Tezi ya thyroid isiyofanya kazi vizuri huathiri mzunguko wa hedhi, ovulation, na hata uwezo wa kijusi kukua vizuri.
7. Premature ovarian insufficiency
Kupungua mapema kwa hifadhi ya mayai (ovarian reserve) kabla ya umri wa miaka 40. Hedhi hupungua au kukoma mapema, na uwezekano wa mimba hupungua sana.
8. Magonjwa ya zinaa sugu
Maambukizi k**a Chlamydia na Gonorrhea yanaweza kuharibu mirija bila dalili za wazi.
Je ni lipi kati ya haya ndio linakusumbua?
☎️+255765770498