TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Ilala.

Tukutane leo live tiktok katika ukurasa wa   Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka TFNC, Dkt. Esther N...
11/03/2026

Tukutane leo live tiktok katika ukurasa wa Mkurugenzi wa Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe kutoka TFNC, Dkt. Esther Nkuba atakuwepo kuzungumzia tatizo la upungufu wa damu kwa watoto wa k**e na suluhisho lake.

Usikose kufuatilia

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa kushirikiana na Wadau wengine wa urutubishaji kupitia ufadhili wa Shirika la Um...
10/03/2026

Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania kwa kushirikiana na Wadau wengine wa urutubishaji kupitia ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) wako mbioni kukamilisha program ya kitaifa ya urutubishaji wa vyakula ikiwemo uwekaji wa madini joto kwenye chumvi.

Kukamilika kwa mpango huo kunatajwa kutasaidia kuhakikisha suala la uongezaji wa viritubishi kwenye vyakula linafanyika kwa upana zaidi ili kuwafikia watu wengi na utaenda kuwaelekeza watekelezaji nini kifanyike kwenye eneo la uongezaji viritubishi kwenye chakula.

Wakizungumza wakati wa kikao kazi cha kuthibitisha mpango huo kilichofanyika Mkoani Morogoro, wadau mbalimbali walioshiriki kwenye kikao hicho wameipongeza Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Pamoja na timu iliyoshiriki katika kuandaa mpango huo hadi kufikia hatua ya mwisho kwani unaenda kusaidia kuimarisha eneo la urutubishaji nchini, na ni mpango ambao wadau wengi wa urutubishaji walikuwa wanauhitaji.

Tukiwa katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani tupate ujumbe kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Chakula na Li...
08/03/2026

Tukiwa katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani tupate ujumbe kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Dkt. Germana Leyna akisema kuwa "Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, tunasisitiza kuwa, lishe bora kwa wanawake ni uwekezaji wa moja kwa moja katika rasilimali watu. Bila wanawake wenye afya na lishe bora, hatuwezi kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo 2050"

Tunawatakia wanawake wote heri katika kuadhimisha na kusheherekea Siku ya Wanawake Duniani
08/03/2026

Tunawatakia wanawake wote heri katika kuadhimisha na kusheherekea Siku ya Wanawake Duniani

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Esther Nkuba, Mkurugenzi...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Esther Nkuba, Mkurugenzi Idara ya Elimu na Mafunzo ya Lishe akisema kuwa “Kumpa mtoto wako lishe bora ni kutimiza ndoto yake na kupanua ubunifu wake.
Kumbuka kuwa uwezo mkubwa wa mtoto wako unaanzia kwenye chakula kilicho kwenye sahani yake.
Lea kizazi chenye nguvu, werevu, na chenye afya njema. Kinamama Tunaweza!"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Devotha Mushumbusi, Afis...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Devotha Mushumbusi, Afisa Mtafiti - Lishe akisema kuwa “Mwanamke anao mchango mkubwa katika kuhakikisha chakula ni salama kwa matokeo chanya ya kilishe"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Wessy Meghji, Afisa Mtaf...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Wessy Meghji, Afisa Mtafiti - Lishe akisema kuwa “Kizazi cha haki na usawa hujengwa na mwanamke anayepanga na kusimamia vyema lishe bora ya familia yake"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Mary Mvungi, Mwanasheria...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Mary Mvungi, Mwanasheria akisema kuwa “Mwanamke ni kitivo cha ubora katika kupanga na kusimamia maendeleo endelevu ndani ya familia"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Upendo Mlengu, Afisa Mta...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Upendo Mlengu, Afisa Mtafiti - Takwimu akisema kuwa “Katika siku ya Wanawake Duniani, tunatambua umuhimu wa wanawake katika kuboresha lishe ya familia na jamii, Takwimu sahii hutusaidia kuelewa hali ya lishe na kupanga hatua madhubuti za kuwawezesha wanawake na kuboresha afya ya jamii"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Elizabety Lyimo, Afisa M...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Elizabety Lyimo, Afisa Mtafiti - Lishe akisema kuwa “Epuka magonjwa sugu yasiyoambukiza k**a vile kisukari, magonjwa ya moyo na saratani kwa kula vyakula visivyo na sukari, mafuta na chumvi kwa wingi"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Adeline Munuo, Afisa Mta...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Adeline Munuo, Afisa Mtafiti - Mtafiti akisema kuwa “Tembea angalau hatua 7000 kwa siku ili uwe na afya njema na kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza, Tabia bwete siyo poa"

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Shufaa Uvira,  Afisa Mta...
07/03/2026

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake, tupate ujumbe kutoka kwa mwanamke wa nguvu Shufaa Uvira, Afisa Mtafiti akisema kuwa “Mwanamke mwenye afya bora huanza na maamuzi bora; na maamuzi bora huanza na takwimu sahihi"

Address

Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category