TFNC Tanzania

TFNC Tanzania Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from TFNC Tanzania, Nutritionist, Ilala.

Tutakukumbuka daima kwa kuhamasisha ushiriki wa sekta katika mapambano dhidi ya utapiamlo hususani sekta binafsi katika ...
12/12/2025

Tutakukumbuka daima kwa kuhamasisha ushiriki wa sekta katika mapambano dhidi ya utapiamlo hususani sekta binafsi katika utekelezaji wa programu ya uongezaji virutubishi katika chakula kwa lengo la kuzuia na kudhibiti tatizo la upungufu wa madini na Vitamini.

Mhe. Dkt. Rajabu Rutengwa, Mkuu wa Mkoa Mstaafu Katavi, Tanga na Morogoro (wa kwanza kulia) akiwa na wajumbe kutoka Taas...
11/12/2025

Mhe. Dkt. Rajabu Rutengwa, Mkuu wa Mkoa Mstaafu Katavi, Tanga na Morogoro (wa kwanza kulia) akiwa na wajumbe kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji (wa pili kulia) Dkt. Germana Leyna wakijadili namna TFNC inavyoweza kujenga uwezo na kuongezeka ufanisi wa wataalamu wa sekta mtambuka katika kutekeleza Mkakati Jumuishi wa Lishe wa pili (NMNAP II ) katika ngazi za Mikoa na Halmashauri. Majadiliano hayo yamefanyika 11 Desemba, 2025 katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa TFNC.

09/12/2025
MAFUNZO KWA WATAALAMU WA MAABARA.Wafanyakazi wa Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), wamepatiwa  mafu...
05/12/2025

MAFUNZO KWA WATAALAMU WA MAABARA.

Wafanyakazi wa Maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), wamepatiwa mafunzo ya kanuni bora za ufanyaji Kazi kwenye maabara yaani GLP na GCLP, ikiwa ni sehemu ya kuboresha usimamizi, ubora na usalama katika Maabara ya Chakula na Lishe iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yametolewa na mwezeshaji Prof. Reginad Kavishe kutoka KCMC University na yamefanyika mkoani Morogoro katika Chuo cha Kilimo cha Sokoine.

Mafunzo ya uandaaji bora wa chakula kwa watoa huduma ya chakula kutolewa tarehe 11-12 Februari, 2026 mkoani MorogoroKwa ...
04/12/2025

Mafunzo ya uandaaji bora wa chakula kwa watoa huduma ya chakula kutolewa tarehe 11-12 Februari, 2026 mkoani Morogoro

Kwa maelezo zaidi piga namba hizi; 0623 752 063 au 0683 467 454

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania  Dkt. Germana Leyna (wa nne kulia mstari wa mbele) akiwa kat...
02/12/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna (wa nne kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine wa mafunzo ya namna ya kuratibu mikakati jumuishi ya kisekta kwenye lishe, mafunzo yaliyofanyika hivi karibuni nchini Zimbabwe.

Mafunzo hayo yalifanyika na kuratibiwa na Jukwaa la Vuguvugu la Lishe (Scaling Up Nutrition Network)

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania  Dkt. Germana Leyna (wa nne kulia mstari wa mbele) akiwa kat...
02/12/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania Dkt. Germana Leyna (wa nne kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wengine wa mafunzo ya namna ya kuratibu mikakati jumuishi ya kisekta kwenye lishe, mafunzo yaliyofanyika hivi karibuni nchini Zimbabwe.

Mafunzo hayo yalifanyika na kuratibiwa na Jukwaa la Vuguvugu la Lishe (Scalling Up Nutrition Network)

SIKU YA UKIMWI DUNIANI
01/12/2025

SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI...
26/11/2025

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (WAVIU) na TB wakiwasilisha kazi za vikundi kuelezea sababu zinazopelekea WAVIU na wagonjwa wa TB kupata matatizo ya kilishe nchini.

Mafunzo haya yanatolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kwa watoa huduma za afya, maafisa ustawi na maaendelo ya jamii.

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Abela Twinomujuni akiwasilisha mada kuhusu uhusi...
25/11/2025

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Abela Twinomujuni akiwasilisha mada kuhusu uhusiano wa Lishe, UKIMWI na TB wakati wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB yanayotolewa na TFNC kwa watoa huduma za afya, maafisa usawi na maaendelo ya jamii katika ukumbi wa TFNC jijini Dar es Salaam

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Elizabeth Lyimo akiwasilisha mada kuhusu Masuala...
25/11/2025

Afisa Lishe Mtafiti kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Elizabeth Lyimo akiwasilisha mada kuhusu Masuala ya Msingi ya Lishe wakati wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB yanayotolewa na TFNC kwa watoa huduma za afya, maafisa usawi na maaendelo ya jamii katika ukumbi wa TFNC jijini Dar es Salaam.

Washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB wak...
25/11/2025

Washiriki wa mafunzo ya tathimini ya lishe, unasihi na huduma za lishe kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI na TB wakicheza mchezo wa karata za kupanga makundi ya chakula wakati wa mafunzo hayo yanayotolewa kwa siku nne (25 - 28, Novemba, 2025) na TFNC kwa watoa huduma za afya, maafisa usawi na maaendelo ya jamii ili kuwaongezea ufanisi katika majukumu yao ya kila siku.

Address

Ilala

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

0658990996

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TFNC Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category