15/02/2026
Afisa Elimu Watu Wazima Manispaa ya Temeke, Sister, Mwalimu Donasiana Njuu akimwakilisha Afisa Elimu Manispaa kufungua kikao cha kuhamasisha wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule ya msingi Kilamba kuchangia mpango wa chakula shuleni ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa Afya na Lishe unaotekelezwa katika shule za msingi 15 za Manispaa ya Temeke.
Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania, Manispaa ya Temeke na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP).