18/03/2026
TFNC, NBS, MUHAS NA IHI YATAMBULISHA B MRADI WA KUIMARISHA MFUMO WA UFUATILIAJI VIASHIRIA VA LISHE TANZANIA (MNBi-URT)
Na, Mwandishi Wetu
Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Taasisi ya Utafiti Ifakara (IHI) kupitia ufadhili wa Gates Foundation, imebuni mradi wa Kuimarisha Mfumo wa Ufuatiliaji wa Viashiria vya Lishe Nchini kwa kutumia mabaki ya sampuli za tafiti na hospital katika kupima na kukadiria viwango vya aina ya upungufu wa vtamini na madini kwa wanawake waliom katika umri wa kuzaa.
Mradi huo utasaidia kukabiliana na changamoto za Uhaba wa takwimu za lishe hususani zinazohusu upungufu wa Vitamini na Madini nchini. Aidha mradi huu unatarajia kutoa taarifa za lishe kwa wakati, kwa gharama nafuu na kwa uendelevu kupitia mifumo mingine ya kisekta ya Afya na TAMISEMI ambayo tayari imesimikwa.
Akizungumza wakati wa kutambulisha mradi huo kwa Kamati ya kitaifa ya watalaam ya usimamizi na ushauri wa masuala ya lishe, iliyokutana tarehe 16 Machi 2026 katika Ofisi za Waziri Mkuu jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Dkt. Germana Leyna, amesema mradi huo pia unatarajia kuimarisha uwezo wa maabara ya Taasisi ya Chakula na Lishe, kuchakata mabaki ya sampuli bila kupeleka nje ya nchi, sambamba na hilo mradi huu utagharamia upatikanaji wa ithibati za kikanda na kimataifa katika uchakataji wa sampuli za chakula na kibailojia.
“Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha sekta, mikoa, halmashauri na taifa kwa ujumla kupanga mikakati na afua za lishe kwa kutumia takwimu na taarifa zinazozalishwa na mifumo ya nchi bila kutegemea ufadhili kutoka nje.” Alisema Dkt. Germana.
.tanzania .sbu