St. Gaspar Referral and Teaching Hospital

St. Gaspar Referral and Teaching Hospital The St. Gaspar Referral and Teaching Hospital is a national referent center in Tanzania.

"Cure, educate, console" is the motto of the hospital and it expresses the true identity and the real nature of the mission of the hospital.

Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Tawi la Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi,...
28/03/2026

Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE), Tawi la Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi, kimefanya kikao chake leo tarehe 28 Machi 2026 kwa lengo la kufanya uchaguzi wa viongozi wapya katika nafasi mbalimbali ndani ya chama hicho.

Katika uchaguzi huo, Katibu wa TUGHE Mkoa wa Singida, Ndg. Tamsoni Msighati, alimtangaza Bi. Iliminatha Herman Kway kuwa Mwenyekiti mpya wa TUGHE Tawi hilo, huku Bi. Idagiovana Wilson akiendelea na nafasi yake ya Katibu wa chama.

Aidha, katika zoezi hilo, wajumbe nane walichaguliwa, pamoja na Mwenyekiti na Katibu wa Kamati ya Wanawake, na mwakilishi wa vijana wa TUGHE katika Tawi la Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi.

Awali, Ndg. Tamsoni Msighati alitumia fursa hiyo kutoa elimu kwa anachama kuhusu umuhimu wa Watumishi kujiunga na chama hicho, akisisitiza kuwa TUGHE ina jukumu la kusimamia haki za wafanyakazi, kutoa msaada wa kisheria, kuwawakilisha wanachama katika kushughulikia changamoto za kiutendaji, kutoa fursa ya kujadili stahili zao, pamoja na kuimarisha nguvu ya pamoja miongoni mwa watumishi.

πŸ”” KAMBI MAALUMU YA MADAKTARI BINGWA WA UPASUAJI BANDIA NA UPASUAJI REKEBISHIπŸ“… Tarehe: 10 – 18 Aprili 2026πŸ“ Mahali: Hospi...
25/03/2026

πŸ”” KAMBI MAALUMU YA MADAKTARI BINGWA WA UPASUAJI BANDIA NA UPASUAJI REKEBISHI

πŸ“… Tarehe: 10 – 18 Aprili 2026

πŸ“ Mahali: Hospitali ya Rufaa na Mafunzo St. Gaspar – Itigi

πŸ‘¨ Huduma zitatolewa na:
β€’ Madaktari bingwa bobezi kutoka Marekani
β€’ Kwa kushirikiana na madaktari Bingwa wa St. Gaspar-Itigi

πŸ“ž Mawasiliano:
β€’ 0784 738 432
β€’ 0764 077 625
β€’ 0769 956 853
β€’ 0755 454 040

πŸ“ŒπŸ“ŒHUDUMA HII NI BURE

Chanjo ya Matone ya Polio kwa watoto chini ya miaka 10 imeanza kutolewa leo  Machi 24 - 27, 2026,Hospitali ya Rufaa na M...
24/03/2026

Chanjo ya Matone ya Polio kwa watoto chini ya miaka 10 imeanza kutolewa leo Machi 24 - 27, 2026,

Hospitali ya Rufaa na Mafunzo St.Gaspar-Itigi inatoa chanjo hii muhimu katika kampeni hii ya kitaifa ya utoaji wa chanjo ya polio

Wizara ya Afya Tanzania

iπŸ”” KAMBI MAALUMU YA MATIBABU YA KIBINGWA πŸ””(GOITRE NA HERNIA)Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi inakutan...
23/03/2026

iπŸ”” KAMBI MAALUMU YA MATIBABU YA KIBINGWA πŸ””(GOITRE NA HERNIA)

Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi inakutangazia rasmi kambi maalumu ya matibabu ya kibingwa kwa wagonjwa wa Goitre na Hernia.

πŸ“… Tarehe: 20 – 24 Aprili 2026

πŸ“ Mahali: Hospitali ya Rufaa na Mafunzo St. Gaspar – Itigi

πŸ‘¨βš•οΈ Huduma zitatolewa na:
β€’ Madaktari bingwa bobezi kutoka Ulaya
β€’ Kwa kushirikiana na madaktari bingwa wa St. Gaspar-Itigi

πŸ’° Gharama za Matibabu:
β€’ Watu wazima: Shilingi 50,000/=
β€’ Watoto: Shilingi 25,000/=

πŸ“ž Mawasiliano:
β€’ 0784 738 432
β€’ 0764 077 625
β€’ 0769 956 853
β€’ 0755 454 040

πŸ‘‰ Usikose fursa hii adhimu ya kupata matibabu ya kibingwa karibu nawe!
πŸ‘‰ Huduma bora, salama na kwa gharama nafuu.

DcHalmashauri ya Wilaya ya ManyoniWizara ya Afya TanzaniaHospitali ya rufaa mkoa wa dodomaMuhimbili University of Health and Allied Sciences

20/03/2026
Wanafunzi wa Kidato cha Sita kutoka Shule ya Sekondari Itigi wametembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa na Ma...
20/03/2026

Wanafunzi wa Kidato cha Sita kutoka Shule ya Sekondari Itigi wametembelea Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi kwa lengo la kuwafariji wagonjwa na kuwapatia zawadi mbalimbali.

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa na Mafunzo ya St. Gaspar – Itigi unathamini na kupongeza moyo wao wa huruma na kujitoa, uliodhihirishwa kupitia tendo hili jema walilolifanya leo.

DcHalmashauri ya Wilaya ya ManyoniWizara ya Afya TanzaniaHospitali ya rufaa mkoa wa dodomaMuhimbili University of Health and Allied Sciences

Siku ya kimataifa ya Afya ya Kinywa na MenoTunawakaribisha katika Klinikiyetu ya Kinywa na Meno kwa huduma zifuatazo..1....
20/03/2026

Siku ya kimataifa ya Afya ya Kinywa na Meno

Tunawakaribisha katika Klinikiyetu ya Kinywa na Meno kwa huduma zifuatazo..

1. Kuziba meno yaliyotoboka
2. Matibabu ya mzizi wa jino
3. Kusafisha meno
4. Upasuaji wa kinywa na Taya
5. Huduma ya meno bandia
6. Matibabu ya meno na Taya yaliyoathiriwa na ajali
7. Kupanga meno
8. Kutoa meno yaliyooza

DcHalmashauri ya Wilaya ya ManyoniWizara ya Afya TanzaniaHospitali ya rufaa mkoa wa dodomaMuhimbili University of Health and Allied Sciences

18/03/2026

Hospitali ya rufaa na Mafunzo St.Gaspar-Itigi inawatangazia watu wote kuwa kutakuwa na KAMBI MAALUMU YA MATIBABU YA KIBI...
18/03/2026

Hospitali ya rufaa na Mafunzo St.Gaspar-Itigi inawatangazia watu wote kuwa kutakuwa na KAMBI MAALUMU YA MATIBABU YA KIBINGWA YA MAGONJWA YA GOITA PAMOJA NA NGIRI YA KUSHUKA {HERNIA} kuanzia tarehe 20 - 24/4/2026.
Kambi hii itaendeshwa na madaktari bingwa bobezi kutoka ulaya kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka hospitali yetu kwa gharama nafuu sana..
1. Wakubwa sh. 50,000/=
2. Watoto sh. 25,000/=
Dc Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni - Mitunduruni Singida Ked Man MpondoWizara ya Afya TanzaniaMuhimbili University of Health and Allied Sciences

Mazingira safi ndani na nje ya hospitali huchangia huduma bora na usalama wa wagonjwa, wahudumu na wageni. Kila mmoja an...
14/03/2026

Mazingira safi ndani na nje ya hospitali huchangia huduma bora na usalama wa wagonjwa, wahudumu na wageni.

Kila mmoja ana wajibu wa kutunza usafi ili kulinda mazingira ya hospitali.

13/03/2026

Address

Itigi
12

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when St. Gaspar Referral and Teaching Hospital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to St. Gaspar Referral and Teaching Hospital:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category