09/02/2026
Mmoja wa wanafunzi wangu niliyemsaidia kupata kemikali za kuanzia uzalishaji, leo tayari ameanza rasmi biashara yake.
Nikiwa bado njiani kwenye safari yangu, alinipigia akisema amekwama kupata baadhi ya malighafi muhimu kwa ajili ya uzalishaji wake. Nikamwambia kuwa sikuwa mjini, lakini nitakaporudi nitaangalia namna ya kumsaidia.
Mara tu niliporejea Ubungo(Dar es Salaam) mwezi Januari, alinikumbusha tena. Nikachukua muda wangu, nikaenda sokoni, nikamnunulia kemikali zote alizohitaji.
Nilimsindikiza hatua kwa hatua kwenye mchakato mzima wa uzalishaji, na matokeo yakawa bora kabisa.
Jana aliniletea picha za bidhaa zake na kwa kweli nilifurahi sana kuona ndoto yake inaanza kuchanua.
Namtakia mauzo makubwa na baraka tele.
Ufungashaji wake uko daraja la juu kabisa.
Darasa letu lijalo la mafunzo ya uzalishaji mtandaoni linaanza tarehe 23 Februari.
Ada ya ushiriki: 15,000/=
Kwa mawasiliano: Piga simu au WhatsApp: 0679 544 671
©️ TabasamuLetu Hub
CEO – Tabasamu Letu Hub
Ninatengeneza na kuuza bidhaa za usafi, nywele, perfume na ngozi.
Pia nawafundisha watu kuanzisha uzalishaji wao kuanzia sifuri hadi sokoni.