10/03/2026
MY QUIET PAIN JOURNEY
(Part 8: The Call I Didn’t Return)
Nakumbuka vizuri sana tukio hili.
Na kwa kweli, sitaweza kulisahau kwenye safari ya maisha yangu ya utafutaji wa riziki.
Ilikuwa ni Desemba 11, 2023.
Usiku huo nilikuwa nimekaa nyumbani nikiwa na utulivu wa uchovu baada ya siku ndefu ya pilikapilaka za kazi zangu za ujasiriamali wa sabuni na bidhaa za usafi.
Kufikia kipindi hicho, mambo yalikuwa yameanza kusonga mbele kwa namna ambayo miaka michache nyuma nisingeweza hata kuifikiria.
Nilikuwa nimefanikiwa kufungua ofisi kubwa ya uzalishaji wa bidhaa za usafi—sabuni, cleaners, na pia huduma za cleaning service kwa majumbani, kwenye sites za ujenzi na maofisini.
Kwa wakati huo, nilikuwa nasimamia timu ya watu 8. Tulifanya kazi k**a familia. Kila mmoja alikuwa na jukumu lake, na tulijitahidi kuhakikisha kila huduma tunayotoa ina ubora na heshima.
Mbali na hilo, tulikuwa tumefungua pia Tabasamu Hub Café, sehemu ndogo lakini yenye hadhi ya vyakula vya breakfast na natural smoothie pale Goba Njia Panda–Barabara ya Makongo.
Ofisi yetu ya uzalishaji na huduma za cleaning service ilikuwa ndani ya workshop pale Mtaa wa Muhimbili Njia Panda, kuelekea Njia Nne Tegeta.
Kwa kifupi, mambo yalikuwa yanaanza kujengeka.
Timu nzima ilijituma. Tuligawana majukumu, tuligawana mapato kwa uwazi, na tulianza kuweka akiba kwa ajili ya ukuaji wa taasisi yetu ndogo ya Tabasamu Letu Hub Clinic.
Nakumbuka vizuri mwezi huo tulifungua savings account ya taasisi katika tawi la NMB Mbezi Louis, Dar es Salaam, na akiba yetu ilifikia zaidi ya milioni 12 za Kitanzania.
Kwa mtu aliyewahi kuanza kwenye chumba kimoja kisichokamilika…
hii ilikuwa hatua kubwa.
Lakini maisha yana namna yake ya kukukumbusha kwamba safari ya mwanadamu ina sura nyingi.
Usiku huo, majira ya saa 9 usiku, nilishtuka kidogo usingizini kwa sababu nilihitaji kwenda kujisaidia.
Nilichukua simu yangu na kugusa kioo chake nilikuwa nimeweka sensitive touchpoint ili kuona saa bila hata kuifungua kabisa.
Nilipoangalia, nikagundua kuna missed call.
Nilifungua kuona ni nani aliyepiga.
Ilikuwa ni namba ya dada yangu mkubwa.
Nilishtuka kidogo.
Lakini nilipoangalia muda wa simu ile, niliona alipiga saa 7 usiku.
Nikajiuliza kimoyo moyo;
“Ni nini kilimfanya anipigie usiku ule?”
Lakini kwa sababu nilikuwa bado nusu usingizini, nilijiambia;
“Nitamtafuta asubuhi nikiamka.”
Nikanyanyuka nikaenda chooni, nikarudi kitandani, na usingizi ukachukua nafasi tena.
Sikujua kwamba ule ulikuwa uamuzi mdogo ambao ungekuwa mzito moyoni mwangu baadaye.
Asubuhi yake nilishtuka saa 2. Nilikuwa tayari nimechelewa kwenda ofisini. Nikajiandaa haraka kuoga, kuvaa, kisha nikakimbia kwenda kazini.
Kwa bahati mbaya, hata nikiwa njiani sikumpigia dada yangu. Nikajiambia tu;
“Nikipata utulivu ofisini nitampigia.”
Wakati shughuli za ofisi zikiendelea, majira ya saa 5 asubuhi, nilipigiwa simu na namba mpya ambayo sikuwa nimeihifadhi.
Kwa uzoefu wangu, nilidhani huenda ni mteja.
Nikapokea.
Mazungumzo yetu yalikuwa mafupi lakini mazito.
Yeye: “Hallo.”
Mimi: “Hallo, habari ya leo ndugu.”
Sauti ilikuwa ya mwanaume.
Yeye: “Naongea na Msirikale? Kaka yake fulani…” akalitaja jina la dada yangu mkubwa.
Moyo wangu ukashtuka kidogo.
Mimi: “Ndiyo, ni mimi. Kuna habari gani?”
Yeye: “Dada yako ni mgonjwa. Yuko mahututi hapa hospitali Tabora. Ameweza kutaja namba yako kwa tabu ili tukupigie. Inahitajika pesa ya matibabu.”
Nilipata kigugumizi kwa sekunde kadhaa.
Kisha nikasema...
“Sawa, hamna tatizo. Niambieni kiasi cha bill na hali yake ipoje. Tafadhali naomba niongee naye.”
Jibu lilikuwa zito.
“Hawezi kuongea. Hali yake siyo nzuri.”
Nilijikaza.
“Nitumieni bill ya matibabu. Anzeni kumpa huduma. Tutawasiliana.”
Simu ikakatwa.
Lakini bado sikuelewa uzito wa hali ile. Nilidhani labda ni hali ya kawaida tu ya ugonjwa.
Nikapiga simu ya dada yangu moja kwa moja. Simu ilipokelewa na mwanamke mmoja ambaye nilimfahamu k**a rafiki yake wa karibu.
Nilipomuuliza hali ikoje, sauti yake ilianza kutetemeka.
“Kaka… hali siyo nzuri.”
Akalizimika kulia kwa kwikwi.
Moyo wangu ukaanza kubadilika.
Nikamtafuta rafiki mwingine wa dada yangu; kijana mmoja aliyekuwa karibu sana naye. Nilipomuuliza kilichotokea, alinijibu kwa uwazi:
“Ni kweli tupo hospitali ya Mission Tabora. Hali yake siyo nzuri. Madaktari wanasema ni poison—sumu ya mazao. Yuko chumba cha uangalizi maalum.”
Nilimwambia;
“Tafadhali tafuta namba ya baba kwenye simu yake. Ninaomba uongee nae mzazi wetu.”
Niliongeza pia;
“Usijali kuhusu bill ya hospitali. Nitalipia.”
Dakika k**a 30 baadae, ile namba ya daktari ilinipigia tena.
“Ndugu Msirikale, upo huru tuongee?”
“Ndio, sema ndugu.”
Alikaa kimya kwa sekunde kadhaa.
Kisha akasema kwa sauti tulivu sana:
“Tumejitahidi kwa uwezo wetu kumhudumia mgonjwa ambaye ni dada yako… lakini hatujaweza kurejesha matumaini ya maisha yake.”
Kisha akasema maneno ambayo bado yanagonga moyo wangu hadi leo.
“Dada yako… amefariki dunia. Pole sana.”
Kwa sekunde chache sikuweza kuongea.
Nilihisi k**a sauti imeondoka ndani yangu.
Nilifikiria kitu kimoja tu...
Ile missed call ya saa 7 usiku…
ilikuwa simu yake ya mwisho kwangu.
Nilijilaumu sana siku hiyo.
Kwa nini sikumpigia?
Kwa nini niliahirisha hadi asubuhi?
Ofisini hali haikuwa nzuri kabisa.
Nililazimika kukabidhi majukumu kwa timu yangu ili waendelee na kazi. Nilituma taarifa kwa ndugu na jamaa, kisha siku hiyo hiyo Desemba 11 nikakata tiketi ya safari kutoka Dar es Salaam kwenda Tabora.
Safari ile haikuwa tu ya kwenda kwenye msiba.
Ilikuwa safari ya kunikumbusha ukweli mmoja mkubwa wa maisha;
Muda ni mali ambayo hatuna udhibiti nayo.
Na labda ndiyo sababu leo nimechagua kutumia muda wangu kusaidia wengine kujenga maisha yao kwa njia ya heshima.
Kwa washiriki wa Marathon Acquisition SMP2026, nataka mfahamu kitu kimoja...
Hii sio tu program ya kujifunza kutengeneza sabuni.
Ni jukwaa la kujifunza;
• kujenga chanzo cha kipato
• kupata mwongozo wa one-on-one mentorship
• kupata malighafi salama za uzalishaji
• kujifunza kujenga brand yako
• kuongeza mauzo kupitia soko la kidigitali
Program hii bado inaendelea, na watu wengi tayari wameanza kuona mwanga wa mfumo wa kujitegemea.
Na mimi ninaendelea kusimama, kufundisha, na kushirikisha kile ambacho maisha yamenifundisha.
Kwa sababu safari yangu bado haijaisha.
Bado inaendelea…
Usikose kupata mwendelezo.
To be continued…