19/08/2025
SHINE Project ni mradi uliotekelezwa na Comunità Solidali nel Mondo (COM-SOL TZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na PORALG, ukiungwa mkono na Italian Agency for Development Cooperation (AICS) kuanzia mwaka 2023 hadi sasa.
Mradi huu umejikita katika:
✅ Kushughulikia changamoto za kifafa (epilepsy) na lishe duni (malnutrition), hasa kwa watu wenye ulemavu.
✅ Kuimarisha huduma katika kliniki maalum nne zinazotoa huduma za kifafa na lishe.
✅ Kutoa mafunzo kwa mfumo wa cascade katika mikoa 10 ya Tanzania kwa wahudumu wa afya na wadau wa jamii.
✅ Kuandaa mapendekezo ya sera na vitendo kwa ajili ya huduma jumuishi za afya.
Mnamo 18 Julai 2025, TAEFI ilishiriki katika Final Conference ya SHINE Project jijini Dar es Salaam. Ushiriki huu ni hatua muhimu kwani unawakilisha sauti za watu wanaoishi na kifafa na changamoto za ulemavu katika mjadala wa kitaifa kuhusu huduma jumuishi za afya.
Kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali, tunajivunia kuona mapendekezo ya mwisho ya mradi huu yakizinduliwa rasmi, yakilenga kuimarisha huduma za kifafa na lishe nchini.
👉 TAEFI itaendelea kusimama pamoja na wapambanaji wa kifafa kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma.
💜