Rojorojo Natural Home Remedies

Rojorojo Natural Home Remedies Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Rojorojo Natural Home Remedies, Medical Center, Muhimbili university of health and allied sciences, Kinondoni.

20/11/2017

MAISHA NI SAWA NA UKUAJI WA MMEA

Wengi wetu huongelea mafanikio katika nyanja zote za maisha.
Ukimuuliza kijana yeyote njozi zake ni mafanikio tu!
Kila mtu hupenda mafanikio na maisha ya raha na furaha daima.

Hata hivyo pamoja na kutaka mafanikio bado wengi hawavifikii vilele vya mafanikio kwa sababu hawazingatii kanuni za msingi za mafanikio, iwe katika ndoa, biashara, elimu, uongozi, utumishi, na mengineyo.

Hebu leo tuangalie kanuni chache za mmea kufikia kilele cha mafanikio;

Shambani mwangu niliipanda punje moja ya mahindi. Baada ya siku chache ilivimba na hatimaye polepole ikachipua kwa kuipasua ardhi.Nilipoiangalia kwa makini niliona siku si nyingi punje ile imeoza na kuishia kabisa. Ndipo nikashangaa sana kuona mche mwororo umechipia na ghafla ukakua kufuatia mvua zilizoendelea kuunywesha maji.
Ngoja nikuambiae ndugu unahitaji mvua ili uweze kufanikiwa.
Unahitaji watu wa kuchochea kufikia kilele cha mafanikio yako!

Mche huo ulipitia hatua kadha wa kadha hadi kufikia kimo cha kuzaa.
Mche huu hata hivyo ulikabiliwa na wadudu waharibifu na ulikuwa ukiharibiwa mara nyingi na kudhoofu sana lakini uliendelea kuvumilia na haukuacha kutoa majani mapya baada ya siku si nyingi za mashambulizi.
Sikiliza maadui ni sehemu ya hatua ya kufikia mafanikio yako... Ustawi wa mmea uliwavutia wadudu ili waushambulie!

Wakati mwingine mvua zilizidi sana na mmea badala ya kukua ulidumaa siyo hivyo tu bali pia jua lilipozidi sana ulikaribia kukauka.
Yote hayo yalikuwa ni mapito ambayo mche huu ulipaswa kuyapitia ili kufikia kilele cha mafanikio.

Hatimaye miezi ikaenda na ndipo mmea huu kwa mara ya kwanza ulionekana umeweka mbelewele na kwa pembeni ukiwa umebeba matunda.
Ulionekana kunawiri na hata wapita njia waliutamani hata wakadhani mmea huu ulikuwa haujapitia shida ya uhaba wa mvua, wadud,ukungu, jua kali na ardhi isiyo na rutuba.

Mkulima aliutunza kwa matazamio makubwa.
Kumbuka katika magumu yote haya mkulima anautunza mmea...yaani Mungu!

Na sasa twashuhudia makumi mengi ya punje yakiwa yamepangwa kwa ustadi mkubwa. Iwapo tulipanda mbegu moja lakini sasa tumevuna mamia ya punje kwa hakika hiki ni kilele cha mafanikio kwa mmea huu.

Lakini cha ajabu huu mmea umetoa vyote kwetu na haukuwa na choyo ulipofikia kilele cha mafanikio.

Cha ajabu mmea huu ulikubali kufa ili uvunwe na kutoa mazao yake yaliyokomaa.
Huu mmea haukuwa mbinafsi hata ulipofikia kwenye kilele cha mafanikio.

Mbegu yenyewe ilikufa huko ardhini na haikuonekana tena, nauliza iko wapi mbegu niliyoipanda mwanzoni na imekuwaje nimeipoteza milele na kuipata ikiwa makumi mengi?
Katika kufikia kilele cha mafanikio wakati mwingine kubali kupoteza, sikiliza hupotezi bali unawekeza!

Kubali kupitia hatua za changamoto na magumu. Punje ililazimika kupasua ardhi ili itoke. Ni kweli punje ingekata tamaa ingebaki ardhini lakini ilijipa moyo ikapenya kwa nguvu kubwa. Kubali kukumbana na magumu maana hayo ndo yatakufanya unekane baada ya kuyavuka! Usikimbie magumu utabaki chini siku zote!

Ikiwa ningeihitaji sana napo ningekuwa sina hekima maana imenishuhudia kwa kunipa zaidi ya matarajio yangu.

Watu wengi wanang'ana na vitu vyao vya zamani wakidhani vitawatoa tu.
Sikiliza ipo namna mpya na mwanzo mpya haijalishi umekuwa mhanga kiasi gani. Uchumi wako, elimu yako na hata utumishi wako umebaki ardhini kwa sababu hutaki kuupoteza umimi. Kila kitu unachokifanya unatanguliza "umimi" acha ni lazima umimi ufe...huo ubinafsi sharti ufe ndipo waweza kuinuka kufikia kilele cha mafanikio.

Kaka na dada mafanikio ya kweli yamejengwa Juu ya Kanuni bora sana za kimbingu k**a ulivyo ukuaji wa mmea.

Amka uanze sasa haujachelewa rafiki yangu.
Mafanikio ya kweli ni kanuni halisi za kimbingu zisizobadilika.
Mungu anaona juhudi zako k**a anavyouangalia mmea unapopambana kufikia kilele cha mafanikio. Anza sasa, mafanikio yako ni ya hakika katika nyanja yoyote!

Ni Rojorojo natural remedies na mtumishi William!

TUREJEE EDENI ( VEGETARIAN LIFE)UtanguliziMaisha ya Edeni ni maisha yaliyosheni matunda, nafaka, mbegu na mbogamboga amb...
20/11/2017

TUREJEE EDENI ( VEGETARIAN LIFE)

Utangulizi

Maisha ya Edeni ni maisha yaliyosheni matunda, nafaka, mbegu na mbogamboga ambazo ndicho chakula alichopewa mwanadamu kwa mara ya kwanza.

Utagundua kwamba Edeni hatuoni ulaji wa wanyama na viumbe wengine wenye pumzi au uhai.

Wanadamu walioishi kwa maisha ya Edeni waliishi mamia ya miaka na hakukuwa na magonjwa bali walikufa katika utimilifu wa miaka yao k**a matokeo ya dhambi. Ni ajabu sana leo watu wanakufa na magonjwa ya mtindo wa maisha.

Ukweli ni kwamba magonjwa hayawezi kuisha mpaka watu waelewe mpango wa Mungu wa maisha katika ulaji na unywaji. Wengi leo wanasema eti magonjwa watayamaliza na kuyatibu kwa dawa, hiyo siyo kweli hata kidogo. Mtatumia hela nyingi kwenye ununuzi wa madawa lakini vifo vitaongezeka kila siku kwa sababu watu wameacha asili ambao ndio mpango wa Mungu kwa mwanadamu.
Nawaombeni mfuatilie makala zangu watu wa Mungu. Njooni muanze maisha ya Edeni hamjachelewa Bwana atawaponya.

OMBI KWA SERIKALI

Tunawaomba serikali na wizara ya afya wasisumbuke kuongeza idadi ya wataalamu wa afya yaani madaktari kwani utafiti unaonesha huko Marekani muuaji namba nne ni madaktari na hospitali ( Institute of medicine reports). Na mbaya zaidi kila mwaka watu 350,000 hufa kwa intervention ya madaktari na isitoshe matumizi ya dawa ni namba 4 kusabisha vifo kwa mjibu wa tafiti. Hatuna budi kutumia bajeti kubwa kuleta mauti nchini bali tutumie fedha hizo kuimarisha kilimo na upatikanaji wa matunda, nafaka nzima na mbogamboga za majani kwa kila mtanzania.
" Watu wangu wanaangamizwa kwa kusosa maarifa"

KWA NINI TUREJEE EDENI?

Mungu Muumbaji aliwapa wazazi wetu wa kwanza chakula chenye kujaa virutubisho tele na akaamuru kiwe ndicho chakula cha jamii ya wanadamu wote.

Hakutaka hata kidogo uhai wa kiumbe utolewe na kumwaga damu ya viumbe wake.Alipanga kusiwe na kuua kabisa kwenye Bustani nzuri ya EDENI.
Matunda ndicho kingekuwa chakula cha mwanadamu maisha yake yote milele na milele.

Bwana amedhamiria nyakati zetu tulizopo kuurejesha mpango wake kwa wanadamu ili waishi kwa kula matunda, mbogamboga za majani, na nafaka nzima...
Amekuwa akiihurumia jamii ya wanadamu kwa kipindi kirefu kwa magonjwa na udhaifu uliosababishwa na ulaji na unywaji wa kufisha.

WITO

Shida na magonjwa mengi ni matokeo ya kuacha mpango wa Mungu wa awali yaani vyakula vya mimea. Haujachelewa wakati ni sasa acha kuharibu hekalu la Mungu kwa ulaji na unywaji unaodhoofisha afya yako ya mwili, akili na roho.

Turejee Edeni ndiko kuna afya na uzima.
Rojorojo natural remedies wanakutakia pumziko jema ...Tel.0686187412.

Rojorojo natural remedies sanitarium, the hidden treasures natural healing centre of the world. Ijue hazina iliyositirik...
20/11/2017

Rojorojo natural remedies sanitarium, the hidden treasures natural healing centre of the world. Ijue hazina iliyositirika katika uponyaji kwa njia ya matunda na mbogamboga za majani pasipo kuacha madhara kwenye mifumo ya mwili. Pata juisi iliyosheheni viini lishe vya tiba.

A young poet from Tanzania"A patient's speech to a physician"Composer: William Clement, 25 December 2016Written by: Will...
20/11/2017

A young poet from Tanzania

"A patient's speech to a physician"

Composer: William Clement, 25 December 2016
Written by: William.

We know what makes us I'll
And when we fall sick we are told
That It's you who will cure us
For more than five years we are told
You learned healing arts, in modern universities
Built at the people's expense
And to get your fantastic knowledge
Spent a fortune
So you must be able to heal and restore life
Are you able to heal?

When we come to you
Our general outlooks are intimidating you
We understand
And you listen all over malnourished body
As to the cause of our malady
One glance at our physical appearance
Tell you more. It is the same cause that wears out
Our physical bodies and our mental capabilities

The pain in our head and muscles come comes
You say, from the inflammation; and this is also the reason
For the diet on the table of our home
So tell us:
Where does the inflammation come from?

Too much junk food and sedentary life with poisonous environment
Make us weak and sick
Your prescription says:
Meloxicam and diclofenac
Put on more balanced diet, moderate alcohol and meat
You might as well tell a pill for appetite
Not to get thin

How much time can you give us for balanced diet?
We see: One meal in your cupboard costs
The fees you earn from
Twenty consultations

You will no doubt say
You are as innocent as Job. The meal on the table of your consulting room
Tells the same story.

Mara nyingi huwa hatuna tabia ya kuangalia viambata vilivyoko kwenye vipodozi, hebu chukua muda upate maarifa kidogo. Ni...
20/11/2017

Mara nyingi huwa hatuna tabia ya kuangalia viambata vilivyoko kwenye vipodozi, hebu chukua muda upate maarifa kidogo. Ni Rojorojo natural remedies international.

Rojorojo natural remedies washirika wa tiba za asili kwa mimea,matunda,nafaka na mbegu pamoja na mbogamboga.
20/11/2017

Rojorojo natural remedies washirika wa tiba za asili kwa mimea,matunda,nafaka na mbegu pamoja na mbogamboga.

Rojorojo natural remedies. We believe in Nature rather than artificialism.
20/11/2017

Rojorojo natural remedies. We believe in Nature rather than artificialism.

08/09/2017

Lifestyle diseases are overthrowing my generation.

Where can I find true remedy?

The Rojorojo natural home remedies and health reforms remains the assured companion for health.

08/09/2017

Rojorojo natural remedies is the key to health reforms. This is a therapeutic diet with Rojorojo. A number of diseases originate from what we eat and drink. You are what you ingest!

Address

Muhimbili University Of Health And Allied Sciences
Kinondoni

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rojorojo Natural Home Remedies posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category