Afyakiganjani / Ushauri wa kitabibu

Afyakiganjani  /  Ushauri wa kitabibu Tunatoa ushauri wa kitaalamu kuhusiana na Afya na magonjwa mbali mbali, Tanzania nzima. Karibu sana.

KICHOCHO: >Ni ugonjwa unaosababishwa na maambukizi ya vijidudu vya schistosoma. Vijidudu hivi vipo vya aina zaidi ya nne...
05/09/2023

KICHOCHO:
>Ni ugonjwa unaosababishwa na maambukizi ya vijidudu vya schistosoma. Vijidudu hivi vipo vya aina zaidi ya nne.
>Aina moja wapo inayoitwa schistosoma Haematobium ndiyo kwa kiasi kikubwa imekuwa ikipatikana katika mazingira ya nchi yetu.
>Aina hii hupatikana zaidi maeneo ya kanda ya ziwa na maeneo ya pwani mwa nchi yetu.
>Vijidudu hivi husambaa kati ya binadamu na konokono(aina ya bullinus) hususani kwenye uwepo wa maji yaliyotwama.
>Mara nyingi watu ambao hufanya shughuli zao katika mazingira ambayo maji yametwama huwa katika hatari ya kupata ugonjwa huu mf: kulima mpunga, kuogelea au Kutumia maji ya yaliyotwama (vidimbwi, bwawa n.k?) n.k hususani kwenye maeneo ambayo vijidudu hivi hupatikana.

AFYA YA AKILI*Ni Hali ya mtu kuwa sawa kihisia, kisaikolojia na kijamii. *Afya ya akili ina mchango mkibwa katika uelewa...
23/10/2022

AFYA YA AKILI

*Ni Hali ya mtu kuwa sawa kihisia, kisaikolojia na kijamii.

*Afya ya akili ina mchango mkibwa katika uelewa wa mtu, mtizamo wake juu ya mambo mbali mbali na lakini pia Tabia anazoonesha mtu.

*Afya ya akili ndio inayobainisha ni namna gani mtu anaweza pambana na matatizo au changamoto mbalimbali anazokutana nazo kwenye maisha, uwezo wake wa kuhusiana na watu na uwezo wake wa kufanya maamuzi juu ya maswala mbalimbali.

*Afya ya akili inahusisha uwezo wa mtu kufurahia maisha na kuweka usawa Kati ya matukio yanayotokea katika maisha na uwezo wake wa kuwa katika hali ya kawaida ya kisaikolojia pindi anapopitia changamoto.

*Afya ya akili humfanya mtu kuwa mzalishaji na kuweza kuwa na mchango chanya kwa jamii.

****Note: Afya ya akili ni muhimu Sana kwa ajili ya ustawi wa jamii.








CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI #2. KUJIONA MKOSAJI/KUJILAUMU, KUJIHISI HUNA THAMANI NA KUPOTEZA MATUMAINI✓Watu Hawa hujilau...
22/10/2022

CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

#2. KUJIONA MKOSAJI/KUJILAUMU, KUJIHISI HUNA THAMANI NA KUPOTEZA MATUMAINI

✓Watu Hawa hujilaumu muda mwingi kwa mambo ambayo yanatokea/yametokea kwenye maisha yao hata k**a kiuhalisia ni Jambo la kawaida ambalo linaweza mtokea mtu yeyote tu.
✓Huwa hawatafuti suluhisho la mambo wanayopitia, wao hutafakari juu ya changamoto wanazopitia na kuendelea kujilaumu tu, huwa fahamu zao hazitafakari juu ya kupata ufumbuzi..
✓Pia wakati mwingine hujihisi kuwa hawana thamani katika hamii na dunia hii wakijilinganisha na wengine, hujidharau, hujihisi hawana maana Kabisa kwasababu ambazo kiuhalisia hazipo au ni mambo ya kawaida tu kwenye maisha.
✓Hujihisi kuwa ni watu wasio na msaada Kabisa katika jamii
✓Hali hii hupelekea watu Hawa kupoteza matumaini kwakuwa fikra zao hazioni utatuzi wa mambo wanayopitia.
✓Wanakuwa ni watu wa kukata tamaa, wasioona mbele, wasioona mlango wa kutokea kwa chochote kile kinachowasibu.

****USHAURI: Tafuta msaada kisaikolojia pindi unapokutana na changamoto hihiI.

Freemarket Tanzania
Mifugo Tz
Kilimo Tz
Amani AK

CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI #1. MAWAZO HASI✓Hii ni dalili moja wapo inayowatokea baadhi ya watu wenye changamoto ya akil...
22/10/2022

CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI

#1. MAWAZO HASI

✓Hii ni dalili moja wapo inayowatokea baadhi ya watu wenye changamoto ya akili.
✓Watu Hawa huwa hawafurahii kabisa maisha,Mara nyingi huisi kila mambo wanalofanyiwa/kuambiwa kuwa ni mabaya.
✓Mara nyingi huisi watu wanalenga kuwatendea wao ubaya muda wote ingawa kiuhalisia hamna baya lolote ambalo wanatendewa.
✓Hii ni shida kubwa kwa kuwa muda wote watakuwa wanaona kuwa watu ni wabaya na hivyo kupelekea hata kushindwa Kabisa kuishi vizuri na jamii.
✓Hufikia hatua ya kujitenga na pia kujihami kwa kugombana na watu ambao wao wanahisi wanawatendea ubaya.
✓Kutokana na hali hiyo, watu hawa huwa katika hatari kubwa ya kukosa msaada pindi wapatapo matatizo, kwakuwa mara nyingi hutofautiana Sana na ndugu na jamaa wa karibu na hata kufikia hatua ya kutengwa.

***USHAURI: Ikiwa una dalili hii au una ndugu/rafiki mwenye dalili hii, hakikisha unapata/anapatiwa msaada wa kisaikolojia mapema.

Mifugo Tz
Kilimo Tz
FrFreemarketTanzania
Freemarket Tanzania
Amani AK

TAFITI: Inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050, asilimia 50(50%) ya watu duniani, watakuwa na matatizo ya macho yanayo wala...
17/10/2021

TAFITI:
Inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2050, asilimia 50(50%) ya watu duniani, watakuwa na matatizo ya macho yanayo walazimu kutumia miwani. Tatizo hili litakuwa kubwa zadi katika nchi zilizoendelea, na hii Ni kutokana na ongezeko la matumizi ya vifaa vya kidigitali K**a simu, tablet, computer n.k.

USHAURI: Jicho ni taa ya mwili. Linda macho yako dhidi ya vitu vinavyo weza leta athari kwenye macho yako.

Kwa elimu zaidi, endelea kufuatilia kurasa Mara kwa Mara.







TUNZA MACHO YAKO, TUNZA MACHO YA MTOTO WAKO.Matumizi ya vifaa vya kidigitali K**a simu na iPads kwa kipindi kirefu na kw...
13/10/2021

TUNZA MACHO YAKO, TUNZA MACHO YA MTOTO WAKO.

Matumizi ya vifaa vya kidigitali K**a simu na iPads kwa kipindi kirefu na kwa muda mrefu huweza athiri macho na kupelekea kushindwa kuona vizuri na pia husababisha adha zifuatazo kuuma, kuwasha na kuchoka kwa macho, maumivu ya kichwa, shingo na mwili kuchoka.

USHAURI:
1. Tusipende kuwazoesha watoto wetu matumizi ya vifaa hivi, Ni hatari kwa afya macho yao.
2. Tutumie vifaa hivi pale inapobidi tu, na si kukaa ukiangalia simu na kwa muda mrefu k**a hakuna sababu ya kufanya hivyo.
3. Tukumbuke kuweka sawa mwanga wa vifaa hivi kulingana na mazingira unapokitumia vifaa hivi, hakikisha mwanga si mkali saaana wala si hafifu sana, haitakiwi macho yapate tabu katika kuangalia pindi unapotumia vifaa hivi.





UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUMENi tatizo linaloongezeka kwa kasi Sana miongoni mwa vijana. Tatizo hili hutokana na sababu mba...
10/10/2021

UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Ni tatizo linaloongezeka kwa kasi Sana miongoni mwa vijana. Tatizo hili hutokana na sababu mbali mbali zinazo athiri afya ya mwili na akili.

EPUKA matumizi holela ya dawa za kuongeza nguvu za kiume. Fika kwa wataalam wa afya kwa ajili ya Ushauri, vipimo na matibabu.






.

KANSA YA TEZI DUME.Kansa ya tezi dume, huwa na tabia ya kusambaa kuelekea kwenye mifupa, hususani mifupa ya uti wa mgong...
07/10/2021

KANSA YA TEZI DUME.

Kansa ya tezi dume, huwa na tabia ya kusambaa kuelekea kwenye mifupa, hususani mifupa ya uti wa mgongo; Hali hii huweza kupelekea mtu kupata ganzi katika miguu na huendelea mpaka kusbabisha miguu kulemaa na kushindwa kutembea Kabisa.

USHAURI: Ni muhimu kufanyiwa uchunguzi wa tatizo hili walau Mara moja kwa mwaka kwa wazee ambao wamefika umri wa miaka 50.




  wa SAUNA(KUJIFUKIZA) Mara kwa Mara,   wa laptop ukiwa umeipakata pamoja na   nguo za ndani zenye kubana kwa muda mrefu...
05/10/2021

wa SAUNA(KUJIFUKIZA) Mara kwa Mara, wa laptop ukiwa umeipakata pamoja na nguo za ndani zenye kubana kwa muda mrefu, husababisha joto la kwenye korodani kuongezeka Sana na kupelekea kupungua kwa uzalishaji wa mbegu za kiume.

Kupungua huku kwa uzalishaji wa mbegu hizi huwa Ni kwa muda mfupi na mtu hurudi kwenye hali take ya kawaida pindi atakapoachana na tabia tajwa hapo juu.




VARICOCELEKuvimba kwa mishipa ya damu kwenye korodani, Ni miongoni mwa sababu zinazopelekea kupungua kwa uzalishaji wa m...
04/10/2021

VARICOCELE

Kuvimba kwa mishipa ya damu kwenye korodani, Ni miongoni mwa sababu zinazopelekea kupungua kwa uzalishaji wa mbegu za kiume na hivyo kupelekea mtu kushindwa kupata mtoto.

Tatizo hili linatibika, Fika kwa wataalam wa afya walio karibu nawe, kwa ajili ya vipimo, ushauri na tiba.




TAFITI: Tafiti zinaonesha kuwa karibu asilimia 40 mpaka 50 (40%-50%) ya matatizo ya kukosa watoto hutokana na matatizo y...
04/10/2021

TAFITI: Tafiti zinaonesha kuwa karibu asilimia 40 mpaka 50 (40%-50%) ya matatizo ya kukosa watoto hutokana na matatizo ya kwenye via vya uzazi vya wanaume.

USHAURI: Ni muhimu wote wawili (mke na mume), kufika kwa pamoja kwa wataalam wa afya kwa ajili ya vipimo, tiba na ushauri juu ya masuala haya ya uzazi.




TATIZO LA KUJIKOJOLEA- Hii ni hali inayoweza kumpata mtu mzima au mtoto akiwa amelala au akiwa macho, ambapo anakuta mko...
02/10/2021

TATIZO LA KUJIKOJOLEA

- Hii ni hali inayoweza kumpata mtu mzima au mtoto akiwa amelala au akiwa macho, ambapo anakuta mkojo unatoka wenyewe bila ridhaa yake. Hali hii huweza tokea wakati wowote wa maisha ya mtu, si lazima liwe ni tatizo la kuzaliwa nalo.

- Tatizo hili Mara nyingi linayempata huwa hajakusudia kufanya hivyo na humpata kutokana na sababu mbali mbali za kiafya.

- Kwa yeyote mwenye tatizo hili au mwenye mtoto mwenye tatizo hili, Afike kwa wataalam wa Afya walio karibu nae kwa ajili ya Ushauri na matibabu juu ya tatizo hili. EPUKA KUWASEMA VIBAYA au KUWA ADHIBU WATOTO/WATU WAZIMA WENYE TATIZO HILO, HALI HIYO HUWEZA KUWAPELEKEA KUPATA MATATIZO YA KISAIKOLOJIA.

Kwa ushauri zaidi, wasiliana nasi kupitia 0744122169.




Address

Tegeta
Kinondoni

Telephone

+255744122169

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Afyakiganjani / Ushauri wa kitabibu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Afyakiganjani / Ushauri wa kitabibu:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category