Mbeya Referral Hospital

Mbeya Referral Hospital welcome to Mbeya regional referral hospital official Page

Pumzika kwa amani Mhe. Edward Ngoyai Lowassa , Waziri mkuu mstaafu.
12/02/2024

Pumzika kwa amani Mhe. Edward Ngoyai Lowassa , Waziri mkuu mstaafu.

19/08/2023

Madaktari Bingwa wa Macho kutoka Ujerumani kuweka kambi Hospitali ya rufaa ya mkoa Mbeya.

23/07/2023

Ni tarehe 22 mwezi wa nane 2023, wananchi tujitokeze kwa wingi.

Wizara ya Afya imeendelea kuwa kuwa kinara wa matumizi ya kidigitali ya mitandao ya kijamii katika utoaji wa habari mita...
15/07/2023

Wizara ya Afya imeendelea kuwa kuwa kinara wa matumizi ya kidigitali ya mitandao ya kijamii katika utoaji wa habari mitandaoni na kwenye vyombo mbalimbali vya habari pamoja na kutumia nyenzo za kidigitali kurahisisha utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Wizara imeibuka mshindi wa Tuzo za Kidigitali kwa Mwaka 2022 katika Kipengele cha Wizara iliyoongoza katika mawasiliano Kidigitali.

Taasisi ya Serengeti Bytes kwa mara nyingine tena wameanda tuzo hizi ambazo hushirikisha Taasisi na Watu wenye ushawishi kwenye jamii waliofanya vyema kwenye matumizi bora ya kidigitali.

Tuzo hizi zimetolewa leo Tarehe 15 Julai, 2023 Jijini Dar Es Salaam na kupokelewa na Mwakilishi sa Katiku Mkuu Dkt. Omary Ubuguyu Mkurugenzi Msaidizi Programu ya Kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza pamoja Bw. Englibert Kayombo Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalino, Wizara ya Afya.

Shukrani ziwaendee Viongozi wetu wakiongozwa na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwa uongozi hodari na kuzingatia umuhimu wa nyezo za kidigitali kuweza kufikisha habari na mawasiliano kwa umma, kutumia nyezo za kidigitali kuweza kurahisisha utoaji wa huduma za afya, Taasisi zote zilizo chini ya Wizara ya Afya, Mabaraza na Hospitali za Rufaa za Mikoa, Waandishi wa habari na wananchi wote kwa kuendelea kufuatilia taarifa mbalimbali za Wizara kwenye mitandao yetu.

TAARIFA KWA UMMA
27/06/2023

TAARIFA KWA UMMA

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa kishindo!
16/05/2023

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Afya kwa kishindo!

"KAIMU MGANGA MFAWIDHI Dkt. NGWILO MWAKYUSA AMBAYE ALIMUWAKILISHA MGANGA MFAWIDHI Dkt. ABDALLAH MMBAGA K**A MGENI RASMI ...
14/05/2023

"KAIMU MGANGA MFAWIDHI Dkt. NGWILO MWAKYUSA AMBAYE ALIMUWAKILISHA MGANGA MFAWIDHI Dkt. ABDALLAH MMBAGA K**A MGENI RASMI KILELE CHA MAADHIMISHO YA WAUGUZI DUNIANI" ALIKUWA NA HAYA YA KUSEMA:

Kaimu Mganga Mfawidhi alisema " Leo hii, tumekusanyika hapa kuadhimisha siku ya Wauguzi Duniani na kutumia fursa hii kuwashukru Wauguzi kwa moyo wangu wote kwa kazi yenu yabkujitolea na huduma bora mnayotoa kwa jamii yetu. K**a Kaimu Mganga Mfawidhi kwa niaba ya Mganga Mfawidhi na timu nzima ya menejimenti, ninapenda kuelezea shukrani zangu za dhati kwa kila mmoja wenu.

Aidha, ijulikane kuwa Wauguzi ni moyo wa Mfumo wa Afya. Mna jukumu muhimu katika kutoa Huduma bora za afya kwa wagonjwa wetu na kuleta farqja na matumaini kwa familia zao. Kazi yenu inahitaji ujuzi mkubwa, uvumilivu, na upendo. Mnafanya kazi masaa mengi, mkiwapokea wagonjwa kwa tabasamu, kuwasikiliza, na kuwahudumia kwa upendo na heshima.

Nimeona juhudi zenu zisizochoka na weledi katika kipindi chote, ambacho kimetuweka katika changamoto ya uhaba wa wauguzi ambayo ni changamoto ya Kitaifa. Mlikabiliana na hali ngumu, mkafanya kazi kwa juhudi kubwa, na mkaweka maisha yenu hatarini ili kulinda afya za wenanchi. Hakika, nyote ni Mashujaa na tunawapongeza kwa moyo Mkunjufu.

Pia, tunatambua changamoto zinazowakabili za kila siku. Mnapambana na uchovu wa kazi, ukosefu wa rasilimali na mengi zaidi. Lakini bado mnaendelea kuwahudumia wagonjwa na kujitoa kikamilifu. Hili ni jambo la kuvutia na linaonyesha dhamira yenu ya kweli na upendo kwa kazi yenu.

Leo, nataka kusisitiza umuhimu wa kutambua mchango wenu katika mfumo wa Afya. Tunapaswa kuwekeza katika kuimarisha mazingira yenu ya kazi, kuwezesha mafunzo yenu, na kuwasidia katika kukabiliana na changamoto zinazojitokeza. Wauguzi ni rasilimali muhimu sana, na tunahitaji kuwathqmini na kuwasaidia katika kazi zenu.

Nawashukru pia familia zenu na wapendwa wenu kwa kuwapa nguvu na kuwasaidia katika safari yenu ya kuwa wauguzi. Tunaona Mchango wao na tunawashukru kwa kusaidia wauguzi wetu katika kuwahudumia wqgonjwa na jamii yetu.

Kwa hitimisho, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kila mmoja wenu. Mwenyezi Mungu awabariki Wauguzi wote."

Eid El fitr
21/04/2023

Eid El fitr

Ahsante kwa Feedback
19/04/2023

Ahsante kwa Feedback

Address

Forest Mpya
Mbeya
MBEYAREGIONALREFERRALHOSPITAL

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbeya Referral Hospital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Mbeya Referral Hospital:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category