Ushauri wa Ndoa

Ushauri wa Ndoa Let them be them Ndoa zimakuwa changamoto sana Katika Kizazi cha Sasa, ni Muhimu kushirikian udhoefu ili kujenga misingi mizuri ya jamii yetu

JE Nimsamehe mke wangu Baada ya Usaliti?Huu ni ushuhuda binafsi, labda pia ni sababu ya Mimi kuwa na hii page, Nilioa mi...
24/08/2025

JE Nimsamehe mke wangu Baada ya Usaliti?

Huu ni ushuhuda binafsi, labda pia ni sababu ya Mimi kuwa na hii page, Nilioa miaka 20 iliyopita, kwa ndao nzuri tu ya Kanisani, Baba na Mama yangu walikuwa watumishi wa Mungu, wafanya kazi wa Serikali. Mimi nilikuwa nimemaliza chuo, na nilikuwa na Uchumba wa miaka mi 2 wa chuo, nilipomaliza nikamsaidia Mchumba wangu mambo madogo madogo naye ak**aliza.

Tulifunga ndoa za furaha na baada ya mwaka tulipata Mtoto wa Kwanza, miaka mi 5 baada ya ndoa nilik**ata mawasiliano ya mke wangu na X wake, ambaye ni wa kutoka high school ( Keshaoa ), Haikuwa na ushahidi sana, kwamba alilala naye, nikamsamehe.

Miaka 10 baadaye, nilimshika tena na yule mwanaume na wengine wawili tena ( Ma X ) Jumla wa watatu, sikusema kitu, ila nilidhamiria kumuacha, maana ilikuwa k**a surprise, nilikaa kwa maumivu mwaka mmoja tena kujiandaaa kuondoka kwa amani!

Ninachotaka kusema ni nini ?

1. Ukithibitisha mke kakusaliti hasa na X wake, ndugu yangu mwanaume, ondoka, usikae kabisa, maana kuna mambo mawili, la kwanza umempa ujasiri kwamba una samehe, la pili ; Anakuwa mjanja zaidi.

2. Ukikaa, unajipunguzia mda wako wa kutoka mapema na kuanza upya, Mimi ningeondoka miaka mitano tu nikiwa kwenye ndoa na watoto wawili, lakini nilikuwa kuondoka nikiwa na miaka 48 na watoto wa tatu ( Hasara zaidi )

3. Mwanmke akishaanza kukusaliti, anapokea order na maelekezo kutoka kwa mwanaume anayeshiriki naye, wewe unabaki kuwa mtoaji tu, ila Heshima, na hisia zote ni kwa mtu asiya na msaada wowot ?

Ndugu yangu, mwanaume mwenzangu, ingawa sio rahisi kuondoka, ila jipe mda, kwa amani kabisa, Jipange upya na uondoke, huna haja ya kufia humo ndani kwa maumivu, na hasira na kudhuru mtoto wa watu!

Wakati mwingine ni vyema tu kumruhusu mtu aondoke maishani mwako k**a hataki kukuelewa, Kutokuwepo kwake kutakufundisha ...
25/07/2025

Wakati mwingine ni vyema tu kumruhusu mtu aondoke maishani mwako k**a hataki kukuelewa, Kutokuwepo kwake kutakufundisha vitu ambavyo Huwezi jifunza akiwepo.

Acha kujiumiza kwa kulazimisha Mahusiano au ndoa ambayo wewe ni Shahidi siyo sahihi kwako, Huwezi kufanya mtu akujali, awe mwaminifu au kuwabadilisha unavyotaka.

Wakati mwingine mtu unayelazimisha kuwa naye ndo hukupaswa kabisa, wakati mwingine watu huja kwa sababu tu nakupita, waache waende.

Kuwa makini usipoteze utu na nafsi yako kurekebisha jambo ambalo kamwe hutaliweza. Huwezi pata Upendo / mapenzi toka kwa mtu ambaye hayupo tayari kukuthamini.

Ni ngumu sana ukiwa unafikiri mtu uliye naye " Ni sahihi" halafu anakuwa ndo anakuuza kabisa, Utapona tu na kupata mtu mwingine.

Kumbuka ni Bora kuwa "single" - Kuishi mwenyewe kuliko kupoteza utu wako, K**a mtu anakufanya k**a wewe mbadala, kamwe usimfanye kipaumbele chako.

, , ,

Jifunze kufunga MdomoUnanunua Nyumba? Funga Mdomo.Unanunua gari jipya? Funga MdomoUnanunua gari jipya? Funga Mdomo.Unaen...
23/06/2025

Jifunze kufunga Mdomo

Unanunua Nyumba? Funga Mdomo.

Unanunua gari jipya? Funga Mdomo

Unanunua gari jipya? Funga Mdomo.

Unaenda Kuoa ? Funga mdomo

Umepandishwa cheo ? Funga Mdomo.

99.9% ya mambo yote / ndoto na mipango haitimii k**a tunavyopanga, Kwa sababu tunafungua midomo yetu mapema kwa watu wasio sahihi na Kwa wakati usio sahihi.

Tulikosea kuwashirikisha watu mafanikio / miradi yetu kwa watu wanaojiita "Marafiki" Haya yamesababisha wivu na mazingira ya mambo yetu kutotimia Kwa wakati, kwa hiyo jifunze kufunga Mdomo.

Marafiki zako wengi wanaweza kutaka ufanye vizuri na ufanikiwe lakini sio uwazidi ki mafanikio.

Na pia uelewe, hata ndugu zako wa Damu wanalo jicho la wivu ambalo limejificha na gumu kuliona.

Lakini hawawezi zuia mipango ya Mungu kwako.

Kuwa na Hekima, Kumbuka k**a samaki angefunga Mdomo, ndoano ya mvivu ingekosa pa kushika!

Anza Leo kutengeneza tabia ya kufunga Mdomo!

30/01/2025
Eti ndugu zangu wanandoa!!!"Kwanini umsaliti mtu unayetaka kuishi naye na wala hutaki mpoteza na mtu ambaye hutaki na hu...
28/07/2024

Eti ndugu zangu wanandoa!!!

"Kwanini umsaliti mtu unayetaka kuishi naye na wala hutaki mpoteza na mtu ambaye hutaki na huna mpango wa kuishi naye"

Tujali familia zetu, We Baba kumbuka ulichagua Mama wa watoto wako, k**a hukuchagua vizuri sio kosa la watoto wako, huna haja ya kuwatesa!!!!!

Hapa naweza kusema nidhamu au discipline hujengwa ndani ya mtu na adhabu au punishment ni vitu vya nje(mf. Fimbo). Ni vy...
20/06/2022

Hapa naweza kusema nidhamu au discipline hujengwa ndani ya mtu na adhabu au punishment ni vitu vya nje(mf. Fimbo). Ni vyema tukawafundisha watoto nidhamu kwa Lengo la mtoto kuweza kutatua changamoto atakazo au anazo kabiliana nazo. Adhabu itampa maumivu kwa kosa au changamoto aliyokutana nayo na anaweza asijifunze. Maamuzi ya miongozo hii imo mikononi mwetu sisi wazazi, tuchague kilicho na advantage zaidi kwetu sisi (wazazi/walezi) na watoto wetu.

Address

Tabata Shule
Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ushauri wa Ndoa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram