AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Elimu na Ushauri kuhusu Afya 👏🙏😷⛑️ karibu kwa ushauri wa afya

Kunyonyesha ni njia ya asili ya uzazi wa mpango huitwa Lactational Amenorrhea Method (LAM). Ni njia salama na yenye ufan...
16/12/2025

Kunyonyesha ni njia ya asili ya uzazi wa mpango huitwa Lactational Amenorrhea Method (LAM). Ni njia salama na yenye ufanisi endapo vigezo maalum vitazingatiwa kikamilifu.

LAM ni njia ya kuzuia mimba inayotegemea kunyonyesha mara kwa mara na kwa ukamilifu, jambo linalozuia utolewaji wa yai (ovulation) kwa mama baada ya kujifungua.

Vigezo 3 muhimu vya LAM lazima vinazingatiwe, K**a ifuatavyo ;

1️⃣ Mtoto ana chini ya miezi 6

Baada ya miezi 6, mtoto huanza vyakula vya nyongeza hivyo ufanisi wa LAM hupungua.

2️⃣ Mama hajaanza kupata hedhi tangu ajifungue

Kutoka damu baada ya kujifungua (lochia) haichukuliwi k**a hedhi. Damu ya baada ya kujifungua kawaida hukoma kati ya week 6 hadi 8

Hedhi ikianza tuu mhimu mama akaanza kutumia njia zingine za uzazi wa mpango ambazo zitamkinga dhidi ya mimba zisizo tajarajiwa

3️⃣ Kunyonyesha kikamilifu (Exclusive or near-exclusive breastfeeding)

Hii ina maana:

Mtoto ananyonya mara nyingi mchana na usiku

Hakunywi maji, uji, maziwa mbadala au vyakula vingine

Hakai muda mrefu bila kunyonya (zaidi ya saa 4 mchana au saa 6 usiku)

Ufanisi wa LAM hufikia 98% ikiwa vigezo vyote vitazingatiwa kikamilifu

Ni sawa na baadhi ya njia za kisasa za uzazi wa mpango kwa miezi 6 ya mwanzo

Faida za LAM

✅Haina gharama

✅Haina homoni wala madhara

✅Hukuza afya ya mtoto (kinga, lishe bora)

✅Husaidia mama kupona haraka baada ya kujifungua

✅Hupunguza hatari ya kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua

Mapungufu ya LAM

▪️Ni ya muda mfupi (miezi 6 tu)

▪️Haikingi dhidi ya magonjwa ya zinaa (STIs)

▪️Ufanisi hupungua haraka ikiwa mtoto hatonyonyeshwa mara kwa mara

▪️Inahitaji ufuatiliaji wa karibu wa hali ya mama na mtoto

Baada ya miezi 6 au kigezo kuvunjik Mama anashauriwa kuanza njia nyingine ya uzazi wa mpango (k**a kondomu, vidonge vinavyofaa kwa wanaonyonyesha, sindano, kitanzi n.k.)

Kunyonyesha ni njia nzuri ya asili ya uzazi wa mpango kwa muda mfupi, lakini inahitaji nidhamu na uelewa mzuri wa vigezo. Elimu kwa mama ni muhimu ili kuepuka mimba zisizotarajiwa.

Vipi wewe hedhi ili rudi baada ya mda gani...!?

Baada ya kujifungua watu huzingatia mtoto tu lakini mwili wako mama pia  unahitaji uangalizi wa karibu hali kadharika zi...
15/12/2025

Baada ya kujifungua watu huzingatia mtoto tu lakini mwili wako mama pia unahitaji uangalizi wa karibu hali kadharika zitatokea yote ni mwendelezo wa kupona baada ya kujifungua, kila mama ana hatua zake za uponaji wengine huwahi na wengine huchelewa hivyo kusubiri upone kulingana na uponaji wa mwili siyo udhaifu bali tofauti ya uponaji wa kila mtu kulingana na umri, ulaji, mazoezi na mambo yaliyotokea baada ya kujifungua k**a vile kuchanika, kushonwa nk. Haya ni baadhi ya mabadiliko ambayo mama anaweza pitia baada ya kujifungua ;

▪️ TUMBO LAKO KUONEKANA LINA Ujauzito BADO

Tumbo la uzazi linahitaji wiki kadhaa ili lisinyae.
Hii ni kawaida, kitalaam hali ya kizazi kurudi katika hali yake ya kawaida baada ya kujifungua kitalaam wanaita Uterine Involution, ndo maana hakunaga umhimu wa kufunga tumbo baada ya kujifungua kwa kuwa hurudi lenyewe katika hali yake ya kawaida ndani ya week 6-8.

▪️KUTOKWA NA DAMU KUNAWEZA KUDUMU WIKI

Damu inayotoka mara baada ya mama kujifungua kitalaam Lochia, ambayo inaweza kuendelea kutoka kwa wiki 6-8 .
Rangi na kiasi vitabadilika polepole kadri ya uponaji unavyoendelea .
Kutokwa na damu nyingi ghafla SI kawaida hapo utahitaji uangalizi wa dharura .

▪️UNAWEZA KUJISIKIA HISIA KALI BILA SABABU ZISIZO WAZI.

Homoni hupungua sana baada ya kujifungua.
Machozi, hofu, hasira, huzuni, yote yanaweza kutokea.
Wewe si dhaifu.
Unazoea.

▪️MATITI YAKO YATAJAA NA MDA MWINGINE HADI MAUMIVU

Maziwa yanayoingia yanaweza kusababisha UVIMBE ikiwa mama utakuwa hanyonyeshi , kupanda kwa joto, na maumivu kutokana na mtoto kutonyonya .
Kunyonyesha mara kwa mara husaidia kupunguza maumivu.

▪️UNAWEZA KUHISI MAUMIVU WAKATI WA KUKOJOA AU WAKATI WA KUJISAIDIA HAJA KUBWA

Kushonwa, kuchanika na shinikizo wakati wa mimba au wakati wa kupush au kujifungua vinahitaji muda wa kupona.

▪️ USINGIZI WAKO UTABADILIKA KABISA

Sio tu kwa sababu ya mtoto
bali kwa sababu mwili wako bado unapona.

▪️HARUFU YA MWILI WAKO INAWEZA KUBADILIKA

Homoni baada ya kujifungua huathiri tezi za jasho.
Inaboreka kadri muda unavyopita.

▪️MWILI WAKO UNAHITAJI KUPUMZIKA SI HUKUMU

Uponyaji si ushindani.
Kila mama hupona tofauti na mwingine hivyo basi tunafanana lakini hatulingani .

Kipi kilikupa shida kuzoea au baada ya kujifungua..!?

Ni page gani imegusa maisha yako sana kwa mwaka huu 2025. Hebu itag hapa na useme neno juu ya huyo mwenye page❣️Credit
14/12/2025

Ni page gani imegusa maisha yako sana kwa mwaka huu 2025. Hebu itag hapa na useme neno juu ya huyo mwenye page❣️

Credit

Baada ya kutoka katika marosoroso ya mimba sasa ni wakati mwingine wenye marosoroso mengine ya uchanga lakini ndani saa ...
14/12/2025

Baada ya kutoka katika marosoroso ya mimba sasa ni wakati mwingine wenye marosoroso mengine ya uchanga lakini ndani saa 24 za mwanzo ndiyo mwanzo na mwendelezo mzuri wa kujua kipi cha kufanya yote kwa ajili ya ulinzi wa mama na mtoto, Haya ni baadhi ya mambo ya Kuzingatia ndani ya saa 24 baada ya mama kujifungua.

▪️ WATEMBELEAJI WENGI SANA WANAWEZA KUWA CHANZO CHA MTOTO MCHANGA KUUGUA .

Kinga ya mtoto mchanga ni dhaifu sana.

Kila mkono, kila pumzi, kila busu hubeba vijidudu.
Mapenzi ni mazuri lakini umbali ni ulinzi.

▪️NGOZI KWA NGOZI NI DAWA

Kumweka mtoto kifuani mwa mama mara tu baada ya kuzaliwa:
✅ Husaidia mtoto kupumua vizuri
✅ Hudhibiti halijoto
✅ Huimarisha uhusiano
✅ Huongeza mafanikio ya kunyonyesha

▪️ KUCHELEWA KUNYONYESHA KUNAWEZA KUATHIRI UTOAJI WA MAZIWA

Maziwa hayo mazito ya njano (colostrum) ni chanjo ya kwanza ya mtoto.
Mtoto anaponyonya mapema, ndivyo mtiririko wa maziwa unavyokuwa mzuri zaidi. Hivyo jitahidi kunyonyesha mtoto ndani ya nusu saa toka ukijifungua ikizidi sana ndani ya saa moja toka ujifungue.

▪️ KUMWOSHA MTOTO MCHANGA MAPEMA NI HATARI.

Kuoga mapema huondoa mafuta ya kinga na husababisha upotevu wa joto.
Mtoto mchanga anapaswa kusubiri angalau saa 24 kabla ya kuoga kwanza.

▪️UKIMYA NI TIBA

Kelele kubwa humtia wasiwasi mtoto mchanga.
Mazingira tulivu na tulivu huwasaidia kuzoea maisha ya nje.

▪️ANGALIA ISHARA ZA ONYO KWA MTOTO KWAMBA HALI HAIKO SAWIA.

✅Kushindwa kunyonya
✅Kupumua haraka
✅Macho ya njano au ngozi kwa ujumla
✅Kilio dhaifu
✅Mwili kupoa au kuwa baridi sana
Hizi si "tabia ya kawaida ya mtoto mchanga."
Wanahitaji uangalizi wa haraka.

▪️MAMA PIA ANAHITAJI UANGALIZI KWAKUWA PIA HUPATWA NA DALILI HATARI K**A VILE

✅Kutokwa na damu
✅Maumivu makali ya KICHWA, Kuona maruweruwe
✅Kizunguzungu
✅Maumivu ya matiti au kuvimba kwa mtiti yote au moja
✅Kuvunjika kwa kihisia, msongo wa mawazo, wasiwasi kiasi cha kuona hana thamani teena, kutaka kujitoa uhai nk.
Kupuuza afya ya mama ni hatari.

Jambo gani wakati wa uchanga lilikutatiza sana...!?

Hii  ni aina ya hofu kali (anxiety disorder) ambapo mtu huogopa sana kuwa katika maeneo yaliyofungwa au yenye nafasi ndo...
13/12/2025

Hii ni aina ya hofu kali (anxiety disorder) ambapo mtu huogopa sana kuwa katika maeneo yaliyofungwa au yenye nafasi ndogo, hata k**a hakuna hatari ya kweli.

Maeneo yanayoweza kuchochea claustrophobia

▪️Lifti

▪️Vyoo vidogo au vilivyofungwa

▪️Chumba kisicho na madirisha

▪️Gari lililofungwa kwa muda mrefu

▪️Mashine za hospitali k**a MRI/CT scan

Dalili za claustrophobia ambazo hutokea mtu anapokuwa au anapofikiria kuingia sehemu iliyofungwa:

▪️Kupumua kwa shida au haraka

▪️Mapigo ya moyo kwenda kasi

▪️Kutokwa na jasho

▪️Kizunguzungu au kuhisi kuzimia

▪️Maumivu ya kifua

▪️Hofu kali ya kupoteza udhibiti au kufa

▪️Hamu kubwa ya kukimbia au kutoka haraka

Sababu zinazoweza kuchangia

✅Tukio baya la zamani (mf. kufungiwa ndani ya chumba, ajali)

✅Kurithi hofu (familia kuwa na anxiety disorders)

✅Mabadiliko kwenye kemikali za ubongo (neurotransmitters)

✅Kujifunza hofu kutoka kwa watu wengine

Matibabu ya Claustrophobia inatibika kwa njia kuu ambazo ni:

▪️ Cognitive Behavioral Therapy (CBT) – humsaidia mtu kubadilisha fikra za hofu

▪️Exposure therapy – kumzoesha mtu taratibu kwenye maeneo aliyoyaogopa

▪️ Dawa (kwa baadhi ya watu):

Dawa za kupunguza wasiwasi

Wewe hali hii huwa inakutokea ukiwa kwenye nini...!?

❤️🙏
12/12/2025

❤️🙏

Nawatakia usiku mwema...... 🙏❤️
10/12/2025

Nawatakia usiku mwema...... 🙏❤️

Hii ni hali ambapo mama anajifungua haraka sana na kitalaam hali wanaita Precipitate labor , yaani hatua zote za uchungu...
09/12/2025

Hii ni hali ambapo mama anajifungua haraka sana na kitalaam hali wanaita Precipitate labor , yaani hatua zote za uchungu zinatokea kwa muda mfupi kuliko kawaida na uchungu huu unadumu chini ya saa 3.

Baadhi ya sababu za kutokea kwa precipitate labor

▪️Msisimko mkubwa wa uterus
Uterus inajikaza kwa nguvu na kwa haraka sana kuliko kawaida.

▪️Historia ya kujifungua haraka
Ikiwa mama aliwahi kujifungua haraka awali.

▪️Multiparity
Wanawake waliowahi kujifungua mara nyingi wanaweza kupata uchungu unaoendelea haraka.

▪️ Uterine stimulants
Matumizi ya dawa za kuanzisha uchungu kwa kiasi kikubwa yanaweza kuongeza kasi kupita kawaida.

Madhara yanayoweza kutokea ikitoea precipitate labor.

Kwa mama:

©️Kupasuka kwa uke au mlango wa uzazi (perineal tears).

©️Kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua (PPH) kutokana na uterine atony.

©️Mshtuko (shock) kutokana na maumivu makali na mabadiliko ya ghafla.

©️Maambukizi ikiwa kujifungua kunatokea bila usafi au bila msaada wa kitaalamu.

Kwa mtoto:

©️Kuumia wakati wa kutoka haraka (birth trauma).

©️Kuvuta uchafu au maji machafu (aspiration).

©️Hypoxia—mtoto kukosa hewa kutokana na kukosa uangalizi wa karibu.

©️Kupumua vibaya (respiratory distress).

🩺 Dalili na ishara za precipitate labor

▪️Maumivu makali yanayoanza ghafla na contraction zinakuja mfululizo bila kupumzika.

▪️Cervix kufunguka kwa kasi sana.

▪️Mama kuhisi "pressure" ya mtoto kushuka haraka.

▪️Mtoto kusukumwa nje ndani ya muda mfupi.

Usimamizi (Management)

✅Kumpa mama msaada wa haraka wa wahudumu wa afya.

✅Kudhibiti contraction ikiwa dawa ndiyo imeongeza kasi (kupunguza/ kusimamisha ).

✅Kumpa mama oxygen na kumuweka katika mazingira salama ili asianguke.

✅Kuepuka kupasuka kwa tishu au misuli ya uke kwa kufanya usimamizi sahihi wa kichwa kinatoka mda wa kujifungua (controll delivery of head)

✅Kuandaa vifaa vya kumsaidia mtoto kupumua mapema (neonatal resuscitation equipment) ikiwa mtoto atapata changamoto ya kushindwa au kusaidiwa kupumua .

Mara nyingi Precipitate labor haiwezi kuzuilika, hasa ikiwa ni ya asili. Lakini:

Uchungu ukianza kwa kasi isiyo ya kawaida, mama anatakiwa kufika kituo cha afya mara moja.

Kudhibiti matumizi ya dawa zinazoanzisha au kuongeza uchungu.

Ulikaa mda gani hadi ulipokuja kujifungua...! ?

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏
08/12/2025

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏

Hii ni hali ambayo ujauzito unafika zaidi ya wiki 42 bila mama kuingia leba au bila kujifungua. Kwa kawaida ujauzito una...
07/12/2025

Hii ni hali ambayo ujauzito unafika zaidi ya wiki 42 bila mama kuingia leba au bila kujifungua. Kwa kawaida ujauzito unakadiriwa kudumu wiki 40, lakini unaweza kwenda hadi wiki 41 bila kuwa tatizo. Zaidi ya hapo ndiyo huitwa postdate au post-term pregnancy.Baadhi ya zinazoweza kuchangia kutokea kwa hali hii ni ;

▪️Historia ya kuwa na mimba zilizopita muda (postdate) katika ujauzito uliopita

▪️Makosa katika kuhesabu tarehe ya mimba kuanza (mfumo wa hedhi usio wa kawaida)

▪️Mama akiwa na mimba kwa mara ya kwanza (primigravida), Wanawake wenye ndiyo mimba yao ya kwanza huwa katika hatari ya kupata postdate kuliko waliowahi kujifungua.

Kadiri ujauzito unavyopita wiki 41–42, baadhi ya hatari huongezeka, ikiwemo:

Kwa mtoto

▪️Kupungua kwa maji ya uzazi (oligohydramnios)

▪️Placenta kuchoka na kupunguza hewa na virutubisho kwa mtoto

▪️Distress ya mtoto (kupungua mapigo ya moyo)

▪️Uzito mkubwa (macrosomia) → hatari ya kushindwa kupita njia ya uzazi

Kwa mama

▪️Hatari ya kujifungua kwa upasuaji (C-section) kuongezeka

▪️Kuona damu au uchungu wa muda mrefu

Baada ya wiki 41–42 kawaida daktari anaweza kupendekeza:

▪️Induction of labour (kuanzisha uchungu) na itashindikana basi mama atajifungua kwa upasuaji

Ikiwa mimba ishakuwa na week 42 wasiliana mara moja na daktari k**a:

▪️Mtoto kupunguza harakati au kucheza

▪️Kutokwa na damu

▪️Maji kutoka bila uchungu

▪️Maumivu makali isivyo kawaida

▪️Homa

Hakuna mama anaweza kuzuia postdate?

Haiwezi kuzuilika moja kwa moja, lakini:

▪️Kufahamu tarehe sahihi ya hedhi ya mwisho (LMP)

▪️Kufanya ultrasound ya mapema (wiki 8–12) hupunguza makosa ya tarehe ya makadilio

▪️Kufuatilia ujauzito mara kwa mara

Je wewe uwaga unajifungua tarehe ile ile ya makadilio au..!?

Nawatakia usiku mwema.... 😜😌😉
06/12/2025

Nawatakia usiku mwema.... 😜😌😉

Baadhi ya wanawake wajawazito husubiri hadi uchungu uanze ndiyo waanze kufikiria kuhusu maandalizi…Lakini mama, wiki za ...
05/12/2025

Baadhi ya wanawake wajawazito husubiri hadi uchungu uanze ndiyo waanze kufikiria kuhusu maandalizi…
Lakini mama, wiki za mwisho ni nzuri kwa kujiandaa.

▪️PAKI BEGI LAKO LA HOSPITALI

Jumuisha nguo, vitu muhimu vya mtoto, vitafunio, hati, na vitu vya usafi.
Kuwa tayari, uchungu haumsubiri mtu yeyote.

▪️FANYA MAZOEZI YA KUPUMUA KWA KINA NA KUPUMZIKA

Kupumua kwa kina husaidia kudhibiti maumivu ya uchungu wa uchungu.
Fanya mazoezi kwa dakika chache kila siku.

▪️FUATILIA HEKAHEKA AU KUCHEZA KWA MTOTO

Hesabu mateke kila siku.
Ripoti kupungua kwa mizunguko mara moja kwa nurse wako, mkunga wako au daktari wako .

▪️TEMBEA TEMBEA MWILI USHUGHULIKE KIDOGO

Matembezi ya pole pole husaidia mtoto kushuka na kuboresha mzunguko wa damu.

Epuka shughuli zenye nguvu.

▪️ KAA NA MAJI PIA KULA

Maji na chakula kizuri hutoa nguvu kwa ajili ya uchungu wa kujifungua.
Milo midogo ya mara kwa mara hufanya kazi vizuri zaidi kuliko kula ile milo mikubwa mitatu .

▪️JIFUNZE DALILI ZA UCHUNGU WA KUJIFUNGUA

Kubana kwa misuli mara kwa mara, kutokwa au kupasuka kwa chupa la uchungu , shinikizo la nyonga.
Jua wakati wa kwenda hospitalini.

▪️PATA MDA WA KUPUMZIKA.

Mwili wako unafanya kazi kwa bidii.
Pumziko husaidia kutunza nguvu na msawadhiko kihisia.

Wiki za mwisho ni za maandalizi punguza hofu, mungu atatenda kwa uweza wake na daima yupo nawe .
P**i begi lako kila kitu cha mhimu weka , pumzika, fuatilia mienendo ya mtoto, kula na kunywa maji ya kutosha.

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category