AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.⛑️

Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.🩺

Nani anastahili kuachiwa seat hapo na kwa nini...!???Credit ©Kaka Milton Tunge
16/02/2026

Nani anastahili kuachiwa seat hapo na kwa nini...!???

Credit ©Kaka Milton Tunge

Mama, kitendo hicho rahisi cha kusugua tumbo lako kina nguvu zaidi kuliko unavyofikiria. Kwa mtoto Mguso huo sawa na maw...
15/02/2026

Mama, kitendo hicho rahisi cha kusugua tumbo lako kina nguvu zaidi kuliko unavyofikiria. Kwa mtoto Mguso huo sawa na mawasiliano ya ana kwa ana, mtoto anaweza kuhisi hali ya furaha, amani na huzuni kwa mama ndo mama akiwa na huzuni mtoto pia hupunguza kucheza, mama akila chakula kitamu basi mtoto hucheza zaidi, mama akiwa na furaha mtoto pia huwa furaha na kucheza zaidi,hali huongeza ukaribu na muunganiko (bonding) wa mama na mtoto hata baada ya kuja Duniani.
Hivi ndivyo mtoto huhisi Mama anapogusa tumbo lake kwa mikono yake ;👇

▪️Mtoto huhisi utulivu na faraja
Mguso wako hutuma utulivu moja kwa moja tumboni mwako.

Ni k**a kukumbatiana na mtoto wako akiwa ndani.

▪️Mtoto husogea kuelekea mkono wako
Baadhi ya watoto husogea au kupiga mateke unaposugua tumbo lako
Wanafuata mguso wako k**a mchezo hivyo mtoto huhisi k**a vile mnacheza pamoja.

▪️Mtoto anakuwa na anacheza zaidi
Mguso wako huongeza mtiririko wa damu na joto,
kumfanya mtoto atetemeke, anyooshe, na aitikie.

▪️ Mtoto hutambua k**a wakati wa kuungana(bonding)
Homoni zako hubadilika unapogusa tumbo lako.
Mtoto huhisi na kuungana nawe kwa undani zaidi.

▪️ Mtoto huhisi hisia zako
Ukiwa na furaha, umetulia, au umetulia,
mguso wako unamwambia mtoto: "Mama yuko sawa. Uko salama."

▪️Mtoto hupokea ishara za mapenzi
Mwili wako hutoa oxytocin (homoni ya mapenzi)
na mtoto wako hupokea ujumbe huo mara moja.
Ndiyo mama, mtoto wako tayari anahisi upendo wako.

Je ni mwitikio gani huupata kutoka kwa mtoto wako unapogusa tumbo lako.... ⁉️

Nawatakia Valentine njema wapendwa.... 🎈🍓🍿🌹
14/02/2026

Nawatakia Valentine njema wapendwa.... 🎈🍓🍿🌹

Kwa dada na mama yangu mpendwa anayesubiri baraka ya mtoto…Najua safari hii si rahisi.✅Najua kuna siku unacheka mbele za...
13/02/2026

Kwa dada na mama yangu mpendwa anayesubiri baraka ya mtoto…
Najua safari hii si rahisi.

✅Najua kuna siku unacheka mbele za watu lakini ukiwa peke yako machozi yanatiririka. Najua kuna maswali mengi moyoni mwako, na wakati mwingine unajiuliza, “Kwa nini mimi?”

✅Lakini nataka ujue kitu kimoja muhimu sana — thamani yako haipimwi kwa kuwa na mtoto au kutokuwa naye. Wewe ni wa thamani, wa kipekee, na umeumbwa kwa kusudi kubwa.

✅Mungu hakusahau. Mungu hajapuuza maombi yako. Wakati wake si wetu, lakini ni mkamilifu. Kuna hadithi nyingi za wanawake waliochelewa, wakaumizwa, wakangoja… lakini mwisho wake ulikuwa wa furaha.
Usiruhusu shinikizo la watu, maneno ya kejeli au maswali yasiyo na huruma yakuvunje moyo. Ni sawa kuumia. Ni sawa kulia. Lakini usikate tamaa.

✅Endelea kuamini. Endelea kuomba. Endelea kujitunza kimwili na kiroho.
Na hata k**a safari yako itaonekana tofauti na ya wengine, bado wewe ni mwanamke kamili, mwenye nguvu na anayestahili heshima na upendo.

▪️Muda wako utakuja.
▪️Tumaini lako halitapotea.
▪️Wewe ni wa thamani sana.
Mungu akutie nguvu, akufariji, na akupe amani moyoni mwako.

Nawatakia maandalizi mema ya Valentine day ❤️

Nawatakia usiku mwema..... ❤️🙏
12/02/2026

Nawatakia usiku mwema..... ❤️🙏

Hapa chini ni mambo muhimu ya kuangalia unaponunua dawa pharmacy:✅ Tarehe ya kuisha muda (Expiry date)▪️Hakikisha haijai...
11/02/2026

Hapa chini ni mambo muhimu ya kuangalia unaponunua dawa pharmacy:

✅ Tarehe ya kuisha muda (Expiry date)
▪️Hakikisha haijaisha muda.
▪️Usinunue dawa inayokaribia ku-expire k**a utatumia kwa muda mrefu.
▫️Dawa iliyo-expire inaweza:
▪️Kupungua nguvu
▪️Kuwa hatari kwa sababu matumizi holera ya dawa ni hatari kwa Afya ya Ini, Figo na huongeza sumu mwilini.

✅ Hali ya kifungashio (Packaging condition)
Kifungashio kisiwe:
▪️Kimechanika
▪️Kimefunguliwa
▪️Kimevunjika seal
▪️Syrup isiwe imevuja.
▪️Blister pack isiwe imechomoka yaani zile dawa zilizowekwa kwenye pack za paracetamol, amoxilini nk pia dawa isiwe imebadilika rangi, imevunjika vunjika au imesagika au ni dawa aina ya amoxilini isiwe imetengeneza ukungu kungu .

✅ Hifadhi ya dawa (Storage condition)

Angalia k**a inahitaji:
▪️Kuhifadhiwa kwenye friji
▪️Joto la kawaida
Sasa hapa ndiyo tatizo lipo kwa watu wengi dawa wamesema tunza kwenye friji au joto lisizidi 30°C wanaweka dawa madirishani ambako mwanga wa jua unalifikia moja kwa moja na kupunguza ubora wa dawa au kuiharibu kabisa , weka mbali na watoto,

✅Dozi sahihi (Strength)
Kwa wale ambao hutumia dawa nusu nusu au awamalizi dozi wanajiweka kwenye hatari ya kufanya ▪️ugonjwa kuwa sugu
▪️kufanya wadudu wasiwe wanakufa baada ya kutumia dawa (drug resistance)
▪️ gharama ya matibabu kuwa kubwa kutokana na kutopoona kutokana na unywaji wa nusu nusu wa dawa.

✅Epuka kununua dawa bila ushauri
▪️Usinunue antibiotics bila cheti/ushauri wa mtaalamu.
Nunua dawa kutoka:
▪️Pharmacy iliyosajiliwa
▪️ Duka la dawa linalotambulika
▪️Mahali penye mtaalamu wa afya

Vipi wewe huwa unaangalia nini unaponunua....???

AFYA YAKO NA LUCAS

Mwenzenu amekubwa na rosoroso namba 201 la mimba.... Soda inanunuliwa ili tuu kizibo kitafunwe tafunwe.... 😂😂😂.... Wewe ...
10/02/2026

Mwenzenu amekubwa na rosoroso namba 201 la mimba.... Soda inanunuliwa ili tuu kizibo kitafunwe tafunwe.... 😂😂😂.... Wewe rosoroso namba ngapi lilikusumbua kipindi cha mimba... ⁉️

Mayai ni chakula bora sana kwa mama mjamzito 🥚🤰. Yana virutubisho muhimu vinavyomsaidia mama na ukuaji wa mtoto tumboni....
09/02/2026

Mayai ni chakula bora sana kwa mama mjamzito 🥚🤰. Yana virutubisho muhimu vinavyomsaidia mama na ukuaji wa mtoto tumboni.

Hizi ndizo Faida za kula mayai kipindi cha ujauzito
✅Protini nyingi za ubora wa juu
Husaidia:
▪️Kujenga tishu za mtoto
▪️Ukuaji wa misuli na viungo vya mtoto
▪️Afya ya mama kwa ujumla

✅Yana Choline – muhimu sana kwa ubongo wa mtoto
▪️Husaidia ukuaji wa ubongo na mfumo wa fahamu
▪️Hupunguza hatari ya kasoro za ubongo (neural tube defects) k**a vile mgongo wazi na mdomo wa sungura nk

✅Yana madini ya Iron (chuma)
▪️Husaidia kutengeneza damu
▪️Huzuia upungufu wa damu (anemia) kwa mama

✅ Yana madini ya Folate (Vitamin B9)
▪️Muhimu kwa ukuaji sahihi wa mtoto
▪️Hupunguza hatari ya mtoto kuzaliwa na matatizo ya uti wa mgongo

✅Yana Vitamin D
▪️Husaidia ukuaji wa mifupa na meno ya mtoto
▪️Huimarisha kinga ya mama

✅Vitamin B12
▪️Muhimu kwa mfumo wa fahama (nerves systems)
▪️Husaidia uzalishaji wa damu

✅Yana Omega-3 fatty acids (hasa DHA)
▪️Huchangia ukuaji mzuri wa ubongo na macho ya mtoto
▪️Husaidia kudhibiti njaa na kichefuchefu
▪️Mayai hushibisha kwa muda mrefu

⚠️ Tahadhari muhim

✅Mayai yapikwe vizuri kabisa (yai lililochemshwa au kukaangwa vizuri)
✅Epuka kula mayai mabichi au yenye ute ili kuepuka maambukizi k**a salmonella

▫️ Kiasi kinachoshauriwa
Yai 1 kwa siku au 3–5 kwa wiki ni salama na cha kutosha kwa wajawazito wengi
Kifupi: Mayai ni chakula rahisi, nafuu, na chenye faida nyingi sana kwa mama mjamzito na mtoto.

🗣️.............. ⁉️❔
08/02/2026

🗣️.............. ⁉️❔

Nimesikia sauti ikinielekeza nimwambie mtu mmoja, aliyeingia mwaka huu, lakini anahisi kuchoka," MUNGU YUPO KAZINI! HATA...
07/02/2026

Nimesikia sauti ikinielekeza nimwambie mtu mmoja, aliyeingia mwaka huu, lakini anahisi kuchoka," MUNGU YUPO KAZINI! HATA KWENYE NYAKATI ZA GIZA,BADO ANATAWALA."

Ni mapema sana kukata tamaa,...ni mapema sana kutamani mwaka huu uishe.
Neema ambayo MUNGU AMEIACHILIA MWAKA HUU NI KUBWA TENA YA AJABU, ili ikusimamishe tena na kukufuta machozi.
Huu siyo mwaka wa kulialia na kujihurumia...Siyo mwaka wa kuishi kinyonge...Siyo mwaka wa kuruhusu changamoto zikunyong'onyeze.

Neema ya Faida, Neema ya ulinzi, Neema ya Afya, Neema ya kusaidiwa na Mungu ni kuu mno mwaka huu.
Pumzi ya uhai uliyonayo ni zawadi kubwa itakayokusaidia kupiga hatua kubwa ya upenyo na ya kuacha alama njema.

Anachohitaji kwako mwaka huu ni kumpenda sana Yeye na kuishi kwa utii maelekezo yake.

ATAKUSHANGAZA KIPEKEE mwaka huu...Usiogope wala usikate tamaa...!
Shalom...🙏🙏!

●ZABURI 23

Nawatakia ahsubuhi na siku njema....❤️🙏

Wengine huweza kuita dawa za usingizi  au Ganzi (Anaesthesia) ni matumizi ya dawa maalum ili kupunguza au kuondoa maumiv...
06/02/2026

Wengine huweza kuita dawa za usingizi au Ganzi (Anaesthesia) ni matumizi ya dawa maalum ili kupunguza au kuondoa maumivu, hisia au fahamu wakati wa upasuaji au taratibu za kitabibu.

Kuna aina kuu 4 za Anaesthesia:

▪️General Anaesthesia (Anaesthesia ya jumla)
Humfanya mgonjwa apoteze fahamu kabisa

Sifa zake:
✅Mgonjwa hulala usingizi mzito
✅Hahisi maumivu wala hatambui kinachoendelea
✅Kupumua hudhibitiwa na mashine

Hutumika wakati:
▫️Upasuaji mkubwa (mf. upasuaji wa tumbo, kifua, ubongo)
▫️Upasuaji unaochukua muda mrefu

▪️ Regional Anaesthesia

Huzuia maumivu katika sehemu kubwa ya mwili, mgonjwa huwa macho au usingizi hafifu

Aina zake:
✅Spinal Anaesthesia
▫️Dawa huwekwa kwenye mgongo wa chini (CSF)
▫️Huzuia hisia kuanzia kiunoni kushuka chini

Hutumika kwa:
Upasuaji wa kujifungua kwa upasuaji (C/S)
Upasuaji wa miguu

✅Epidural Anaesthesia
▫️Dawa huwekwa karibu na uti wa mgongo (epidural space)
▫️Inaweza kudhibitiwa kwa muda mrefu
Hutumika kwa:
Maumivu ya uchungu wa uzazi
Upasuaji wa nyonga na miguu

▪️Local Anaesthesia

Hufanya sehemu ndogo tu isiwe na maumivu
Sifa zake:
✅Mgonjwa hubaki macho
✅Maumivu huondolewa eneo moja tu
Hutumika kwa:
▫️Kushona vidonda
▫️Kung’oa jino
▫️Taratibu ndogo za upasuaji

▪️Sedation (Anaesthesia ya usingizi hafifu)

Humfanya mgonjwa apumzike, apate usingizi mdogo, lakini bado anaweza kuamshwa
Sifa zake:
✅Hupunguza hofu na maumivu
✅Mgonjwa anaweza kukumbuka kidogo au kabisa
Hutumika kwa:
Kung'oa jino (Dental procedures)

Vipi wewe walitumia ipi....!??

Kutumia kifaa k**a hiki kujipiga maji ukeni (douching) au kujichochea kingono (kujiridhisha) kunaweza kuwa na madhara ya...
05/02/2026

Kutumia kifaa k**a hiki kujipiga maji ukeni (douching) au kujichochea kingono (kujiridhisha) kunaweza kuwa na madhara yafuatayo, hasa k**a kinaingizwa au maji yanaingia kwa nguvu:

✅ Madhara ya kutumia kwa douching

Kuharibu usawa wa bakteria wa ukeni
Uke una bakteria wazuri (lactobacilli). Douching huwaua → huongeza:
▪️UTI
▪️Bacterial vaginosis
▪️Fangasi (candidiasis)
▪️Kuongeza hatari ya maambukizi ya zinaa (STIs)
▪️Maji yanaposukumwa kwa nguvu, hupeleka vijidudu juu hadi kwenye mfuko wa uzazi.
▪️Pelvic Inflammatory Disease (PID)
Maambukizi yanaweza kupanda hadi kwenye:
mfuko wa uzazi
mirija ya uzazi
▪️Kuwasha, maumivu na kutokwa damu kidogo
Shinikizo la maji linaweza kujeruhi kuta laini za uke.
▪️Harufu mbaya kuongezeka badala ya kupungua
Kinyume na imani ya wengi, douching huharibu kinga ya asili.

✅ Ushauri wa kitaalamu:

Uke hujisafisha wenyewe. Usifanye douching. Safisha nje tu (v***a) kwa maji safi.

✅ Madhara ya kutumia kwa kujichochea kingono
▪️Majeraha ya uke au shingo ya kizazi
▪️Maji yenye pressure yanaweza kusababisha mipasuko midogo (micro-tears)
▪️Hatari ya kuingiza bakteria
Kifaa hakijatengenezwa kwa matumizi ya ndani ya uke
▪️Kuvimba au maumivu ya muda mrefu
Haswa k**a matumizi ni ya mara kwa mara
▪️Kuingiza hewa (air embolism – nadra lakini hatari)

✅ Njia salama zaidi
Kwa usafi:
▪️ Maji safi nje tuu
Kwa afya ya uke:
▪️ Epuka douching kabisa

🔴 Muhimu sana
K**a kuna:harufu kali, muwasho, uchafu usio wa kawaida, nenda kituo cha afya, usijitibu kwa douching.

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category