AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.⛑️

Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.🩺

Tuambie kipindi cha ujauzito chakula gani...!?▪️Ulikuwa unakipenda sana... ✅✅▪️Ulikuwa ukipendi kabisa.... ⁉️
10/03/2026

Tuambie kipindi cha ujauzito chakula gani...!?

▪️Ulikuwa unakipenda sana... ✅✅

▪️Ulikuwa ukipendi kabisa.... ⁉️

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏
09/03/2026

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏

▪️Watashindana na wewe lakini hawatakushinda✅Watakujia kwa njia moja na Mungu wa majeshi atawatawanya kwa njia saba▪️Ngu...
08/03/2026

▪️Watashindana na wewe lakini hawatakushinda

✅Watakujia kwa njia moja na Mungu wa majeshi atawatawanya kwa njia saba

▪️Nguvu yako inaongezeka

✅Imani yako inajengwa

▪️Na unaenda mbele kwa jina la Yesu.

Sema AMEN ya Imani

Credit ©Suzzane clement

Hakika.... Hakika... Ukisikia mwili ulikuwa gereji haya ni baadhi tuu ya mabadiliko ambayo yanaonekana na kutokea wakati...
07/03/2026

Hakika.... Hakika... Ukisikia mwili ulikuwa gereji haya ni baadhi tuu ya mabadiliko ambayo yanaonekana na kutokea wakati wa mimba kutoka mwezi mmoja hadi miezi 9... Ndio maana mjamzito baada ya kujifungua anahutaji kupona vizuri ambapo kitalaam tunategemea baada ya week 6 hadi 8 viungo vingi au mabadiliko mengi yaliyotokea kwa kiasi chako mwili utakuwa umerudi katika eneo lake na huo siyo mwisho wa kuendelea kupona na mwili kuendelea kuimarika.

Haya ni baadhi ya mabadiliko ambayo hutokea wakati wa ujauzito.... 👇

▪️Uterasi hupanuka au hupanda juu
Mtoto anapokua, uterasi huinuka kutoka kwenye kizazi kilicho ndani ya nyonga ( pelvis) hadi tumboni.

▪️Viungo husogea ili kutoa nafasi
Tumbo, utumbo, na ini husogea kidogo ili kumpa mtoto nafasi ya kukua.

▪️ Kibofu cha mkojo huwa katika shinikizo
Kadri mimba au umri wa mtoto unavyo kua ndivyo kizazi (Uterus) huweka shinikizo katika kibofu, ndiyo maana akina mama wengi wajawazito hukojoa mara nyingi zaidi.

▪️ Mapafu husogea juu
Kadri mimba au umri wa mimba unavyo kuwa kubwa ndivyo Uterus (kizazi) kinapopanuka na husukuma msuli unaotenganisha kifua na tumbo (diaphragm) kupanda juu, hapa ndo maana wajawazito wanasistizwa kula ubavu na siyo kulala kifudifudi au chali inaweza sababisha mama kupumua kwa shida na kuathiri mtoto pia kukosa hewa ya kutosha (fetal distress).

▪️Utumbo (intestine) husogea upande
Utumbo husogea juu na pande za tumbo wakati wa ujauzito na kutoa nafasi ya ukuaji wa mtoto.

Hivyo basi kiasilia mwili hupitia mabadiliko mbali mbali ya viungo ili kupata nafasi na kumlinda mtoto anayekua.

Niambie nini kimekushangaza.... ⁉️

Kaka Milton shikamoo naomba ujumbe huu uwafikishie wagalatia wote yawezekana utawasadia mahala. Mimi ni binti wa miaka 2...
06/03/2026

Kaka Milton shikamoo naomba ujumbe huu uwafikishie wagalatia wote yawezekana utawasadia mahala. Mimi ni binti wa miaka 25 mwaka jana nilianzisha mahusiano na kijana wa kilokole nikasema asante Mungu kwa huyu mwanaume sasa tukapima afya tukawa vizuri kuna siku akaniambia anaumwa nikaenda kwake kumsalimia nikiwa kwenye ovulation nikamuweka kwenye mtengo akanasa sasa nilipomshika tu dudu akamwaga mkononi basi nikasema labda ana hamu sana. Haikuamka tena nikajaribu wapi unajua ukiwa na HISIA kali halafu mwenzako hata haisimami nikateseka wewe hakuna. Nikatoka kitandani nikaenda kukaa kwenye kiti. Akaniomba samahani basi nikasema labda pressure nikasema nilale ili usiku itakuwa sawa usiku ikisimama alipoweka tu dakika moja tayari na ndio basi tena nikaona nimuulize ana changamoto akawa anakataa

Basi asubuhi nikaona niongee naye kwa nia ya kutaka kujua zaidi akasema amekuwa mtu wa KUJICHUA kwasababu hawataki kufanya mapenzi ni dhambi. Amefanya hiyo miaka sita sasa na akasema alishawahi kuwa kwenye mahusiano na kila mwanamke alimkimbia ndipo nikajua wapo watu tunawaona walokole kumbe wanajichua sana na mwisho wanakuja kuoa wakiwa hawana nguvu ndio maana ndoa za walokole zingine zina changamoto Kwa sababu watu wao walikuwa wanachuaga sana.

Credit Milton Tunge

✅Kujifungua ni tukio kubwa na la thamani katika maisha ya mwanamke na familia kwa ujumla. Baada ya kupitia uchungu na ch...
05/03/2026

✅Kujifungua ni tukio kubwa na la thamani katika maisha ya mwanamke na familia kwa ujumla. Baada ya kupitia uchungu na changamoto za kujifungua, kumpa mama zawadi ndogo kutoka kwa mume au familia ni ishara ya upendo, shukrani na kuthamini juhudi zake. Zawadi inaweza kuwa maua, nguo, maneno mazuri au kitu chochote cha kumbukumbu kinachoonyesha kwamba jitihada zake zinaonekana na kuthaminiwa. Hii humfariji mama kisaikolojia, huongeza furaha na kuimarisha uhusiano wa ndoa.

✅Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa thamanu ya mama haipimwi na zawadi. Wapo kina mama wengi ambao hawajawahi kupewa zawadi baada ya kujifungua, lakini bado wanabaki kuwa wenye thamani kubwa na wenye heshima mbele ya familia na jamii. Wao wanastahili faraja, heshima na upendo sawa.

✅Kwa akina mama ambao hawakuwahi kupewa zawadi, kumbuka kuwa thamani yako ipo katika ujasiri na upendo wako kwa mtoto wako. Kitendo chako cha kuleta maisha mapya duniani ni zawadi kubwa yenyewe. Upendo wa mtoto wako na furaha ya familia yako ni zawadi isiyolinganishwa na kitu chochote.

✅Ni vyema jamii na wanaume kujifunza kuthamini na kuwajali akina mama, kwa maneno mazuri, msaada na hata zawadi ndogo, kwa sababu mama anayejisikia kuthaminiwa huwa na moyo wa furaha na nguvu zaidi katika kulea familia. ❤️

Mda mwingine inatokea tuu k**a dharura uchungu ulikuwa unaenda vizuri mambo yanabadilika tu ghafla inakuwa dharura ya ku...
04/03/2026

Mda mwingine inatokea tuu k**a dharura uchungu ulikuwa unaenda vizuri mambo yanabadilika tu ghafla inakuwa dharura ya kuokoa maisha.

Baadhi ya sababu hizi hapa za mama kujifungua kwa upasuaji ambao haukupangwa yaani dharura (EMERGENCY CESAREAN SECTION).... 👇

▪️ Mtoto kuchoka (fetal distress)
Ikiwa mapigo ya moyo wa mtoto yatashuka ghafla au kuwa yasiyo ya kawaida, madaktari wanaweza kuchukua hatua haraka. Fetal distress hutokea pale uchungu unapochukua mda mrefu, kondo kujizungusha shingoni, mtoto kukosa hewa ya okisijeni akiwa tumboni nk

▪️ Kutokwa na Damu nyingi
Kutokwa na damu nyingi wakati wa uchungu kabla ya kujifungua kunaweza kuwa hatari kwa mama na mtoto.

▪️ Leba Haiendelei au uchungu umekwama hapo mwanzo ulikuwa unaenda vizuri lakini mwishowe ukakoma.
Njia haifunguki.

Mtoto hashuki kwa kwenye nyonga (no engagement),

Mikazo mikali lakini hakuna mwendelezo wa mtoto kushuka wala njia kuendelea kufunguka,

Kukaa muda mrefu sana kwa uchungu (labor) kunaweza kusababisha matatizo.

▪️ Matatizo ya Kiunganishi cha mtoto na mama (cord)
Ikiwa kitovu(cord) kitaachia kabla ya mtoto kuzaliwa na ndiyo hufanya kazi ya kumpa mtoto virutubisho mhimu na oksijeni kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto inaweza kuwa tatizo kwa mtoto hivyo hufanya mama ajifungue kwa upasuaji wa dharura .

▪️ Matatizo ya kondo au Placenta
Ikiwa kondo la nyuma litaziba njia ya kuzaliwa (placenta previa ) au kutengana mapema (placenta abruption ) hapa upasuaji wa dharura unaweza kuhitajika kwakuwa kondo ndiyo limebeba mtoto na njia ya kupita mtoto ikiziba(placenta previa) mtoto atapita wapi.

▪️ Kupasuka kwa kizazi (Uterine Rupture )

Hapa inaweza pelekea
Maumivu makali ya tumbo (sever abdominal pain), mapigo ya moyo yasiyo ya kawaida(abnormal heartrate) na mtoto kuchoka (fetal distress) . Ili kuokoa maisha ya mama na mtoto upasuaji wa dharura unatakiwa kwa haraka.

Tuwafariji wenzetu ambao hujifungua kwa upasuaji kwakuwa nao hayakuwa mahaba au mapenzi yao ilitokea tuu..... Mie nawapenda sana.. ❤️🙏

K**a ni MUNGU amekushikilia,haijalishi wangapi wako nyuma wakikusukuma. ATAKUSAIDIA...!Hutaanguka!Hutaaibika!Hutaishia p...
03/03/2026

K**a ni MUNGU amekushikilia,haijalishi wangapi wako nyuma wakikusukuma. ATAKUSAIDIA...!
Hutaanguka!
Hutaaibika!
Hutaishia pabaya!

➡️Daudi akasema kwenye Zaburi 118:13-14,"Ulinisukuma sana ili nianguke;Lakini BWANA akanisaidia.BWANA ni nguvu zangu na wimbo wangu.Naye amekuwa wokovu wangu."

Credit ©Suzzane Clement

Nacheka k**a mazuri lakini mimba iache iitwe mimba... 😂😂... Hebu fikiria mtu anatafuna mwingine anafura..... Kaona kitu ...
02/03/2026

Nacheka k**a mazuri lakini mimba iache iitwe mimba... 😂😂... Hebu fikiria mtu anatafuna mwingine anafura..... Kaona kitu kwenye TV machozi.. 😂

▪️Utasahau Kila Kitu
Utaingia jikoni na kusahau kwa nini ulienda huko.

▪️ Kulia Bila Sababu isiyo na mantiki
Tangazo kwenye TV? Machozi.
Mume akitafuna kwa sauti kubwa? Machozi.
Hujui hata kwa nini unalia.... 😂😂

▪️Uchovu Ambao Usingizi Hauwezi Kurekebisha
Unaamka umechoka.
Unalala umechoka.
Umechoka tu.

▪️ Kutopenda Chakula Ulichokuwa Ukikipenda
Hicho chakula unachokipenda hapo hata huku wahi kuwaza k**a utakipenda na kile ulichokuwa unakipenda ghafla kinanuka k**a moshi wa jenereta

▪️Kukojoa K**a Ni Hobby Yako Mpya
Umesimama tu kutoka chooni…
Unarudi tena.

Kati ya hayo marosoroso lipi umepitia (umewahi)... Ongeza na mengine pia.... ⁉️😂

MAOMBI MAALUM KWA AJILI YA MWEZI MARCH.(Kwa kila ombi,omba kwa imani kwa zaidi ya dakika 5/kadiri Roho Mtakatifu atakavy...
01/03/2026

MAOMBI MAALUM KWA AJILI YA MWEZI MARCH.
(Kwa kila ombi,omba kwa imani kwa zaidi ya dakika 5/kadiri Roho Mtakatifu atakavyokuongoza)

▪️Ee Bwana Yesu,Asante kwa zawadi ya mwezi mpya,Mwezi March.
▪️Ee Bwana Mungu, Nakusihi ufanye mwezi huu uwe mwezi wa Upenyo,Ushindi,Faida,Fidia na Ongezeko kwangu na familia yangu kwa jina la Yesu.
▪️Kwa jina la Yesu,kila mishale ya mauti ya ghafla,irudi ilikotoka!
▪️Chochote kibaya kilichoelekezwa kwangu ili kuniharibia mwezi wa Tatu hakitafanikiwa kwa jina la Yesu!
▪️Kila sauti za kinyume zinazoongea kinyume changu kwenye mwezi huu wa 3,naziamuru zinyamaze kwa jina la Yesu.
▪️Kila mipango ya misiba, maumivu na vilio kwenye familia na boma letu,haitafanikiwa kwa jina la Yesu.
▪️Kila mishale ya kukandamizwa, ajali za barabarani na hasara,IRUDI ilikotoka kwa jina la Yesu!
▪️Kila sauti za mizimu zinazoongea kinyume cha mafanikio yangu mwezi huu,zinyamaze kwa jina la Yesu.
▪️Mashambulizi ya majini mahaba hayatanipata mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Kila shimo walilonichimbia ili nitumbukie mwezi wa 3, watatumbukia wao kwa jina la Yesu!
▪️Nyota yangu ya mafanikio na ushindi,Nakuamuru, NG'AA mwezi huu na kuniletea faida kwa jina la Yesu.
▪️Mikono yangu,sikia sauti ya MUNGU,FUNGUKA mwezi huu March na umiliki vitu vizuri kwa jina la Yesu.
▪️Miguu yangu,pokea nguvu ya kumiliki popote utakapokanyaga kwa jina la Yesu!
▪️Kichwa changu, pokea nguvu ya mawazo mapya yenye faida mwezi huu wa 3 kwa jina la Yesu!
▪️Yeyote anayepanga anguko langu, ataanguka Yeye kwa jina la Yesu.
▪️Yeyote anayepanga aibu yangu,ataaibika yeye kwa jina la Yesu.
▪️Nyumba yangu, sikia sauti hii; Amani, furaha, kicheko na afya tele ni fungu lako mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Kila madhabahu zinazoongea kinyume na ustawi wangu mwezi huu,KUFA kwa jina la Yesu.
▪️Ee Roho Mtakatifu, nipe neema ya kuomba, kukutumikia,kuishi maisha ya utakatifu mwezi huu kwa jina la Yesu.
▪️Ee Roho Mtakatifu, niongezee hekima,busara na maarifa zaidi mwezi huu kwa jina la Yesu.

●ZABURI 23

Credit © Pastor Suzzane B. G Malisa

Kuanzia week 28  za ujauzito wanaweza kulia au kuonyesha nyuso zenye kufanana na kulia kutokana na mitetemo au miitikio ...
28/02/2026

Kuanzia week 28 za ujauzito wanaweza kulia au kuonyesha nyuso zenye kufanana na kulia kutokana na mitetemo au miitikio ya nje wakiwa tumboni japo hawatoi sauti kutokana na uchanga wa mapafu yao hali hii husaidia kupumua na mawasiliano.... Hapa chini ni baadhi ya mambo ambayo hufanywa na watoto wakiwa tumboni pasipo mama kujua.. 👇

▪️ Wanalia kimya kimya, ndio, watoto wachanga hufanya mazoezi ya kulia tumboni!

▪️Wanaonja chakula chako, chenye viungo, tamu, chungu… mtoto anajua yote 😂

▪️Wanakojoa… na kumeza tena (usipige kelele, ni kawaida!)

▪️Wanaota, wanasayansi wanasema watoto huanza kuota ndoto kabla ya kuzaliwa.

▪️Wanaitikia hisia zako, unapokuwa na huzuni, mtoto pia anaihisi.

▪️ Wanatambua sauti yako, wanamjua mama kabla hata hawajafika.

Lipi limekushangaza kati ya haya.... ⁉️

●Kumbukumbu la Torati 31:6,"Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana BWANA,Mungu wako ndiye a...
28/02/2026

●Kumbukumbu la Torati 31:6,"Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana BWANA,Mungu wako ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha."

Baba katika jina la Yesu, tunapoianza wiki hii, tutangulie kwa nguvu na mkono wako wa neema.
Bariki kazi zetu za mikono.
Bariki mifugo na mazao yetu.
Bariki watoto wetu na jamaa zetu.
Tubariki kwa afya njema.
Baba, nyumba zetu zisipungukiwe chakula, mavazi na malazi.
Baba tunaomba, wiki hii kusiwe na taarifa mbaya kwenye familia na boma zetu.

Baba,k**a kuna safari tutaenda na tusirudi salama wiki hii, tuepushe nayo kwa jina la Yesu.
K**a kuna safari ndugu zetu wataenda na wasirudi wakiwa hai, Baba fanya jambo wasisafiri.

Baba, kwa kila manuizo mabaya dhidi yetu na dhidi ya kazi za mikono yetu, TUNAYAFUTA KWA DAMU YA YESU.

Wiki hii itakuwa nzuri, wiki hii itakuwa na ushindi, wiki hii itakuwa ya faida na fidia.
Wiki hii tutatoka salama na kurudi salama kwa jina la Yesu. Mema yote yatatufuata wiki hii sawa na Zaburi 23.Amen 🙏!

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category