AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.⛑️

Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.🩺

Maji ni msingi wa uhai na nguzo muhimu ya kuondoa  sumu ( detoxification) ya asili ya mwili.Kwa kunywa maji ya kutosha, ...
22/01/2026

Maji ni msingi wa uhai na nguzo muhimu ya kuondoa sumu ( detoxification) ya asili ya mwili.

Kwa kunywa maji ya kutosha, unausaidia mwili wako kufanya yafuatayo:

▪️ Kusaidia figo kuchuja na kutoa sumu kupitia mkojo
▪️ Kuliwezesha ini kutekeleza majukumu yake ya uondoaji wa taka mwilini
▪️Kuboresha mmeng’enyo wa chakula na kuzuia kukosa choo
▪️Kusaidia udhibiti wa joto la mwili na utoaji wa taka kupitia jasho

✅ Ukweli wa kisayansi:
Mwili hauhitaji vinywaji vya “detox” maalum.
Maji ya kutosha + lishe bora = detoxification halisi.

Unapohisi kiu mhimu kunywa maji kwa sababu ukinywa soda au kinywaji chochote baridi(carbonated drinks) unaongeza kiu mara mbili ya mwanzo kwa sababu sukari iliyopo kwenye vinywaji hivo ikishaingia mwilini baada ya kunywa nayo itahitaji maji ili iweze kuyeyushwa.
Kunywa maji, linda afya yako, heshimu mwili wako.

Hivi kati ya soda au maji kipi hukata kiu yako kabisa...!??

Mungu akupe neema ya kula matunda mema uliyoyataabikia...Mungu akupe uhai na uzima wa kufurahia matunda yako....Hutakufa...
21/01/2026

Mungu akupe neema ya kula matunda mema uliyoyataabikia...
Mungu akupe uhai na uzima wa kufurahia matunda yako....
Hutakufa kabla ya kula matunda yako kwa jina la Yesu...!

Mwaka huu, MUNGU ATAKUSAIDIA KIPEKEE...
Taabu ya mikono yako haitaenda bure kwa jina la Yesu...🙏🙏!

●ZABURI 23 🙏!

Chanjo huokoa maisha ya hadi watoto milioni 3 kila mwaka.Chanjo hukinga maradhi, ulemavu na vifo vitokanavyo na magonjwa...
20/01/2026

Chanjo huokoa maisha ya hadi watoto milioni 3 kila mwaka.
Chanjo hukinga maradhi, ulemavu na vifo vitokanavyo na magonjwa yanayozuilika kwa chanjo ikiwa ni pamoja na surua, homa ya ini (hepat**isi B), dondakoo, kifaduro, nimonia, polio, kuhara kunakosababishwa na virusi vya rota, rubela na pepopunda.
Kisayansi chanjo ni kitendo cha kupewa kinga mwili kwa njia ya kuamsha vitoa kinga viwe tayari kupambana na adui ambaye wanamjua tayari.

Umuhimu wa chanjo
Watoto waliopata chanjo huwa wamekingwa dhidi ya magonjwa hatari, ambayo kwa kawaida huweza kusababisha ulemavu au kifo. Watoto wote wana haki ya kupata kinga hii. Kinga ya utotoni ni muhimu sana hasa kwa ukuaji wa baadae. Hivyo basi, chanjo kwa mtoto katika mwaka wake wa kwanza na katika mwaka wa pili ni muhimu sana.
Ni muhimu pia, kina mama wajawazito kupata chanjo ya pepopunda ili kujikinga wao wenyewe na watoto wao wanaozaliwa. Wazazi na walezi wengine wanapaswa kufahamu sababu za umuhimu wa chanjo, ratiba ya chanjo inayotumika na mahali chanjo inakotolewa kwa watoto.
Wazazi na walezi wengine wanapaswa kufahamu kuwa kutoa chanjo kwa mtoto mgonjwa kidogo au mwenye ulemavu au mwenye upungufu wa lishe ni salama.

Ukweli kwa ajili ya familia na jamii kuhusu chanjo
✅Chanjo ni jambo la lazima. Kila mtoto ni lazima apate chanjo zote zilizopendekezwa. Kinga ya utotoni ni muhimu sana; chanjo katika mwaka wa kwanza na wa pili zina umuhimu wa pekee. Wazazi wote au walezi wengine wanapaswa kuzingatia ushauri wa mtaalamu wa afya kuhusu muda wa kukamilisha chanjo zinazohitajika.

✅Chanjo hutoa kinga dhidi ya magonjwa mengi hatarishi. Mtoto ambaye hajapata chanjo yuko katika hatari kubwa ya kupatwa na maradhi, ulemavu wa kudumu au hata kupoteza maisha.

✅Mama wote wajawazito pamoja na watoto wao wanapaswa kukingwa dhidi ya pepopunda. Hata k**a mama aliwahi kupata chanjo kabla , anapaswa kupata ushauri wa mtaalamu wa afya kuhusu k**a bado anahitaji kupewa chanjo ya pepopunda.

✅Sindano mpya hazina budi kutumika kwa kila mtu anayepata chanjo. Kila mtu anapaswa kudai sindano mpya kwa kila chanjo anayopewa.

✅Ugonjwa huweza kuenea haraka watu wengi wanapokuwa wamekusanyika pamoja. Watoto wote wanaoishi katika maeneo yenye mkusanyiko mkubwa , hasa katika mazingira ya wakimbizi au ya watu waliojikusanya kutokana na janga fulani, wanapaswa kupewa chanjo haraka.

✅Kadi ya chanjo ya mtoto (au ya mtu mzima) haina budi kuwasilishwa kwa mtoa chanjo kabla ya kutolewa kwa chanjo.

Aina za chanjo

▪️BCG (Bacile Calmette-Gu"rin)
Watoto wote wanastahili kupokea chanjo itwayo BCG (Bacile Calmette-Gu"rin) vaccine. Hii huumpa mtoto kinga dhidi ya aina zingine za kifua kikuu na ukoma.

▪️DTP au DPT (Dondakoo, Pepopunda na Kifaduro)
Watoto wote wanastahili chanjo dhidi ya dondakoo, pepopunda na kifaduro kupitia aina ya chanjo iitwayo DTP au DPT vaccine. Viini vya dondakoo husababisha maambukizi ya njia ya kuingizia hewa na huenda ikasababisha shida za kupumua na hata kifo. Pepopunda nayo husababisha kukauka kwa misuli na maumivu makali yanayo sababishwa na mkazo wa misuli. Mkazo huo wa misuli unaweza sababisha kifo. Kifaduro huathiri njia ya kuigizia hewa na kusababisha kikohozi kinachoweza dumu wiki nne hadi nane na ni hatari sana kwa watoto wachanga.

Wanawake wote waja wazito na watoto wachanga wanahitaji chanjo ya pepopunda.

▪️Surua
Watoto wote wanastahili kupokea chanjo dhidi ya surua. Maradhi ya surua husababisha utapiamlo, udhaifu wa maendeleo ya ubongo na huweza kufanya mtoto kiziwi au kipofu. Ishara zinazoelekeza kuwa mtoto anaweza kuwa anaugua surua ni pamoja na kuongezeka kwa joto mwilini, upele, kikohozi, kumwaga k**asi na macho kubadilika na kuwa mekundu. Tahadhari, mtoto anaweza kufa kutokana na surua.

▪️Polio
Watoto wote wanastahili chanjo dhidi ya polio. Dalili za polio ni utepe kwenye mguu au mkono na udhaifu wa kukitumia kiungo kilicho athirika. Kwa kila watoto mia mbili wanaoambukizwa maradhi ya polio, mmoja atapata ulemavu wa maisha.

Ratiba za chanjo hutofautiana kulingana na nchi au sehemu ya nchi unayoishi. Ni muhimu kufuatilia ratiba ya chanjo kwa mujibu wa mwongozo wa taifa. Watoto wanastahili kupokea chanjo kwa umri unaostahili na kwa muda unaostahili.
Pamoja na kutofautiana huku kwa ratiba za chanjo kati ya nchi na nchi, unaweza kufuatilia utaratibu uliopendekezwa na CDC (Centre for Disease Control) hapa chini.

We una mtazamo gani kuhusu chanjo...!?

Mtoto anapozaliwa na uzito wa zaidi ya kilo nne (4kg) inasemwa kwamba huyo mtoto ni mkubwa. Hata hivyo hatari huongezeka...
19/01/2026

Mtoto anapozaliwa na uzito wa zaidi ya kilo nne (4kg) inasemwa kwamba huyo mtoto ni mkubwa. Hata hivyo hatari huongezeka zaidi mtoto anapozaliwa na zaidi ya kilo nne na nusu(4.5kg), wataalam wenyewe wanaita Macrosomia.

Sababu kubwa zinazosababisha mtoto kuzaliwa mkubwa ni
▪️Sababu za kurithi.
▪️Mama kuwa na uzito mkubwa kabla au wakati wa ujauzito, Mama anapoongezeka uzito mkubwa wakati wa ujauzito inawezekana akajifungua mtoto mwenye uzito mkubwa
▪️Ugonjwa wa Kisukari. Ugonjwa wa Kisukari ndio sababu kubwa ya mama kuzaa mtoto mkubwa haswa kisukari kinacho sababishwa na ujauzito (Gestational Diabetes)
▪️Historia ya mama kujifungua watoto wenye uzito mkubwa katika mimba zilizopita au hapo awali.

Kinyume na watu wengi wanavyofikiria kuzaa mtoto mkubwa ni sifa, kitaalam sio salama. Mtoto mkubwa anafanya mama kuwa katika hatari kubwa ya kujifungua kwa njia ya upasuaji,mama kuchanika sana wakati wa kujifungua,mama kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua, uchungu kuchukua mda mrefu.

Pia inaongeza hatari ya mtoto kuumia au kuvunjika wakati wa kuzaliwa haswa bega au mkono . Madhara mengine ni pamoja na mtoto kukwama kutoka kutokana na mabega kuwa makubwa hivyo kushindwa kutoka kitamu Shoulder Dystocia, mtoto kuchoka sana baada ya kuzaliwa pengine kutokana na uchungu kuchukua mda mrefu, sukari ya mwili kushuka (hypoglycaemia) baada ya mtoto kuzaliwa na huongeza hatari ya mtoto kupata kisukari ukubwani na unene hapo baadaye.

Wewe ulipojifungua mwanao alikuwa na kilo ngapi.....!?

WATU WA MUNGUTumefika 2026 kwa sababu kila silaha iliyofanyika kinyume chetu 2025 HAIKUFANIKIWA.Mwaka huu ikawe hivyo hi...
18/01/2026

WATU WA MUNGU
Tumefika 2026 kwa sababu kila silaha iliyofanyika kinyume chetu 2025 HAIKUFANIKIWA.

Mwaka huu ikawe hivyo hivyo.
●Utavuka vizuizi vyote
●Utashinda upinzani wote
●Utakua imara katikati ya changamoto ngumu
●Utastawi katikati ya chuki na fitina
NA UTAJUA YA KUWA MUNGU YUPO UPANDE WAKO

Pokea neema ya kuvuka, kushinda na kustawi kwa jina la Yesu

Katoto kamezaliwa kachafuuuu. Kuna watu wakiona huyu mtoto alivyo watakwambia mtoto kazaliwa mchafu. Hapo tena utapewa s...
17/01/2026

Katoto kamezaliwa kachafuuuu. Kuna watu wakiona huyu mtoto alivyo watakwambia mtoto kazaliwa mchafu. Hapo tena utapewa sababu mbalimbali za mtoto kuzaliwa mchafu. Kuna watakaosema mamake alikuwa anakula vitu fulani ambavyo hakutakiwa kula.

✅ Inayovuma zaidi ni ile ya kusema mama aliendelea kujivinjari na baba k hadi wiki za mwishoni? Hizo zote ni imani potofu!

✅UKWELI ni kuwa hiyo sio uchafu ni kitu kizuri kwa mtoto. Hiyo inaitwa VERNIX CASEOSA . Ni k**a losheni inayomsiliba mtoto akiwa tumboni tangu mimba ikiwa na wiki 27.

✅Huwa inaanza kupotea mwilini mwa mtoto kuanzia wiki ya 36 ya mimba, ingawa kuna watoto huwa wanazaliwa nayo. Hasa wale wanaowahi kidogo kuzaliwa.

✅Kazi yake ni kulinda ngozi ya mtoto akiwa tumboni.
Kumbuka mtoto anazungukwa na maji kipindi chote akiwa tumboni hii vernix Caseosa inasaidia yale maji yasidhuru ngozi ya mtoto.

✅Vernix Caseosa haina uhusiano na chakula wala mama kushiriki na baba tendo.
Iwapo mwanao atazaliwa nayo wala usiwe na wasiwasi, huwa inatoka kirahisi mtoto akiogeshwa au kufutwa ingawa nchi za wenzetu huwa wanaacha mtoto aliyezaliwa hivyo akaekae nayo kwani inaisha yenyewe.

✅Hamna kitu utakachokula ama utakachofanya mwanao asizaliwe nayo, huwa inatokea tu watoto wengine wanazaliwa nayo.

Vipi wako alizaliwa bila hiyo....!?

Hali hii inaweza kuwa maambukizi au uvimbe wa tishu za t**i, mara nyingi huwapata wanawake wanaonyonyesha, hasa ndani ya...
16/01/2026

Hali hii inaweza kuwa maambukizi au uvimbe wa tishu za t**i, mara nyingi huwapata wanawake wanaonyonyesha, hasa ndani ya wiki au miezi ya mwanzo baada ya kujifungua. Ambapo mat**i yanaziba mirija ya kupitisha maziwa au bakteria wanaingia kupitia chuchu iliyopasuka, na kusababisha uvimbe, maumivu na dalili za maambukizi.

Sababu za Mast**is

▪️Kunyonyesha kwa njia isiyo sahihi (mtoto hak**atishi t**i VIZURI AU wapo akina mama hupendelea hunyonyesha mtoto t**i moja mara kwa mara na lingine kutomnyonyesha mara kwa mara )
▪️Kuchelewesha kunyonyesha au kukamua maziwa
▪️Mirija ya maziwa kuziba (blocked milk ducts)
▪️Chuchu kupasuka au kuumia
▪️Kuvaa sidiria inayobana sana
▪️Kinga ya mwili kushuka

Dalili za Mast**is

▫️ Maumivu makali ya t**i
▫️Titi kuwa joto, kuvimba na kuwa jekundu
▫️ Homa, baridi, uchovu
▫️Maumivu wakati wa kunyonyesha
▫️Wakati mwingine usaha kutoka kwenye chuchu

Aina za Mast**is

✅Non-infectious mast**is – uvimbe bila maambukizi (hasa maziwa kuziba)
✅Infectious mast**is – kuna bakteria (mara nyingi Staphylococcus aureus)
✅Breast abscess – hatua mbaya zaidi, usaha hukusanyika ndani ya t**i

Matibabu ya Mast**is

▪️Endelea kunyonyesha au kukamua maziwa (ni salama kwa mtoto)
▪️ Kanda t**i kwa maji ya vuguvugu kabla ya kunyonyesha pia Massage ya t**i kuelekea chuchu
▪️Pumzika na kunywa maji ya kutosha
▪️Dawa za maumivu (k**a paracetamol)

Mama atapewa Antibiotics ikiwa Dalili ni kali
Homa inaendelea zaidi ya saa 24–48
Kuna dalili za maambukizi makubwa

Ili kujikinga dhidi ya Mast**is Mama

✅ Hakikisha mtoto unamk**atisha t**i vizuri
✅ Nyonyesha mara kwa mara
✅ Badilisha nafasi za kunyonyesha yaani ukimpa t**i la kulia mda mwingine unaponyonyesha mpe la kushoto.
✅ Epuka sidiria inayobana
✅ Tunza chuchu, epuka kupasuka

Ni vizuri ukiona dalili ukawa hi hospital kituo cha karibu nawe siyo hadi tuu dalili ziwe k**a hizi
▫️Homa kali
▫️ Maumivu yanazidi
▫️ Uvimbe mgumu haupungui
▫️Dalili hazipungui baada ya siku 2

Je umewahi pata changamoto k**a hii na ulikabiliana nayo vipi..... ..!??

Alikujibu nini.......!!!???
15/01/2026

Alikujibu nini.......!!!???

😂😂😂........ Kwa kweli naomba mungu kila  mmoja wenu humu ampe hitaji lake la moyo kwa mwaka huu 2026.Nawapenda sana.. 🙏😂...
14/01/2026

😂😂😂........ Kwa kweli naomba mungu kila mmoja wenu humu ampe hitaji lake la moyo kwa mwaka huu 2026.

Nawapenda sana.. 🙏😂❤️

Hongera sana.... Nami nashukuru kwa kushukuru pia kunitia moyo kutokana na kazi ambayo mungu amenituma kwenu, mimi na we...
13/01/2026

Hongera sana.... Nami nashukuru kwa kushukuru pia kunitia moyo kutokana na kazi ambayo mungu amenituma kwenu, mimi na wewe ni waja wema wa mungu.... Kila jema 2026 liwe upande wenu, Nawapenda sana... 🙏❤️

Hali hii hutokea pale ambapo  mjamzito hupata presha ya juu (≥140/90 mmHg) ambayo hutokea ➡️ baada ya wiki ya 20 ya ujau...
13/01/2026

Hali hii hutokea pale ambapo mjamzito hupata presha ya juu (≥140/90 mmHg) ambayo hutokea
➡️ baada ya wiki ya 20 ya ujauzito
➡️ bila kuwepo kwa protini kwenye mkojo (tofauti na pre-eclampsia).

Mara nyingi presha hii huonekana kwa mara ya kwanza wakati wa ujauzito
Hupungua au kuisha baada ya kujifungua (ndani ya wiki 6)

Sababu au Chanzo halisi hakijulikani 100%, lakini Kuna kuna sababu k**a hizi zinaweza kuchangia kutokea kwa Gestational Hypertension
✅Mabadiliko ya homoni
✅Msongo wa mawazo (stress)
✅Urithi (genetic factors)

Baadhi wa wajawazito walioko katika hatari ya kupata Gestational Hypertension ni wenye
▪️Ujauzito wa kwanza
▪️Umri 35
▪️Uzito mkubwa kupita kiasi (obesity)
▪️Historia ya presha kabla au kwenye mimba ya nyuma
▪️Mimba ya mapacha au zaidi
▪️Kisukari, magonjwa ya figo
▪️Kipindi kifupi kati ya mimba moja na nyingine

Mara nyingi haina dalili za wazi(often silent ) , ndiyo maana kliniki ni muhimu sana lakini ikizidi inaweza kuambatana na:
✅Maumivu ya kichwa makali
✅Kizunguzungu
✅Kuona ukungu au maruweruwe
✅Kuvimba uso, mikono, miguu (kupita kiasi)
✅Kichefuchefu au maumivu ya juu ya tumbo

Kwa mama inaweza kusababisha
▪️Kuendelea na kuwa Pre-eclampsia au Eclampsia
▪️Kiharusi (stroke)
▪️Matatizo ya figo au ini
▪️Kujifungua kwa dharura

Kwa mtoto inaweza sababisha

▫️Mtoto kukua polepole tumboni (IUGR)
▫️Kuzaliwa njiti (preterm birth)
▫️Kukosa hewa ya kutosha (placental insufficiency)
▫️Uzito mdogo wa kuzaliwa

Matibabu na Usimamizi
Hakuna “tiba ya kuondoa kabisa” isipokuwa kujifungua, lakini presha hudhibitiwa kwa:

✅Kufuatiliwa karibu kliniki(inahitaji uangalizi wa karibu)
✅Dawa salama za presha kwa wajawazito ( kulingana na daktari)
✅Kupunguza matumizi ya chumvi
✅Kupumzika vya kutosha
✅Kuepuka stress
✅Kula lishe bora

⛔ Hairuhusiwi kutumia dawa za presha bila ushauri wa mtaalamu.

👉 Presha ya ujauzito ni hali inayoweza kudhibitiwa ikiwa itagunduliwa mapema
👉 Kliniki za mara kwa mara ni silaha kuu
👉 Mama wengi hupona kabisa baada ya kujifungua

Je umewahi pitia au pata changamoto hii, Je ulipata dalili gani.....!?

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category