AFYA YAKO NA LUCAS

AFYA YAKO NA LUCAS Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.⛑️

Karibu kwenye ukurasa wa Elimu ya Afya 🫶
Pata maarifa sahihi kuhusu magonjwa, lishe, uzazi na mtindo bora wa maisha.🩺

Ninakuombea; Mwezi huu wa APRIL uwe Mwezi mzuri kwako kwa jina la Yesu...!Ikiwa ni Mwezi waNguvu ya Msalaba Ufufuo wa Kr...
01/04/2026

Ninakuombea; Mwezi huu wa APRIL uwe Mwezi mzuri kwako kwa jina la Yesu...!

Ikiwa ni Mwezi waNguvu ya Msalaba Ufufuo wa Kristo Yesu, ninakuombea," NGUVU YA MSALABA WA YESU IKUSHINDIYE YOTE KWA JINA LA YESU!"

Nguvu ya UFUFUO, Ifufue kila chema na kizuri kwenye maisha yako....!

Nakutangazia UZIMA TELE,AMANI, FURAHA, FAIDA, FIDIA,KIBALI, FURSA NZURI, NGUVU MPYA, MAFANIKIO KWENYE KILA ENEO LA MAISHA YAKO, ULINZI WA KIUNGU, USIPUNGUKIWE KITU, NGUVU MPYA kwa jina la YESU KRISTO.....Amen 🙏!

Happy New month of April to us all...🌹🙏!

●Warumi 8:11,"Lakini,ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu,yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu."

Credit ©Suzzane clement

Una kumbukumbu yeyote na hivi vifaa au Kuna kimoja wapo unakikumbuka....‼️⁉️
31/03/2026

Una kumbukumbu yeyote na hivi vifaa au Kuna kimoja wapo unakikumbuka....
‼️⁉️

Kwa kawaida kila mtu huzaliwa na nyama za pua ambazo kitalaam wanaita ADENOID, kazi ya nyama hizo pua huwa ni kudaka au ...
30/03/2026

Kwa kawaida kila mtu huzaliwa na nyama za pua ambazo kitalaam wanaita ADENOID, kazi ya nyama hizo pua huwa ni kudaka au Kupambana au Kunasa (trapping) bakteria na virusi hivyo basi adenoid ni sehemu ya kinga ya mwili (lymphatic tissue) na ndo maana hupambana na hao bakteria na virusi wanaotaka kuingia mwilini kupitia njia ya pua pia adenoid huwa imara sana katika kupambana na bakteria na virusi kati ya umri wa miaka 3 hadi 6 na baada ya hapo basi hupotea.. Sasa kwa baadhi ya watoto nyama hizi za pua huwa kubwa na kupelekea kuziba kwa njia ya hewa. Hi ndo husababisha baadhi ya watoto kupumlia mdomo, akorome akiwa amelala na mda mwingine mafua yasiyopoona. Iwapo mtoto ataendelea kuwa na tatizo hili kwa mda mrefu huathiri ukuaji wa uso wake na kusababisha kuwa na uso uliochongoka, meno ya juu kutoka nje nk na kitalaam hali hii wanaita Adenoid facies. Ikiwa mtoto atakuwa na athari hii basi utapasuaji(adenoidectomy) wa kuondoa nyama hizi unatakiwa.

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏
28/03/2026

Muwe na usiku mwema..... ❤️🙏

Moja ya kiburudisho pendwa kwa watoto mashuleni, nyumbani pia baadhi ya Wazazi hutumia k**a njia ya kubebembelezea watot...
27/03/2026

Moja ya kiburudisho pendwa kwa watoto mashuleni, nyumbani pia baadhi ya Wazazi hutumia k**a njia ya kubebembelezea watoto wao.... Sasa barafu (ice cream) kwa watoto huwa na changamoto k**a vile kuongeza hatari ya watoto kutopoona kikohozi, wengine hupata Tonsili (tonsillitis).. Kuna mama mmoja alisimulia kisa chake kwamba zilipelekea mtoto akafanyiwa upasuaji wa kuondoa tonsil (Tonsillectomy).. Sababu mojawapo ya kutokea kwa tonsillitis ni maambukizi matumizi ya vitu vya baridi ambavyo hupelekea kuvimba kwa tonsil pia bakteria ikiwa zitaandaliwa katika mazingira yasiyo salama kwa kuwa wadudu wengi hupendelea sukari muno mda mwingine zinaweza sababisha kutapika na kuhara... Changamoto nyingine huchangia kutoboka na meno kuoza kutokana na uwepo wa sukari ukizingatia watoto wengi wana usafi duni wa kinywa.

Tumbie wewe kwa udhoefu wako kuhusu hili.... ⁉️

Vipi uwaga unampa mwanao.... ‼️Aya muwe na usiku mwema... ❤️🙏
26/03/2026

Vipi uwaga unampa mwanao.... ‼️

Aya muwe na usiku mwema... ❤️🙏

Hapo...hatua ipi... ❕❗Namba 1️⃣.... Unasubiri kupata... ⁉️Namba 2️⃣..... Unategemea kujifungua .... ⁉️Namba 3️⃣.... Taya...
25/03/2026

Hapo...hatua ipi... ❕❗

Namba 1️⃣.... Unasubiri kupata... ⁉️
Namba 2️⃣..... Unategemea kujifungua .... ⁉️
Namba 3️⃣.... Tayari ushajifungua na unambeba....⁉️

▪️Hivi ushawahi kupewa zawadi ukiwa  P na my wako.... ⁉️▪️My wako ashawahi mkitupe ukiwa  P... ⁉️
23/03/2026

▪️Hivi ushawahi kupewa zawadi ukiwa P na my wako.... ⁉️

▪️My wako ashawahi mkitupe ukiwa P... ⁉️

Wasichana wengi huanza hedhi yao ya kwanza (hedhi ya kwanza) kati ya umri wa miaka 10 na 15, huku wastani wa umri ukiwa ...
22/03/2026

Wasichana wengi huanza hedhi yao ya kwanza (hedhi ya kwanza) kati ya umri wa miaka 10 na 15, huku wastani wa umri ukiwa karibu miaka 12 hadi 12.5. Ingawa baadhi wanaweza kuanza mapema k**a miaka 8 au kuchelewa k**a miaka 16, inashauriwa kushauriana na daktari ikiwa hedhi haijaanza kufikia umri wa miaka 16.

Baadhi ya ushauri ambao Mzazi anatakiwa kumpa binti ambaye anaanza kuingia hedhi... 👇

▪️ Elimu ya msingi kuhusu hedhi

Mwelezee kwa lugha rahisi:
Hedhi ni nini na kwa nini hutokea
Ni jambo la kawaida, si ugonjwa
Mzunguko wa hedhi (siku 21–35 kwa wastani)
Hii humsaidia asiogope au kuona aibu.

▪️Usafi wa mwili (Personal hygiene)

Mfundishe:
Kutumia pedi safi (sanitary pads) na kubadilisha mara kwa mara (kila masaa 4–6)
Kuoga kila siku
Kuosha sehemu za siri kwa maji safi (bila kemikali kali)

▪️Lishe bora

Mpe chakula chenye:
Damu (mfano: maini, nyama, mboga za majani)
Madini ya chuma (iron) kuzuia upungufu wa damu
Maji ya kutosha

▪️ Maumivu ya hedhi

Mweleze kuwa:
Maumivu madogo ni kawaida
Anaweza kutumia maji ya uvuguvugu tumboni au kupumzika
Akipata maumivu makali sana, apelekwe hospitali

▪️Mabadiliko ya mwili na hisia

Mweleze kuwa:
Atapata mabadiliko k**a ukuaji wa matiti na nywele sehemu za siri
Hisia zinaweza kubadilika (hasira, huzuni) — ni kawaida

▪️Kujilinda na elimu ya mahusiano

Hii ni muhimu sana:
Mweleze kuhusu mipaka ya mwili wake (body boundaries)
Asikubali kuguswa sehemu za siri na mtu yeyote
Mfundishe kusema “hapana” na kuripoti vitendo visivyofaa
Anza kumuelimisha taratibu kuhusu ujauzito na mahusiano salama

▪️Kuondoa aibu na kujenga kujiamini

Mruhusu aulize maswali bila kuogopa
Usimkaripie au kumdharau
Mpe faraja na msaada wa kihisia

▪️Ufuatiliaji wa afya

Angalia k**a hedhi zake zinaenda kawaida
Ikiwa kuna damu nyingi sana, maumivu makali, au hedhi kutokuwepo kwa muda mrefu — muone daktari
Kwa kifupi, mzazi anatakiwa kuwa rafiki, mwalimu, na mlezi wa karibu katika hatua hii.

AFYA YAKO NA LUCAS

Eid njema.... ❤️🤲🙏
21/03/2026

Eid njema.... ❤️🤲🙏

Ongezea hadithi zingine ambazo hatujawahi zisikia na hazina ukweli wowote... Na hizi hapa chini nimekuandalia ni baadhi ...
20/03/2026

Ongezea hadithi zingine ambazo hatujawahi zisikia na hazina ukweli wowote... Na hizi hapa chini nimekuandalia ni baadhi tuu.. ❗

▪️Kutokwa na damu nyingi ni kawaida, kutaacha peke yake.

Si kweli! Kutokwa na damu nyingi kunaweza kuua ndani ya saa chache. Usisubiri nenda hospital ikiwa unatokwa na damu ni nyingi sana.

▪️Usioge kwa siku kadhaa baada ya kujifungua.

Ushauri usiofaa. Usafi huzuia maambukizi. Unaweza kuoga kwa maji ya uvuguvugu, ikiwa umejifungua kwa upasuaji weka tu mishono safi na kavu .

▪️Kunywa pombe kali ili kuponesha majeraha ya uzazi haraka, hufanya mtoto awe na akili pia kuongeza maziwa ya mama.
Pombe haiponeshi , wala haiboreshi uzalishaji wa maziwa kwa mama . Hudhoofisha mwili wako tu na inaweza kumdhuru mtoto wako na kupelekea akawa na udumavu, utindio wa ubongo,kuwa na uwezo mdogo wa kupambanua mambo nk hali ambayo kitalaam wanaita fetal alcohol syndrome (FAS).

▪️Funga tumbo lako vizuri mara tu baada ya kujifungua.
Kufunga tumbo lako baada ya kujifungua husaidia kupona haraka, kupunguza maumivu pia husaidia tumbo lisiwe kubwa. Si kweli!

▪️Usilie au kulalamika, kila mwanamke hupitia.
Utawasikia wafariji au wanaomzunguka mama wanasema na kuwaambia wengine baada ya kujifungua, ni kweli kila mama hupitia Je mapito yangu ni Sawa na yako ⁉️ Zungumza ikiwa unahisi huzuni, dhaifu, au kuzidiwa. Unastahili msaada.

▪️Mara tu unapojifungua, hakuna haja ya kwenda hospitalini tena.
Uongo! Uchunguzi wa baada ya kujifungua unaokoa maisha. Hugundua shinikizo la damu, maambukizi, au matatizo ya tumbo mapema

▪️Mtoto akiwa analia mara kwa mara hashibi hivyo aanzishiwe uji mapema.. Eti maziwa ya mama hayatoshiii ebooo❗

▪️Mtoto akiwahi kuota meno ya plastic atakuwa mchawiii na atawamaliza wote... 😂

▪️Mtoto meno yakichelewa kuota ana meno magumu.. 😂😂
▪️Mtoto kuharisha ni hatua za ukuaji... 😂
▪️Mate ya bibi huponesha kitovu haraka.. 😂

Tuongezee zingine kwenye comment section... 🤣

Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when AFYA YAKO NA LUCAS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to AFYA YAKO NA LUCAS:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category