Surgical Clinic Mtwara

Surgical Clinic Mtwara Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Surgical Clinic Mtwara, Medical and health, P. O. BOX MTWARA, Mtwara.

31/01/2020

Tunapenda kuwataarifu kwamba kumefunguliwa kliniki mpya ya ushauri wa magonjwa ya upasuaji ndani ya Mtwara Mjini maeneo ya Shangani Magharibi barabara ya Masandube jirani na hosteli za Mama Mpini.

Kliniki hii inaongozwa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya upasuaji kutoka Ulaya nchini Poland Dr. Jank ambaye aliwahi kufanya kazi zaidi ya miaka 25 katika hospitali ya Nyangao mkoani Lindi.

Tunasaidia katika matatizo yafuatayo:-
1. Magonjwa ya tumbo yasiyoeleweka k**a vile maumivu ya tumbo kwa muda mrefu, kujaa kwa tumbo, kuharisha, kushindwa kupata choo, kutapika na uvimbe tumboni
2. Matatizo katika njia ya mkojo k**a vile kushindwa kupata mkojo, kutokwa na mkojo bila kujizuia, maumivu katika njia ya mkojo, kutokwa na damu au usaha katika njia ya mkojo, maumivu katika kibofu cha mkojo au figo.
3. Matatizo katika njia ya haja kubwa k**a vile kutokwa na damu au usaha katika njia ya haja kubwa, maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, uvimbe katika njia ya haja kubwa k**a vile bawasili n.k
4. Mabadiliko mbalimbali katika ngozi k**a vile uvimbe usiokuwa wa kawaida, kutokwa na damu katika ngozi bila sababu, vidonda sugu au fistula, kucha zinazoota vibaya mfano kujichimbia
5. Matatizo yatokanayo na kuumia/ajali k**a vile maumivu ya muda mrefu, ulemavu, kushindwa kutumia miguu au mikono naada ya ajali.
6. Matatizo sugu ya uti wa mgongo k**a vile maumivu ya mgongo, shida kukunja mgongo au shida ya kutembea.

Kwa mawasiliano zaidi piga namba 0623140254

31/01/2020

KLINIKI YA USHAURI WA MAGONJWA YA UPASUAJI
(SURGICAL CONSULTING CLINIC)

Imefunguliwa Mtwara, Shangani Magharibi Barabara ya Chuno - Masandube jirani na hosteli za Mama Mpini.

Muda wa kazi:
Jumatatu - Ijumaa (Saa mbili kamili asubuhi mpaka saa kumi kamili jioni)

HUDUMA ZITOLEWZO
1. Utambuzi wa Magonjwa ya upasuaji na daktari bingwa wa magonjwa ya Upasuaji kwa kutumia vipimo vifuatavyo:
- Ultrasound
- Kipimo cha moyo (ECG)
- Kipimo cha kuangalia njia ya mkojo
- Kipimo cha kuangalia njia ya haja kubwa
- Kipimo cha kutoa kinyama kwa uchunguzi wa magonjwa ya kansa (yaani Biopsy (Bayopsi))

2. Mapasuaji Madogo mfano:
- Kukata na kupima vinyama vinavyohisiwa kuwa ni kansa (Excisional and True cut needle Biopsy)
- Kukata na kuondoa mabadiliko madogo ya ngozi
- Kushona vidonda vidogo vidogo

3. Huduma zingine za kitabibu mfano malaria, U.T.I, kisukari, uchunguzi ukeni, upungufu wa damu, figo n.k

Address

P. O. BOX MTWARA
Mtwara
568

Telephone

+623140254

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Surgical Clinic Mtwara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram