Njombe RRH

Njombe RRH Ukurasa Rasmi wa Hospitali ya
Rufaa Mkoa wa Njombe
59017 Ramadhani -Njombe
P. O Box 1044 Njombe

‎TUNATAKA NJOMBE RRH IWE KINARA WA HUDUMA BORA, NYANDA ZA JUU KUSINI - BALOZI MPUMILWAMwenyekiti wa Bodi ya Ushauri, Hos...
06/02/2026

‎TUNATAKA NJOMBE RRH IWE KINARA WA HUDUMA BORA, NYANDA ZA JUU KUSINI - BALOZI MPUMILWA

Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Balozi Danford Mpumilwa amesema Bodi ya Ushauri na Timu ya Uendeshaji wa Hospitali (RRHMT) watashirikiana kuhakikisha Njombe RRH inaboresha huduma zake hadi kuwa Kinara wa huduma bora Nyanda za Juu Kusini. ‎ ‎ ‎

Balozi Mpumilwa ameyasema hayo leo Ijumaa, Februari 6, 2026 aliposhiriki Kikao cha Maandalizi ya Bajeti ya Hospitali kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 kinachofanyika Halmashauri ya Mji Njombe. ‎ ‎

Amesema kuwa k**a Bodi wanao wajibu wa kuendelea kujenga mahusiano mazuri baina ya Taasisi, wananchi, na wadau wa maendeleo kwa kuwa sehemu ya Utatuzi wa changamoto ambazo zinaweza kuwa kikwazo cha kukwamisha utoaji wa Huduma bora, mathalani amesema Bodi imeanza mazungumzo na wadau mbalimbali kuhakikisha wanachangia katika utekelezaji wa Bajeti ya Hospitali ili iweze kuwa Bajeti inayotekelezeka.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Dkt. Gilbert Kwesi amesema utekelezaji wa Bajeti pendekezwa utakwenda kutatua changamoto mbalimbali katika utoaji huduma k**a vile;- uimarishwaji zaidi wa huduma za Kibingwa kwa kuongeza manunuzi ya vifaatiba vya kisasa, Malipo ya Motisha na Stahiki za watumishi, kuwajengea uwezo watumishi na kuwapeleka masomoni, ukarabati wa miundombinu na Upanuzi wa Huduma za Tiba na Huduma saidizi.

Kikao cha Maoteo ya Awali kuiendea Bajeti ya Hospitali, kimefanyika kwa siku nne kikihusisha wakuu wa Idara na Vitengo, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WOTE NI ENDELEVU – DKT. MFANGAMganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Juma Mfanga amesema kuwa Elimu ya...
27/01/2026

ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WOTE NI ENDELEVU – DKT. MFANGA

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Juma Mfanga amesema kuwa Elimu ya Bima ya Afya kwa wote inapaswa kuwa endelevu ili kuleta matokeo yaliyokusudiwa na serikali.

Akizungumza jana jioni Januari 26, katika Kikao chake na Menejimenti ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, amesema kuwa ipo haja kubwa ya Uongozi wa Hospitali kupitia wakuu wa Idara na vitengo, kuwafikishia watumishi walio chini yao Elimu ya Bima ya Afya kwa wote, ili kuendana na kasi ya Utekelezaji wa mpango huo ambao umeanza rasmi hapo jana.

Miongoni mwa sababu zilizotajwa kuchangia uanzishwaji wa Bima ya Afya kwa wote ni pamoja na kuwezesha malengo ya kisera, k**a vile kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi yaani vifo vya mama na mtoto, kutengeneza uwiano katika utoaji huduma kwa kujumuisha makundi maalumu k**a vile Watoto, wajawazito, wasio na uwezo, na wazee;Ujumuishaji wa huduma za magonjwa yanayochangia/kusababisha vifo na madhara makubwa ya kiafya kwa haraka.

Menejimenti ya Njombe RRH ilipitishwa katika maeneo mbalimbali ikiwemo utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote,namna mifumo ya TEHAMA itakavyotakiwa kufanya kazi kuanzia Ngazi ya Afya ya Msingi hadi Taifa kwa kusisitiza kuwa mifumo hiyo lazima iboreshwe na ikiwezekana uwepo mfumo mmoja ambao utasaidia kusomana kwa Taarifa kuanzia Zahanati hadi Hospitali ya Taifa, ikiwa ni agizo la Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa,kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za Afya; mfano upatikanaji wa dawa za kutosha, kuimarisha mifumo ya Tiba mtandao (Telemedicine) pamoja na utaratibu wa Rufaa.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Gilbert Kwesi amesisitiza wakuu wa Idara na Vitengo kushusha elimu hiyo kwa watumishi waliopo chini yao, pamoja na kuagiza Mratibu wa Mafunzo na Tafiti kuandaa kipindi ambacho kitasaidia kutoa elimu kwa watumishi wote kuhusu Bima ya Afya kwa wote.

Kupitia Bima ya Afya kwa wote Kaya yenye watu wasiozidi sita (6) wataweza kufaidika na huduma ya matibabu kwa gharama ya 150,000/= kwa mwaka.

BIMA YA AFYA KWA WOTE SHILINGI 150,000 KWA KAYA, WASIO NA UWEZO KUGHARAMIWA NA SERIKALINa WAF - DodomaSerikali imetangaz...
23/01/2026

BIMA YA AFYA KWA WOTE SHILINGI 150,000 KWA KAYA, WASIO NA UWEZO KUGHARAMIWA NA SERIKALI

Na WAF - Dodoma

Serikali imetangaza rasmi kuanza utekelezaji wa Bima ya Afya kwa wote awamu ya kwanza kwa kundi la wananchi wasio na uwezo (wazee, watoto, wajawazito na walemavu) ambao watagharamiwa na Serikali pamoja na kutangaza kitita cha huduma muhimu kitakachotolewa na skimu za Bima ya Afya kwa gharama ya Shilingi 150,000 kwa Kaya ya watu wasiozidi 6.

Hayo yamesemwa Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Januari 23, 2026 Jijini Dodoma kwenye kikao cha kujadili utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote na Viongozi na Watendaji ngazi ya Mikoa, Wilaya pamoja na Serikali za Mitaa.

Wazir Mchengerwa ametangaza kuanza rasmi kwa Bima ya Afya kwa wote Januari 26, 2026 na kuwataka watendaji kuhakikisha wananchi wanapata elimu kabla ya kujiunga na huduma bora za afya kuendelea kutolewa kwa wananchi wakiwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kote nchini.

Waziri Mchengerwa amesema kuwa kwa gharama ya Shiligni 150,000 watu 6 walio kwenye kaya moja watajiunga na Bima ya Afya kwa wote kwa itakayojumuisha mwanachama mchangiaji, mwenza wa mwanachama na wategemezi wanne (4).

“Wategemezi hao wanne wanaweza kuwa ni mzazi wa mwanachama au mzazi wa mwenza wa mwanachama; mtoto wa mwanachama wa kuzaa, kuasili au wa kambo aliye na umri chini ya miaka ishirini na moja au ndugu wa damu wa mwanachama aliye na umri wa chini ya miaka ishirini na moja” amefafanua Waziri Mchengerwa.

Amesema kuwa kitita cha Huduma Muhimu kitatolewa kwa kuzingatia utaratibu wa rufaa katika vituo vya kutolea huduma za Afya vitakavyoingia Mkataba na skimu za Bima ya Afya.

Waziri Mchengerwa amesema ili kufikia azma ya uhakika wa matibabu kwa wananchi wote kupitia Bima ya Afya Viongozi na Watendaji hawana budi kuhakikisha kuwa elimu sahihi inawafikia wananchi waweze kujua umuhimu wa kuwa na Bima ya Afya.

Fuatilia katika Vyombo vya Habari ikiwemo TBC na kurasa za mitandao ya kijamii ili kushuhudia Jukwaa la Uwekezaji wa Viw...
19/01/2026

Fuatilia katika Vyombo vya Habari ikiwemo TBC na kurasa za mitandao ya kijamii ili kushuhudia Jukwaa la Uwekezaji wa Viwanda vya Dawa Tanzania

FUATILIA MUBASHARA
19/01/2026

FUATILIA MUBASHARA

13/01/2026

Pata kufahamu huduma za Kliniki ya Pua, Koo na Sikio

Daktari, Elionora Sitta kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe leo Januari 13 anatupitisha katika moja ya Huduma za Kliniki hiyo, yaani Dondoo kuhusu Sikio.



05/01/2026

Bw. Eusebius Mbilinyi kutoka Halmashauri ya Madaba amefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe baada ya Taarifa iliyosambazwa katika kurasa za Mitandao ya kijamii za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kutangazwa kwa mwananchi aliyefikishwa akiwa Mahututi kisha kuhudumiwa kwa siku 42 pasipo ndugu zake kujitokeza baada ya kufikishwa na watu wema akiwa mahututi.

Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe unaungana na wazazi, ndugu, jamaa na Marafiki wa Steven Eusebius Mbilinyi (anayetibiwa) kwa jamii, na wananchi wema waliosambaza taarifa hii iliyofanikisha kupatikana kwa ndugu zake.

Mungu awabariki na akawakumbuke.

Asante.

01/01/2026
TAARIFA KWA UMMA
30/12/2025

TAARIFA KWA UMMA

IDARA YA WATOTO WAFANYA TATHMINI YA KUFUNGA MWAKAIdara ya Watoto kwa kushirikiana na Idara nyingine za Hospitali ya Rufa...
30/12/2025

IDARA YA WATOTO WAFANYA TATHMINI YA KUFUNGA MWAKA
Idara ya Watoto kwa kushirikiana na Idara nyingine za Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe imefanya hafla fupi leo Disemba 30 ya kujifanyia tathmini katika Utoaji hudumakwa mwaka 2025, ambapo wale waliofanya vizuri katika maeneo mbalimbali wamepata zawadi ikiwa ni sehemu ya motisha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni Rasmi, Kamu Mganga Mfawidhi, Dkt. Lazaro Jassely ameipongeza Idara hiyo kwa kuwa moja ya Idara zilizofanya kazi kwa mafanikio makubwa kwa mwaka 2025.

Amesema ushirikiano uliopo miongoni mwa watumishi katika Idara hiyo unapaswa kuigwa na Idara nyingine za Hospitali ili kuendelea kuboresha hali ya utoaji huduma.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara hiyo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto, Mariam Gaitani, ameomba ushirikiano ulioonyeshwa na Idara nyingine kwa Idara hiyo ubaki kuwa endelevu, huku akiahidi kuwa 2026 utakuwa mwaka wa huduma bora zaidi.

Watumishi wa idara ya watoto waliofanya vizuri katika eneo la uongozi, ukusanyaji wa mapato na Huduma bora kwaMteja walipatiwa zawadi.
Aidha Idara ilitoa zawadi kwa vitengo na Idara nyingine zilizipo hapa hospitali ikiwa ni shukrani na ushirikiano mzuri wanaoipatia idara ya watoto.

Katika hafla hiyo, wakuu wa Idara pia na watumishi mbalimbali wameshiriki kwa kula keki ya pamoja k**a ishara ya kuendeleza ushirikiano na Idara hiyo.

Viongozi na wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Consolata Ikonda, wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe le...
23/12/2025

Viongozi na wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Consolata Ikonda, wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe leo Desemba 23, 2025 na kujionea hali ya utoaji Huduma katika jengo la Huduma za Afya ya Mama na Mtoto ambapo pia wamepata wasaa wa kubadilishana uzoefu na kushauriana na wataalamu wenyeji katika maeneo hayo.

Timu ya wataalamu hao imeongozwa na Elide Ambrositte ambaye aliongozana na Timu ya Wauguzi, na Madaktari kutoka Hospitali hiyo iliyopo wilaya ya Makete.

Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi, Edward Mhina, amepongeza uamuzi uliofanywa na wataalamu hao huku akiahidi pia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kuendeleza ushirikiano ambao umekuwepo na Hospitali ya Ikonda, hasa katika maeneo ya kujengeana uwezo, kushiriki uzoefu ili kuendelea kuboresha hali ya utoaji huduma za afya kwa watanzania.

Kiongozi wa msafara huo wa wataalamu kutoka Ikonda, Bi. Ambrositte, amepongeza uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali katika eneo la Huduma za Afya ya Mama na Mtoto, ikiwemo wataalamu wa kutosha na miundombinu ya kisasa k**a vile vifaa na dawa; ambapo amesisitiza ipo haja kubwa ya kuendeleza ushirikiano miongoni mwa wataalamu ili kujengeana ujuzi na kubadilishana uzoefu baina ya Taasisi hizo mbili.

CALL FOR EXPRESSION OF INTEREST (EOI)
20/12/2025

CALL FOR EXPRESSION OF INTEREST (EOI)

Address

Mgodechi/Ramadhani Njombe Mjini
Njombe
59107

Telephone

+255678888654

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Njombe RRH posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Practice

Send a message to Njombe RRH:

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram