06/02/2026
TUNATAKA NJOMBE RRH IWE KINARA WA HUDUMA BORA, NYANDA ZA JUU KUSINI - BALOZI MPUMILWA
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Balozi Danford Mpumilwa amesema Bodi ya Ushauri na Timu ya Uendeshaji wa Hospitali (RRHMT) watashirikiana kuhakikisha Njombe RRH inaboresha huduma zake hadi kuwa Kinara wa huduma bora Nyanda za Juu Kusini.
Balozi Mpumilwa ameyasema hayo leo Ijumaa, Februari 6, 2026 aliposhiriki Kikao cha Maandalizi ya Bajeti ya Hospitali kwa mwaka wa Fedha 2026/2027 kinachofanyika Halmashauri ya Mji Njombe.
Amesema kuwa k**a Bodi wanao wajibu wa kuendelea kujenga mahusiano mazuri baina ya Taasisi, wananchi, na wadau wa maendeleo kwa kuwa sehemu ya Utatuzi wa changamoto ambazo zinaweza kuwa kikwazo cha kukwamisha utoaji wa Huduma bora, mathalani amesema Bodi imeanza mazungumzo na wadau mbalimbali kuhakikisha wanachangia katika utekelezaji wa Bajeti ya Hospitali ili iweze kuwa Bajeti inayotekelezeka.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe, Dkt. Gilbert Kwesi amesema utekelezaji wa Bajeti pendekezwa utakwenda kutatua changamoto mbalimbali katika utoaji huduma k**a vile;- uimarishwaji zaidi wa huduma za Kibingwa kwa kuongeza manunuzi ya vifaatiba vya kisasa, Malipo ya Motisha na Stahiki za watumishi, kuwajengea uwezo watumishi na kuwapeleka masomoni, ukarabati wa miundombinu na Upanuzi wa Huduma za Tiba na Huduma saidizi.
Kikao cha Maoteo ya Awali kuiendea Bajeti ya Hospitali, kimefanyika kwa siku nne kikihusisha wakuu wa Idara na Vitengo, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.