Dr. Nyonyo

Dr. Nyonyo Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Dr. Nyonyo, Medical Center, NJIA PANDA-MOSHI, Old Moshi.

12/05/2017

: TATIZO LA HARUFU MBAYA MDOMO NA JINSI YA KUEPUKANA NALO.

Dalili nyingine za maradhi ni pamoja na kuonekana kwa sehemu ndogo zenye rangi nyeupe ndani ya kinywa, kupasuka kwa midomo, midomo kuongezeka ukubwa, hisia za kukwama kwa chakula kwenye koo, kuvimba kwa fizi, ladha ya chakula kubadilika na pumzi yenye kutoa harufu.

Kwa watu ambao kinga kinga ya mwili imeshuka, maradhi haya huweza kusambaa kutoka kwenye kinywa na kushuka kwenye koo la chakula mpaka kufikia kwenye tumbo.

Hii inapotokea, mgonjwa hupata maumivu wakati wa kumeza chakula.
Dalili za hatari ni mgonjwa kupata homa kali ikiambataan na kutetemeka mwili na kushindwa kabisa kumeza chakula.

Mgonjwa akifikishwa hospitali maradhi haya hutambulika kirahisi kutokana na dalili zake kuweza kutambukiwa kwa kuangalia kwa macho.

Matibabu ya maradhi haya hutegemea na kilichosababishwa. Iwapo kilichosababisha kinaweza kuepukwa au kutibika, basi nayo yataisha, k**a mtu ameyapata kutokana na kuugua kisukari, ni vyema akakitubu kisukari kwanza.

Watoto wachanga hawahitaji matibabu ya aina yeyote k**a dalili zitaanza kuisha kabla ya wiki nne hazijaisha.

12/05/2017

TATIZO LA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA MDOMONI

Tatizo la kunuka kinywa, huwasibu watu wengi, na huwa kero
kubwa kwa waliokaribu na mwenye tatizo hili. Mara nyingi mwenye tatizo hili huwa hafahamu, na wengi huona vibaya kumweleza mtu mwingine kuwa kinywa chake kinatoa harufu. Na wenye tatizo hili pia wakifahamu hupata mfadhaiko sana wa mawazo, na kutopenda kuongea kwenye kusanyiko la watu kwa kuhofia kuwakera wanaomsikiliza. Tatizo hili linaweza kupatiwa ufumbuzi iwapo mwenye tatizo atafahamishwa na hivyo kutafuta tiba stahiki.

Kunuka kinywa ni nini?

Harufu mbaya kutoka kinywani hutokana na kutoa pumzi inayonuka vibaya ambayo huweza kunuswa na wanaokuwa karibu na mwenye tatizo hili. Pia hii hujulikana kwa lugha ya kigeni k**a “halitosis”. Harufu hii inaweza kutokea mara kwa mara, au inaweza kudumu kwa muda mrefu, kutegemeana na chanzo chake.

Dalili za kutoa harufu mbaya kinywani

Dalili za kuwa na harufu mbaya kinywani huwa zinahisiwa na wale wanaokuwa karibu na mwenye tatizo hili. Mwenye tatizo hili mara nyingi anakuwa ameshaizoea ile hali, hivyo hawezi kuhisi hiyo harufu. Harufu hii huwa kero kwa waliokuwa karibu, wakati mwingine unaona k**a watu wanagusa-gusa pua zao, wanasogeza nyuso zao mbali au kuonyesha kwa mbali (bila kuwa dhahiri sana) dalili ya kukunja uso k**a wanakerwa na jambo fulani.

Chanzo cha harufu mbaya kinywani na dalili zake

Harufu mbaya kinywani inaweza kusababishwa na

Tatizo kinywani au
Tatizo nje ya kinywa
Vyakula au vinywaji vinavyoacha harufu kinywani

Chanzo cha kufikirika (psychological)

Tatizo la hisia tu (kufikirika tu bila kuwa na uhalisia)

1. Tatizo kinywani

Kinywa ni makao ya mamilioni ya bakteria ambao hukaa k**a makazi yao, na sehemu kubwa wanakopatikana kwa wingi ni kwenye ulimi. Bakteria hawa huwa chanzo kikubwa cha harufu mbaya kutoka kinywani kwa watu walio wengi. Kwa kawaida kinywa huweza kutoa harufu ambayo siyo ya kukera, na inakubalika kuwa ni ya kawaida, mfano asubuhi kinywa hutoa harufu ambayo huondoka mara moja baada ya kupiga mswaki au hata kusukutua kwa maji tu. Harufu hii hutokana na kuwa unapokuwa umelala, na kinywa kimefungwa, mate hupungua sana kinywani, hivyo hufanya mazingira haya kuwa mazuri kwa bakteria kuzaliana na kuongezeka kwa kiwango kikubwa na pia kutoa muda kwa bakteria kumeng’enya mabaki ya chakula kinywani na kuleta harufu mbaya kinywani. Hali hii huwa tofauti wakati wa mchana, maana mate hutengenezwa kwa wingi katika hali ya kawaida na kusaidia kusafisha na kuondoa mabaki ya chakula, na kuzuia harufu kinywani.

Harufu hii ikianza kuwa mbaya na ya kukera watu wengine karibu yako ndipo huangaliwa k**a tatizo linalohitaji matibabu. Harufu inayodumu kuwa mbaya na ya kukera huweza kusababishwa na

1.1 Chanzo: Ugonjwa wa fizi

Picha hii inaonyesha ugaga (dental calculus) na ugavu (dental plaque) uliotanda kwenye meno karibu na fizi, na fizi zilizoshambuliwa na kulika kutokana na ugonjwa wa fizi

Ugonjwa wa fizi husababishwa na utando wa uchafu unaoitwa ugavu (dental plaque). Uchafu huu ukiongezeka kwa wingi, husababisha ufizi kushambuliwa, kupoteza ubora wake na kuwa laini, mishipa midogo ya damu kwenye fizi huwa na vidonda vidogo vidogo (ulceration) na kuvuja damu kwa urahisi, fizi zinaachia nafasi kati yake na jino, chakula kinakaa, na pia fizi husinyaa (hurudi nyuma) na kuacha wazi sehemu ya jino inayopaswa kufunikwa na hivyo kuleta ukakasi wa meno. Ugavu ukikaa kwa muda mrefu bila kuondolewa hutengeneza ugaga (dental calculus). Ugavu (dental plaque) huwa na mamilioni ya bakteria, ambao humeng’enya mabaki ya chakula na kusababisha harufu mbaya kutoka kinywani.

Dalili:

• Ufizi kutoa damu kwa urahisi ukiguswa na kitu chochote hata mswaki, kutafuna vitu k**a mkate mkavu, mua, matunda k**a peasi, mapera n.k.

• Usaha kutoka kwenye fizi kati ya meno, au uvimbe wenye usaha pembeni ya jino

• Meno kulegea kutokana na mfupa unaoshikilia jino kumomonyoka kwa ndani

• Harufu mbaya kutoka kinywani

1.2 Chanzo: Ugonjwa wa kuoza kwa meno

Picha inaonyesha meno yenye matundu au yaliyooza, mabaki ya chakula yanaweza kuhifadhiwa kwenye matundu hayo, kuoza, na kutoa harufu

Meno yakitoboka, huweka nafasi ambayo chakula huweza kukaa, na hakiondoki kwa urahisi wakati wa kupiga mswaki. Humo kwenye matundu yaliyoko kwenye meno chakula hicho hushambuliwa na bacteria na hivyo kukiozesha na kuchangia harufu mbaya mdomoni.

Dalili

• Meno yaliyotoboka na yamejaa mabaki ya chakula

• Maumivu ya meno yaliyotoboka

• Maumivu wakati wa kutafuna, au kunywa kitu cha moto au cha baridi

• Jino lililooza kubadilika rangi

• Harufu mbaya kinywani

1.3 Chanzo: Ugonjwa wa kupungua mate kinywani (xerostomia)

Tatizo hili husababishwa na mambo mbali mbali, ikiwemo matumizi ya madawa ya aina mbali mbali mara kwa mara. Madawa mengi husababisha mate kupungua kinywani. Pia magonjwa yanayoshambulia tezi za mate hupunguza mzunguko wa mate kinywani. Mate yana vitu vinavyozuia bakteria kuleta madhara kinywani. Hivyo mate yanapopungua kinywani, hutoa nafasi ya wazi kabisa kwa bakteria walioko kinywani kufanya kazi kwa uhuru zaidi bila kipingamizi ambapo humeng’enya mabaki ya vyakula na kutoa harufu mbaya kinywani

Dalili

• Shida ya kumeza chakula. Chakula kikavu kinakuwa k**a kinakwangua koo la chakula wakati wa kumeza

• Shida ya kuongea kwa muda mrefu kwa sababu ya kinywa kuwa kikavu

• Hisia ya kuwaka moto kinywani

• Kuwa na dalili ya meno mengi kutoboka kwa mara moja

• Kuhisi ukavu kwenye macho

• Harufu mbaya kinywani

1.4 Chanzo: Kutokupiga mswaki vizuri

Picha: Ulimi kuweka mgando mweupe

Kutokupiga mswaki vizuri hupelekea ugavu (dental plaque) kubaki kinywani pamoja na mabaki ya chakula kuwa yamejishika katikati ya meno na hivyo kuoza na kutoa harufu mbaya. Pia mabaki ya ugavu (dental plaque) kwa muda mrefu kwenye meno hupelekea kusababisha ugonjwa wa fizi

Dalili

• Meno kuwa na mgando wa ugaga (dental calculus) wenye rangi ya njano au kijivu, hasa maeneo yanayozunguka ufizi

• Kutoka damu kwa urahisi kwenye fizi hasa wakati wa kupiga mswaki ikiwa hali hii imekuwa ya muda wa siku kadhaa

• Ulimi kuweka mgando mweupe,

• Ulimi ukipitishwa kuzunguka kwenye meno, kunakuwa na hisia za kukosa wororo (sensation of roughness)

• Kutoa harufu mbaya mdomoni

1.5 Kutokusafisha meno ya bandia vizuri

Meno ya bandia ya kuvaa na kuvua (removable partial denture), yanaweza kuhifadhi mabaki ya chakula na ugavu (dental plaque) ambayo hupelekea kutoa harufu yasiposafishwa k**a inavyoelekezwa.

Dalili

• Meno haya huweza hata kusababisha ugonjwa humo humo kinywani unaojulikana k**a “denture stomatitis”, hali ambayo hufanya sehemu zinafunikwa na hayo meno kuvimba, kutoa damu kwa urahisi, na wakati mwingine kuuma na kutoa harufu.

• Pia meno ya bandia ya kugandisha (fixed prosthesis), yakiacha nafasi inaweza kuhifadhi mabaki ya chakula ambacho kikioza huchangia kutoa harufu mbaya mdomoni.

• Ufizi au paa la kinywa (palate) kuvimba na kuuma

2. Tatizo nje ya kinywa

2.1 Chanzo: Magonjwa yanayoathiri mfumo wa hewa

Magonjwa haya yanaweza kuwa kwenye mapafu, kwenye koo, au kwenye uwazi kwenye fuvu la taya unaoitwa “maxillary sinus”. Magonjwa haya yanaweza kusababisha kuongezeka kwa majimaji ambayo yakipata maambukizi hupelekea kutoa harufu mbaya kupitia kinywani

Dalili

• Kuvimba tezi za kinywani

• Kuvimba kooni kunaambatana na maumivu ya kumeza kitu chochote (sore throat)

• Homa kali

• Pua kuziba

• Kutoa mak**asi yenye rangi ya kijani au njano

• Kikohozi kinachoambatana na makohozi

2.2 Chanzo: Magonjwa mengine

Ugonjwa wa kisukari, magojwa yanayoathiri maini,magonjwa ya figo kushindwa kufanya kazi, magojwa yanayoathiri mfumo wa chakula (reflux diseases)

Dalili

• Dalili za ugonjwa wa kisukari: pamoja na hayo mtu huyu hutoa harufu k**a ya matunda kutoka mdomoni mwake

• Dalili za magonjwa ya figo kushindwa kufanya kazi: pamoja na hayo mtu huyu hutoa harufu k**a ya mkojo kutoka mdomoni mwake

• Dalili za magonjwa ya ini, kinywa hutoa harufu inayofanana na harufu ya mtu aliyekunywa pombe anapoamka wakati wa asubuhi

• Dalili za magonjwa ya mfumo wa chakula

3. Ulaji/utumiaji vitu vinavyotoa harufu kinywani

Mfano kula vitunguu (vya kawaida na vitunguu saumu), kutumia kahawa, kuvuta sigara, matumizi ya ugoro, matumizi ya pombe na mvinyo.

Dalili

• Harufu inayofanania na kitu kilichotumika/kinachotumika mara kwa mara mfano vitunguu, kahawa, sigara, ugoro, pombe au mvinyo n.k.

4. Tatizo la kufikirika (psychological/psychiatric illness)

Watu wengine wanakuwa wanaamini kuwa vinywa vyao inatoa harufu mbaya, hali ambayo watu wanaomzunguka hawajawahi kuhisi harufu hiyo kutoka mdomoni. Hali hii ni tatizo la kisaikolojia ambalo mgonjwa anahitaji ushauri nasaha kutoka kwa wataalamu wa saikolojia.

Dalili

• Dalili kubwa ni kuwa hakuna harufu yoyote utakayoisikia kutoka kwa mgonjwa huyu, pia ukimchunguza mdomoni, hana tatizo lolote linalosababisha harufu mbaya mdomoni, na hana historia ya ugonjwa wowote unaoweza kusababisha harufu mbaya kinywani

• Katika mazungumzo mtu huyu huonekana kuongelea mambo mengine ambayo hayana mahusiano sana na tatizo lake, pia huweza kuwa na historia ya kuona madaktari wa aina mbalimbali kwa ajili ya tatizo hili bila kupata suluhisho.

Matibabu ya harufu mbaya Kinywani

Unashauriwa kumwona daktari wa afya ya kinywa k**a una tatizo hili au daktari anaweza kugundua jambo hili unapoenda kwa matibabu ya tatizo lingine. Daktari atashirikiana na wewe ili kuweza kujua chanzo cha tatizo kwa ajili ya kulitibu. K**a inavyoonekana hapo juu, ili kutatua tatizo hili inabidi kutibu chanzo cha tatizo.

Namna ya kuzuia tatizo la harufu mbaya kutoka mdomoni

1. Harufu mbaya kutokanana matatizo ya kinywani yanaweza kuzuiliwa kwa urahisi kwa kupiga mswaki kwa usahihi na kusafisha ulimi pia.

2. Meno yaliyo na matundu kuzibwa.

3. Kusafisha meno ya bandia kila baada ya kula, na kuyahifadhi ndani ya maji (kwenye glass au chombo chochote utakachokiandaa) usiku unapoenda kulala katika chombo safi. Kutumia brashi maalumu kutoa chakula kinachojikusanya juu ya jino/meno yaliyogandishwa (k**a yameacha nafasi inayohifadhi chakula).

4. Kufanya uchunguzi wa kinywa na kusafisha meno angalau mara mbili kwa mwaka.

5. Kunywa maji ya kutosha kila siku ili kuupa mwili wako uwezo wa kutengeneza mate ya kutosha

6. Kutumia bazooka isiyokuwa na sukari inasaidia kuhamasisha mate kutengenezwa mdomoni.

7. Kutumia dawa ya kusukutua utakayoshauriwa na daktari wa afya ya kinywa (epuka matumizi holela ya dawa za kusukutua maana zinapatikana kwa urahisi maduka ya dawa, ni vyema ukatumia dawa hii baada ya kumwona daktari wa afya ya kinywa k**a ataona unahitaji atakushauri).

8. K**a chanzo cha tatizo la harufu mbaya ni nje ya kinywa mfano kutokana magonjwa mengine, basi matibabu sahihi ya magonjwa husika yatasaidia kuzuia tatizo hili.

09/05/2017
Usikubali kinywa chako kiaribike. Onana na Dr. Nyonyo upaate dawa.piga sim: 0769 755 505
09/05/2017

Usikubali kinywa chako kiaribike. Onana na Dr. Nyonyo upaate dawa.
piga sim: 0769 755 505

04/05/2017

YANAYOSABABISHA MDOMO KUTOA HARUFU MBAYA.

Kwa ufupi

Kwa kawaida mdomo na pua hutoa pumzi nje ambayo huwa na harufu asilia ambayo haiwezi kumkera mtu mwingine, lakini mara nyingine hali hiyo inaweza kujitokeza kwa mtu kutoa pumzi yenye harufu mbaya.

Katika maisha ya kila siku inawezekana umewahi kukutana na mtu ambaye ukiwa karibu naye kimazungumzo, utagundua anatoa harufu mbaya mdomoni.

Kwa kawaida mdomo na pua hutoa pumzi nje ambayo huwa na harufu asilia ambayo haiwezi kumkera mtu mwingine, lakini mara nyingine hali hiyo inaweza kujitokeza kwa mtu kutoa pumzi yenye harufu mbaya.

Pengine watu wa karibu au wanaokutana na mwathirika wa hali hii, wanaweza wakadhani mtu huyo ni mchafu mwenye na tabia ya kutopiga mswaki au kutosafisha kinywa chake vizuri.

Wengi hawajui kuwa mtu huyo anaweza kuwa na tatizo linalojulikana kitabibu kwa jina la halitosis, ambalo maana yake ni kutoa pumzi ama mdomoni au puani.

Mtu mwenye tatizo hili anaweza kukumbana na kunyanyapaliwa na wanajamii wanaomzunguka kiasi cha kuweza kumsababishia matatizo ya kisaikolojia.

Mwathirika anaweza kupata na tatizo la hofu iliyopitiliza anapokuwa katika jamii; anaweza akajinyofoa kutoka katika jamii na kujitenga na baadaye anaweza kupata sonona.

Ugonjwa wa halitosis

Karibu asilimia 20 ya watu duniani wanakumbwa na ugonjwa huu na hivyo kukimbilia kwa wataalamu wa afya ya kinywa.

Hufika kwa wataalamu hawa wakidhani wana magonjwa ya kinywa ikiwamo mashimo katika meno, kulika kwa meno, kuoza kwa meno na magonjwa ya fizi.

Ukweli ni kuwa si wagonjwa wote wenye kutoa pumzi yenye harufu mbaya wana tatizo halisi la halitosis, kati ya asilimia tano hadi 72 wanaofika katika huduma za afya hugundulika kuwa hawana tatizo hili moja kwa moja.

Tatizo la kutoa pumzi yenye harufu mbaya ambalo ndiyo ugonjwa halisi, linasababishwa na uwapo wa mrundikano wa bakteria katika uvungu wa fizi na nyuma ya ulimi karibu na koo.

Kinywa kwa ujumla, kikijumuisha meno, fizi, ulimi na vifuko vya mate kinaweza kuwa ni maficho mazuri kwa mamia ya bakteria. Ndiyo maana inaaminika tatizo la harufu mbaya mdomoni ni kinywa chenyewe.

Kinywani pekee kuna karibu jamii 600 za bakteria ambao huambatana na mabaki ya vyakula tunayokula kila siku. Kuwapo kwa protini ya kwenye mate na protini ya vyakula tunavyokula na uvunjwaji wa mabaki yake na bakteria waliopo mdomoni, ni chanzo cha kuwapo kwa harufu mbaya.

Mabaki ya protini mdomoni ambayo huvunjwavunjwa na bakteria na kuwa tindikali ya amino na hapo baadaye inapovunjwa, hutoa gesi yenye harufu mbaya.

Mfano mzuri ni pale protini ijulikanayo k**a methionine na cysteine inapovunjwavunjwa kinywani na hivyo kutoa gesi yenye harufu mbaya ijulikanayo k**a Hydrogen sulphide.

Mara nyingi harufu ya kinywa inaweza kuwa nzito zaidi baada ya mtu kuamka. Hii ni kwa sababu wakati wa kulala mdomoni kunakuwa na kiasi kidogo cha hewa ya oksijeni.

Bakteria waliopo mdomoni ni wale wasiohitaji uwepo wa hewa ya oksijeni hivyo kipindi cha usiku tukiwa tumelalala, ndipo huvunjavunja mabaki ya chakula ambayo huambatana na kutolewa gesi zenye harufu mbaya.

Vilevile harufu ya kinywa inaweza kubadilikabadilika kutokana na vyakula tunavyokula ikiwamo vitunguu maji, vitunguu swaumu, hiliki, tangawizi na pia uvutaji sigara na unywaji wa pombe.

Hivyo siyo mara zote kupumua harufu isiyo ya kawaida ni ugonjwa; mara nyingine inakuwa ni tatizo la muda tu lililochangiwa na vyakula na matumizi mengine ya vitu.

Asilimia 10 zilizobaki, mara nyingi husababishwa na matatizo mengine ikiwamo magonjwa ya kooni, puani, shambulizi za nyufa za mifupa iliyopo usoni, magonjwa ya mfumo wa chakula, magonjwa katika mapafu, magonjwa ya masikioni na madhara ya ugonjwa sugu wa mafindofindo.

Vilevile kuwapo kwa majipu ya fizi au meno, vidonda mdomoni au michubuko, vidonda vya kooni na maambukizi ya virusi vya herpes simplex na HPV. Mara chache pia tatizo hili linaweza kuchangiwa na magonjwa ya ini ikiwamo kuharibika kwa ini na majipu katika ini.

Mara nyingine wanaoshtakia tatizo hili hubainika kuwa na tatizo la usafi wa kinywa. Na wanaposhauriwa kuboresha usafi wa kinywa kwa kutumia dawa za meno, au kusukutua na dawa maalumu za kusafisha kinywa nyuma ya ulimi, tatizo huisha haraka.

Tiba ya ugonjwa

Uchunguzi wa tatizo hili huanzia kwa mhusika mwenyewe kueleza historia ya tatizo, kisha wataalamu wa kinywa au daktari wa kawaida humchunguza kwa kumfanyia majaribio na vipimo kadhaa.

Baada ya wataalamu wa afya kubaini ugonjwa ndipo ushauri na matibabu huanza. K**a chanzo cha harufu mbaya ni maradhi ambayo si ya kinywani wataalam watakupa matibabu ya kutibu chanzo hicho.

K**a chanzo cha kutoa pumzi yenye harufu mbaya ni kinywa, wahudumu wa afya watamwelekeza mgonjwa mambo mbalimbali k**a ifuatavyo;

Kupiga mswaki katika ulimi mara mbili kwa siku kwa kutumia mswaki laini, kifaa k**a kijiko kwa ajili ya kukwangua uso wa ulimi. Pia kutumia dawa yenye kiambata cha kuua bakteria.

Ulaji wa kifungua kinywa chenye afya ikiwamo kula matunda na mboga za majani yenye nyuzi nyuzi, husaidia kusafisha kinywa eneo la nyuma ya ulimi wakati wa kumezwa.

Utafunaji wa bazoka unasaidia kuufanya mdomo usiwe mkavu na hewa ya oksijeni kuingia kinywani kwa wingi. Pia utafunaji wa bazoka unaweza kusaidia kutiririka kwa mate kwa wingi yanayosaidia kusafisha kinywa na kuua vimelea vya maradhi. Mdomo ukiwa mkavu na hautafuni chochote huchangia kujiimarisha kwa bakteria

Kusukutua kwa maji mengi ikiwezekana ya vuguvugu kila mara baada ya kula chakula na kabla ya kwenda kulala. Unaweza pia kutumia dawa maalumu za kusukutulia kinywa zenye dawa ya kuulia vimelea.

Jaribu kuboresha usafi wa kinywa kwa kuusafisha ulimi. Safisha meno kwa mswaki kila unapomaliza kula chakula, ondoa mabaki ya chakula yaliyojibana katika meno na fizi na safisha na sukutua kinywa chako kwa dawa maalumu kabla ya kulala.

Unaweza kutumia vitu asilia k**a majani ya minti na karafuu, k**a njia ya kupunguza kupumua hewa yenye harufu mbaya.

Ni vyema kufanya uchunguzi wa afya ya kinywa kila baada ya miezi sita, ili kuweza kubaini magonjwa mbalimbali ya kinywa mapema.

TUNATIBU MENO YALIYOOZA NA KUZUIA YASIOZE, MENO KUFA GANZI, FIZI KUTOA DAMU, FIZI KUVIMBA, KUTOA HARUFU MBAYA MDOMONI, V...
01/05/2017

TUNATIBU MENO YALIYOOZA NA KUZUIA YASIOZE, MENO KUFA GANZI, FIZI KUTOA DAMU, FIZI KUVIMBA, KUTOA HARUFU MBAYA MDOMONI, VIDONDA MDOMONI AU KWENYE ULIMI.
wasiliana na Dr Michael Nyonyo 0769 755505, 0656 878473 0622 755505

Unatatizo lakutokwa na harufu mbaya mdomoni?Tiba ipo kwa Dkt.Nyonyo 0769755505
29/04/2017

Unatatizo lakutokwa na harufu mbaya mdomoni?
Tiba ipo kwa Dkt.Nyonyo
0769755505

Kwa nini kinywa chako kiaribike wakati Dkt. Nyonyo yupo.?Tupigie simu: 0769755505
29/04/2017

Kwa nini kinywa chako kiaribike wakati Dkt. Nyonyo yupo.?
Tupigie simu: 0769755505

Address

NJIA PANDA-MOSHI
Old Moshi

Telephone

+255 769755505

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dr. Nyonyo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Share on Facebook Share on Twitter Share on LinkedIn
Share on Pinterest Share on Reddit Share via Email
Share on WhatsApp Share on Instagram Share on Telegram

Category